Barua ya Wazi Kwa Askofu Kakobe. Wafalme Hawakosolewi

DLaDLa

Member
Jul 8, 2012
10
10
Wafalme Hawakosolewi!!!!

Hakuna mfalme anayeweza kufanikiwa kutawala watu wa Mungu ikiwa yeye hana Mungu. Nikitumia Biblia kama kitabu cha rejea, watawala wengi sana wametajwa kushindwa au kuangamia kwa sababu hawakudumu katika maagizo ya Mungu.

Sauli alikuwa ni mfalme wa kwanza katika taifa la Uyahudi. Halikuwa kusudi la Mungu kuruhusu Wayahudi wawe na mfalme. Lakini Wayahudi walitaka kuwa na mfalme wafanane na mataifa mengine yenye wafalme wao.

Kabla ya wafalme, Mungu alikuwa ni mwamuzi wao. Lakini Wayahudi walitaka na wao wawe na wafalme ili wawaamulie. Mungu aliwaonya Wayahudi kwa kuwafunulia madhara ya wafalme. Haya ni baadhi ya madhara ambayo Mungu aliwaonya Wayahudi (1 Samweli 8:10-22):

 Mfalme atawatwaa watoto wenu ili wamtumikie
 Mfalme atawafanya watoto wenu wawe askari wa jeshi lake
 Mfalme atawatwaa mabinti zenu wamtumikie.
 Mfalme atatwaa mashamba yenu mazuri na mazao yake awape maakida wake
 Mfalme atawatoza ushuru ili awalishe watumishi na maakida wake
 Mfalme atawatoza fungu la kumi katika mapato yenu
 Nanyi mtalia sana mkijuta kuwa na mfalme mliyejichagulia wenyewe.

Hata hivyo Wayahudi walimtaka mfalme licha ya madhara hayo ambayo Mungu aliwaonya hapo mwanzo. Mungu akawapa Sauli kuwa mfalme wa kwanza wa Uyahudi.

Sauli alikuwa na shida yake kubwa iliyosababisha miisho yake mibaya. Cheo kile alipewa na Mungu lakini hakuhitaji busara ya Mungu akajiinua kwa hekima yake. Uovu ukamwingia akamkosea Mungu.

Sio kusudi langu kumzungumzia mfalme Sauli. Nia yangu ni mfalme Daudi, mrithi wake. Mfalme aliyepata kumpendeza Mungu kwa kiasi kikubwa sana.

Siku moja mfalme Daudi akiwa katika kasri yake, alimwona mwanamke mzuri sana kupitia dirishani. Mwanamke yule alikuwa ni mke wa Uria, mmoja wa askari wake waliokuwa vitani. Mfalme Daudi akamtamani mke wa Uria na akagizwa alatwe kwake.

Mfalme Daudi alifanya ngono na mke wa askari wake aliyekuwa vitani akimpigania! Kitendo kile kilipelekea mke wa Uria kupata ujauzito. Mfalme akaagiza Uria arudishwe nyumbani akiamini akija atalala na mkewe hivyo ataangushiwa jumba bovu juu ya ujauzito ule.

Hata hivyo Uria aliporudi alikataa kulala na mkewe akihoji kuwa ana furaha gani ya kulala na mkewe wakati askari wenzake wako vitani! Mpango huo wa mfalme Daudi ukafeli. Uovu ukazidi kumtafuna mfalme Daudi naye akaona ni heri kumwua Uria. Basi aliamuru askari yule arudi vitani huku akimtaka jemedari wa jeshi kumweka Uria kwenye mstari wa mbele wa mapambano. Mfalme Daudi alikusudia kusikia Uria akifia vitani.

Baada ya mapambano kuendelea, kweli Uria akafia vitani. Mfalme Daudi akapumua maana alijua sasa siri yake iko salama. Lakini kwa bahati mbaya mfalme Daudi alisahau kuwa Mungu alikuwa anaona uovu wake. Machoni pa watu mfalme Daudi alikuwa ni mtu mwema sana lakini alikuwa amemkosea Mungu na mwanadamu pia.

Dhambi yake ilikuwa ni kubwa sana na alistahili kufa. Ndipo Mungu alipomtuma Nathani kupeleka ujumbe kwa mfalme Daudi. Nathani alijua nguvu za wafalme. Nathani alijua wafalme hawapendi kukosolewa. Nathani alijua siku zote wafalme huamini kuwa wana uwezo mkubwa wa kutoa haki. Hivyo lilikuwa ni jambo la hatari sana kwa Nathani kumkosoa au kumwonya mfalme Daudi juu ya dhambi yake.

Nathani akaamua kumtupia mfalme Daudi kitanzi ili ajinyonge mwenyewe. Ndipo alipomsimulia kisa kilichopo katika kitabu cha Samweli wa Pili Sura ya kumi na mbili (2 Samweli 12:1ff). Nakusihi kabla ya kuendelea kusoma makala hii naomba usome sura niliyoitaja hapo juu ili ujue kile ambacho mfalme Daudi aliambiwa na Nathani mjumbe wa Mungu.

Jambo alilolifanya Nathani ndilo ambalo watumishi wa Mungu nchini wanapaswa kufanya. Wafalme wengi wanapenda sana kubarikiwa ila hawapendi kuoneshwa kuwa ni wakosaji mbele za watu wao maana watapoteza sifa ya kutawala. Ndio maana hata wakifanya makosa huwa hawataki yajulikane kwa watu wao maana kuishi kwao kunategemea watu! Mamlaka zao hazitakuwa na nguvu iwapo watapoteza imani kwa watu wao wanaowatawala.

Hivyo usitarajie kuwa unaweza kumkosoa mfalme hadharani na ukabakia salama. Huu ni utaratibu ambao uko tangu siku nyingi. Maana siku zote mfalme yuko sahihi! Kama si kwa kauli ya mfalme mwenyewe, basi maakida au watumishi wake watakushughulikia mara moja itakapobainika umejaribu kumkosoa mfalme maana kuishi kwao hutegemea hisani ya mfalme. Haya ndio Mungu aliyowaonya Wayahudi maana alijua desturi za wafalme.

Haki wanayosema wanaitoa si haki ya kweli bali ni haki yenye kuwatukuza wao zaidi. Si kweli watawaliwa wanaweza wasione uovu wa mfalme wao, lahasha! Wengi wanajua hatima yao iwapo watamkosoa mfalme hadharani.

Kwa jinsi hiyo, Mungu pekee ndiye hushughulika moja kwa moja na wafalme. Hata hivyo Mungu hawezi kuruhusu watu wake waumie kwa sababu ya uovu wa mfalme. Ipo njia itakayojitokeza katika kuwanusuru watu wake maana kilio cha wanyonge ni kelele kubwa sana mbele za Mungu.
Askofu Kakobe ulitakiwa utumie hekima ya Nathani katika kufikisha ujumbe wako kwa mfalme. Kile kinachoweza kukutokea kingeweza kumtokea pia Nathani kama angekifanya kama ulivyokifanya.

Uria yawezekana mpaka kufa kwake hakujua kwamba mfalme Daudi alizini na mke wake na kumpa ujauzito. Yawezekana Uria atastaajabu sana siku ya hukumu pale atakapo baini kuwa kufa kwake vitani haikuwa ushujaa wa kumpigania mfalme wake bali ilikuwa ni hukumu yake ili kuficha uovu wa mfalme anayemtumikia. Ni kweli wafalme hawakosolewi maana ni jambo wasilolipenda!

Ni mwenye akili pekee za kibinadamu ndiye anayeweza kunielewa! Wafalme hukosolewa kwa nguvu ya watu maana watu ndio huwapa mamlaka kwa niaba ya Mungu! ;);););)
 
Tunapochangia mada hii tusisahau pia kwamba Hakuna mfalme aliye Pendeza na wote, na Baadhi ya wakosoaji ni wale ambao wamekosa nafasi kufaidi kama walivyozoea Ktk tawala zilizotangulia wana hasira. Tumesahau makuhani hao walivyogawana mabilioni tegeta bila aibubona walikuwa hawakwmei.
Wakitaka wagharamie uchaguzi kesho waone huyo huyo wanayedhani anawatesa watu atapata asilimia ngapi!! Wakae madhabahuni watuache kama ni kuumia walishatuumiza na wao tumezoea acha tuumie zaidi.
Mie hadi nawashangaa!! Hivi wanatumia akili kweli.? Yaani hadi aibu, wakae kimya tu waone Nchi inavyonyoshwa watashangilia baadae tutakapokuwa tunaimba TUMEFIKA SALAMA!!
 
Tunapochangia mada hii tusisahau pia kwamba Hakuna mfalme aliye Pendeza na wote, na Baadhi ya wakosoaji ni wale ambao wamekosa nafasi kufaidi kama walivyozoea Ktk tawala zilizotangulia wana hasira. Tumesahau makuhani hao walivyogawana mabilioni tegeta bila aibubona walikuwa hawakwmei.
Wakitaka wagharamie uchaguzi kesho waone huyo huyo wanayedhani anawatesa watu atapata asilimia ngapi!! Wakae madhabahuni watuache kama ni kuumia walishatuumiza na wao tumezoea acha tuumie zaidi.
Mie hadi nawashangaa!! Hivi wanatumia akili kweli.? Yaani hadi aibu, wakae kimya tu waone Nchi inavyonyoshwa watashangilia baadae tutakapokuwa tunaimba TUMEFIKA SALAMA!!
Maiti kuukotwa baharini, changuzi za aina ya zile kata 43. Watu kupotea, MTU kupigwa risasi 30+ Uhuru kuminywa.nk bado unawataka wakae kimywa_?? Kaa ukijua MTU mwovu hana huruma!
 
Kila mfalme alijibiwa kwa namna yake ndani ya biblia...ninavyoelewa Mimi...Nabii Eliya alivyomfuata ahabu,alimpa makavu live wala hakutumia hadithi ni tofauti na Nabii Nathani kwa Mfalme Daudi.
 
Kama hakosolewei aende nchi ya kusadikika

Alale pema pepon marehem shaaban robert maandiko yake yanaishi.
Ila nadhani ni HAJARIBIWI sio HAKOSOLEWI. Mleta mada atakuwa amechanganya kidogo.
 
Kutumia kigezo kimoja tu cha mfalme daudi ni udhaifu wa hili andiko.

Pili wale walikuwa "rulers" na sio "leaders"

Tatu neno "mfalme" halina nafasi kwenye mchi ya kidemokrasia.

Nne angalau tumefika hapa kwa sababu kuna watu walipambana kukosoa "watawala".

Tano kiongozi yoyote aliyepata nafasi hiyo ya uongozi kwa kubahatisha lazima aogope kukosolewa kwa sababu hakujipa nafasi ya kujiamini kabla hata ya kuwa kiongozi. Ana-develop psychological disorder inayoitwa self consciousness.
 
Naam, mtakatifu wa watakatifu, Yesu Kristo, wala hakupepesa maneno; alimwita Herodi MBWEHA kutokana na aina ya utawala wake.

Luka 13:31-32:

31 Saa ile ile Mafarisayo kadha wa kadha walimwendea, wakamwambia, Toka hapa, uende mahali pengine, kwa sababu Herode anataka kukuua.

32 Akawaambia, Nendeni, mkamwambie yule mbweha, Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika.
 
Wafalme Hawakosolewi!!!!

Hakuna mfalme anayeweza kufanikiwa kutawala watu wa Mungu ikiwa yeye hana Mungu. Nikitumia Biblia kama kitabu cha rejea, watawala wengi sana wametajwa kushindwa au kuangamia kwa sababu hawakudumu katika maagizo ya Mungu.

Sauli alikuwa ni mfalme wa kwanza katika taifa la Uyahudi. Halikuwa kusudi la Mungu kuruhusu Wayahudi wawe na mfalme. Lakini Wayahudi walitaka kuwa na mfalme wafanane na mataifa mengine yenye wafalme wao.

Kabla ya wafalme, Mungu alikuwa ni mwamuzi wao. Lakini Wayahudi walitaka na wao wawe na wafalme ili wawaamulie. Mungu aliwaonya Wayahudi kwa kuwafunulia madhara ya wafalme. Haya ni baadhi ya madhara ambayo Mungu aliwaonya Wayahudi (1 Samweli 8:10-22):

 Mfalme atawatwaa watoto wenu ili wamtumikie
 Mfalme atawafanya watoto wenu wawe askari wa jeshi lake
 Mfalme atawatwaa mabinti zenu wamtumikie.
 Mfalme atatwaa mashamba yenu mazuri na mazao yake awape maakida wake
 Mfalme atawatoza ushuru ili awalishe watumishi na maakida wake
 Mfalme atawatoza fungu la kumi katika mapato yenu
 Nanyi mtalia sana mkijuta kuwa na mfalme mliyejichagulia wenyewe.

Hata hivyo Wayahudi walimtaka mfalme licha ya madhara hayo ambayo Mungu aliwaonya hapo mwanzo. Mungu akawapa Sauli kuwa mfalme wa kwanza wa Uyahudi.

Sauli alikuwa na shida yake kubwa iliyosababisha miisho yake mibaya. Cheo kile alipewa na Mungu lakini hakuhitaji busara ya Mungu akajiinua kwa hekima yake. Uovu ukamwingia akamkosea Mungu.

Sio kusudi langu kumzungumzia mfalme Sauli. Nia yangu ni mfalme Daudi, mrithi wake. Mfalme aliyepata kumpendeza Mungu kwa kiasi kikubwa sana.

Siku moja mfalme Daudi akiwa katika kasri yake, alimwona mwanamke mzuri sana kupitia dirishani. Mwanamke yule alikuwa ni mke wa Uria, mmoja wa askari wake waliokuwa vitani. Mfalme Daudi akamtamani mke wa Uria na akagizwa alatwe kwake.

Mfalme Daudi alifanya ngono na mke wa askari wake aliyekuwa vitani akimpigania! Kitendo kile kilipelekea mke wa Uria kupata ujauzito. Mfalme akaagiza Uria arudishwe nyumbani akiamini akija atalala na mkewe hivyo ataangushiwa jumba bovu juu ya ujauzito ule.

Hata hivyo Uria aliporudi alikataa kulala na mkewe akihoji kuwa ana furaha gani ya kulala na mkewe wakati askari wenzake wako vitani! Mpango huo wa mfalme Daudi ukafeli. Uovu ukazidi kumtafuna mfalme Daudi naye akaona ni heri kumwua Uria. Basi aliamuru askari yule arudi vitani huku akimtaka jemedari wa jeshi kumweka Uria kwenye mstari wa mbele wa mapambano. Mfalme Daudi alikusudia kusikia Uria akifia vitani.

Baada ya mapambano kuendelea, kweli Uria akafia vitani. Mfalme Daudi akapumua maana alijua sasa siri yake iko salama. Lakini kwa bahati mbaya mfalme Daudi alisahau kuwa Mungu alikuwa anaona uovu wake. Machoni pa watu mfalme Daudi alikuwa ni mtu mwema sana lakini alikuwa amemkosea Mungu na mwanadamu pia.

Dhambi yake ilikuwa ni kubwa sana na alistahili kufa. Ndipo Mungu alipomtuma Nathani kupeleka ujumbe kwa mfalme Daudi. Nathani alijua nguvu za wafalme. Nathani alijua wafalme hawapendi kukosolewa. Nathani alijua siku zote wafalme huamini kuwa wana uwezo mkubwa wa kutoa haki. Hivyo lilikuwa ni jambo la hatari sana kwa Nathani kumkosoa au kumwonya mfalme Daudi juu ya dhambi yake.

Nathani akaamua kumtupia mfalme Daudi kitanzi ili ajinyonge mwenyewe. Ndipo alipomsimulia kisa kilichopo katika kitabu cha Samweli wa Pili Sura ya kumi na mbili (2 Samweli 12:1ff). Nakusihi kabla ya kuendelea kusoma makala hii naomba usome sura niliyoitaja hapo juu ili ujue kile ambacho mfalme Daudi aliambiwa na Nathani mjumbe wa Mungu.

Jambo alilolifanya Nathani ndilo ambalo watumishi wa Mungu nchini wanapaswa kufanya. Wafalme wengi wanapenda sana kubarikiwa ila hawapendi kuoneshwa kuwa ni wakosaji mbele za watu wao maana watapoteza sifa ya kutawala. Ndio maana hata wakifanya makosa huwa hawataki yajulikane kwa watu wao maana kuishi kwao kunategemea watu! Mamlaka zao hazitakuwa na nguvu iwapo watapoteza imani kwa watu wao wanaowatawala.

Hivyo usitarajie kuwa unaweza kumkosoa mfalme hadharani na ukabakia salama. Huu ni utaratibu ambao uko tangu siku nyingi. Maana siku zote mfalme yuko sahihi! Kama si kwa kauli ya mfalme mwenyewe, basi maakida au watumishi wake watakushughulikia mara moja itakapobainika umejaribu kumkosoa mfalme maana kuishi kwao hutegemea hisani ya mfalme. Haya ndio Mungu aliyowaonya Wayahudi maana alijua desturi za wafalme.

Haki wanayosema wanaitoa si haki ya kweli bali ni haki yenye kuwatukuza wao zaidi. Si kweli watawaliwa wanaweza wasione uovu wa mfalme wao, lahasha! Wengi wanajua hatima yao iwapo watamkosoa mfalme hadharani.

Kwa jinsi hiyo, Mungu pekee ndiye hushughulika moja kwa moja na wafalme. Hata hivyo Mungu hawezi kuruhusu watu wake waumie kwa sababu ya uovu wa mfalme. Ipo njia itakayojitokeza katika kuwanusuru watu wake maana kilio cha wanyonge ni kelele kubwa sana mbele za Mungu.
Askofu Kakobe ulitakiwa utumie hekima ya Nathani katika kufikisha ujumbe wako kwa mfalme. Kile kinachoweza kukutokea kingeweza kumtokea pia Nathani kama angekifanya kama ulivyokifanya.

Uria yawezekana mpaka kufa kwake hakujua kwamba mfalme Daudi alizini na mke wake na kumpa ujauzito. Yawezekana Uria atastaajabu sana siku ya hukumu pale atakapo baini kuwa kufa kwake vitani haikuwa ushujaa wa kumpigania mfalme wake bali ilikuwa ni hukumu yake ili kuficha uovu wa mfalme anayemtumikia. Ni kweli wafalme hawakosolewi maana ni jambo wasilolipenda!
Jana niliandika humu, kukosoa kuko kwa aina nyingi na si lazima kukosoa kufanane. Kwa kisa hiki cha mfalme Daudi naomba tujiulize kidogo, huko nyuma Mungu hakumruhusu mtawala wa eneo fulani amguse mke wa Ibrahim japo tayari alikuwa ameshaingizwa ndani kwake, na akamuonya kuwa sikuruhusu umguse maana ni mke wa mtu, lakini kwa Daud aliruhusu na hadi mimba, kisha baaaye akamtumia mujumbe?
 
Hadithi yako anaweza kuisoma mtoto wa chekechea tu na akaikubali si kwa namna unavyojaribu ikusaidie kutetea usichokielewa, bali kwa jinsi inavyofurahisha kama zile hadithi za paka na panya. HUWEZI KUJADILI JAMBO LOLOTE KATIKA BIBLIA KWA KUCHOMOKA NA MSTARI MMOJA WEWE! Biblia iko very ballanced but for you, YOU ARE VERY UNBALLANCED ! Umejitahidi kujipendekeza hata hivyo.
 
Wafalme Hawakosolewi!!!!

Hakuna mfalme anayeweza kufanikiwa kutawala watu wa Mungu ikiwa yeye hana Mungu. Nikitumia Biblia kama kitabu cha rejea, watawala wengi sana wametajwa kushindwa au kuangamia kwa sababu hawakudumu katika maagizo ya Mungu.

Sauli alikuwa ni mfalme wa kwanza katika taifa la Uyahudi. Halikuwa kusudi la Mungu kuruhusu Wayahudi wawe na mfalme. Lakini Wayahudi walitaka kuwa na mfalme wafanane na mataifa mengine yenye wafalme wao.

Kabla ya wafalme, Mungu alikuwa ni mwamuzi wao. Lakini Wayahudi walitaka na wao wawe na wafalme ili wawaamulie. Mungu aliwaonya Wayahudi kwa kuwafunulia madhara ya wafalme. Haya ni baadhi ya madhara ambayo Mungu aliwaonya Wayahudi (1 Samweli 8:10-22):

 Mfalme atawatwaa watoto wenu ili wamtumikie
 Mfalme atawafanya watoto wenu wawe askari wa jeshi lake
 Mfalme atawatwaa mabinti zenu wamtumikie.
 Mfalme atatwaa mashamba yenu mazuri na mazao yake awape maakida wake
 Mfalme atawatoza ushuru ili awalishe watumishi na maakida wake
 Mfalme atawatoza fungu la kumi katika mapato yenu
 Nanyi mtalia sana mkijuta kuwa na mfalme mliyejichagulia wenyewe.

Hata hivyo Wayahudi walimtaka mfalme licha ya madhara hayo ambayo Mungu aliwaonya hapo mwanzo. Mungu akawapa Sauli kuwa mfalme wa kwanza wa Uyahudi.

Sauli alikuwa na shida yake kubwa iliyosababisha miisho yake mibaya. Cheo kile alipewa na Mungu lakini hakuhitaji busara ya Mungu akajiinua kwa hekima yake. Uovu ukamwingia akamkosea Mungu.

Sio kusudi langu kumzungumzia mfalme Sauli. Nia yangu ni mfalme Daudi, mrithi wake. Mfalme aliyepata kumpendeza Mungu kwa kiasi kikubwa sana.

Siku moja mfalme Daudi akiwa katika kasri yake, alimwona mwanamke mzuri sana kupitia dirishani. Mwanamke yule alikuwa ni mke wa Uria, mmoja wa askari wake waliokuwa vitani. Mfalme Daudi akamtamani mke wa Uria na akagizwa alatwe kwake.

Mfalme Daudi alifanya ngono na mke wa askari wake aliyekuwa vitani akimpigania! Kitendo kile kilipelekea mke wa Uria kupata ujauzito. Mfalme akaagiza Uria arudishwe nyumbani akiamini akija atalala na mkewe hivyo ataangushiwa jumba bovu juu ya ujauzito ule.

Hata hivyo Uria aliporudi alikataa kulala na mkewe akihoji kuwa ana furaha gani ya kulala na mkewe wakati askari wenzake wako vitani! Mpango huo wa mfalme Daudi ukafeli. Uovu ukazidi kumtafuna mfalme Daudi naye akaona ni heri kumwua Uria. Basi aliamuru askari yule arudi vitani huku akimtaka jemedari wa jeshi kumweka Uria kwenye mstari wa mbele wa mapambano. Mfalme Daudi alikusudia kusikia Uria akifia vitani.

Baada ya mapambano kuendelea, kweli Uria akafia vitani. Mfalme Daudi akapumua maana alijua sasa siri yake iko salama. Lakini kwa bahati mbaya mfalme Daudi alisahau kuwa Mungu alikuwa anaona uovu wake. Machoni pa watu mfalme Daudi alikuwa ni mtu mwema sana lakini alikuwa amemkosea Mungu na mwanadamu pia.

Dhambi yake ilikuwa ni kubwa sana na alistahili kufa. Ndipo Mungu alipomtuma Nathani kupeleka ujumbe kwa mfalme Daudi. Nathani alijua nguvu za wafalme. Nathani alijua wafalme hawapendi kukosolewa. Nathani alijua siku zote wafalme huamini kuwa wana uwezo mkubwa wa kutoa haki. Hivyo lilikuwa ni jambo la hatari sana kwa Nathani kumkosoa au kumwonya mfalme Daudi juu ya dhambi yake.

Nathani akaamua kumtupia mfalme Daudi kitanzi ili ajinyonge mwenyewe. Ndipo alipomsimulia kisa kilichopo katika kitabu cha Samweli wa Pili Sura ya kumi na mbili (2 Samweli 12:1ff). Nakusihi kabla ya kuendelea kusoma makala hii naomba usome sura niliyoitaja hapo juu ili ujue kile ambacho mfalme Daudi aliambiwa na Nathani mjumbe wa Mungu.

Jambo alilolifanya Nathani ndilo ambalo watumishi wa Mungu nchini wanapaswa kufanya. Wafalme wengi wanapenda sana kubarikiwa ila hawapendi kuoneshwa kuwa ni wakosaji mbele za watu wao maana watapoteza sifa ya kutawala. Ndio maana hata wakifanya makosa huwa hawataki yajulikane kwa watu wao maana kuishi kwao kunategemea watu! Mamlaka zao hazitakuwa na nguvu iwapo watapoteza imani kwa watu wao wanaowatawala.

Hivyo usitarajie kuwa unaweza kumkosoa mfalme hadharani na ukabakia salama. Huu ni utaratibu ambao uko tangu siku nyingi. Maana siku zote mfalme yuko sahihi! Kama si kwa kauli ya mfalme mwenyewe, basi maakida au watumishi wake watakushughulikia mara moja itakapobainika umejaribu kumkosoa mfalme maana kuishi kwao hutegemea hisani ya mfalme. Haya ndio Mungu aliyowaonya Wayahudi maana alijua desturi za wafalme.

Haki wanayosema wanaitoa si haki ya kweli bali ni haki yenye kuwatukuza wao zaidi. Si kweli watawaliwa wanaweza wasione uovu wa mfalme wao, lahasha! Wengi wanajua hatima yao iwapo watamkosoa mfalme hadharani.

Kwa jinsi hiyo, Mungu pekee ndiye hushughulika moja kwa moja na wafalme. Hata hivyo Mungu hawezi kuruhusu watu wake waumie kwa sababu ya uovu wa mfalme. Ipo njia itakayojitokeza katika kuwanusuru watu wake maana kilio cha wanyonge ni kelele kubwa sana mbele za Mungu.
Askofu Kakobe ulitakiwa utumie hekima ya Nathani katika kufikisha ujumbe wako kwa mfalme. Kile kinachoweza kukutokea kingeweza kumtokea pia Nathani kama angekifanya kama ulivyokifanya.

Uria yawezekana mpaka kufa kwake hakujua kwamba mfalme Daudi alizini na mke wake na kumpa ujauzito. Yawezekana Uria atastaajabu sana siku ya hukumu pale atakapo baini kuwa kufa kwake vitani haikuwa ushujaa wa kumpigania mfalme wake bali ilikuwa ni hukumu yake ili kuficha uovu wa mfalme anayemtumikia. Ni kweli wafalme hawakosolewi maana ni jambo wasilolipenda!
Tz kuna utawala wakifalme au ndio unatujulisha leo !!?? Hi tafsiri yako inakufaa wewe na mkeo na watoto wako ndani ya nyumba yako tena usikute umepanga
 
Back
Top Bottom