God knows
JF-Expert Member
- Sep 6, 2011
- 276
- 173
Nimeamua kufukua makaburi.
Ilikuwa mwaka 2013. Niliajiriwa kwenye kampuni X kama IT Technician. Walinitaka nifanye probation kwa muda wa mwezi mmoja ndipo wanipe mkataba na waniconfirm kazini.
Nilifanya kazi ule mwezi wa probation ukapita. Hawakusema chochote so my assumption ni kwamba nilipita ile probation yao. Baada ya mwezi wa kwanza kupita, nikaanza kufuatilia mkataba wa kazi. HR akawa anizungusha kila siku kwamba mara sijui nauandaa, mara sijui mkurugenzi hajasaini, n.k. Nikawa mvumilivu.
Mshahara ulitakiwa kutoka tarehe 24 September, wakanipa mkataba tarehe 19 September huku wakiniambia saini mkataba ili tuweze kuendelea kuprocess mishahara ya wafanyakazi wote. As if mimi ndio kikwazo.
Kilichonifanya nikatae ile kazi ni kufuatia kushushwa mshahara kwenye mkataba tofuati na ule tuliokubaliana wakati wa interview. Na walishaniwekea mtego kwa sababu wanajua hela zinatoka, so ningeshawishika tu kusaini ule mkataba. Nikaamua kuandika barua hii ya kukataa kazi.
Niliondoka siku hiyo hiyo ya tarehe 20 September, saa 6 mchana. Hata huo mshahara wao nilikuwa siutaki tena.
Kuna watu wana courage ya kufanya hivi leo?
It was only possible during those years when men were men. Nawasilisha.
Ilikuwa mwaka 2013. Niliajiriwa kwenye kampuni X kama IT Technician. Walinitaka nifanye probation kwa muda wa mwezi mmoja ndipo wanipe mkataba na waniconfirm kazini.
Nilifanya kazi ule mwezi wa probation ukapita. Hawakusema chochote so my assumption ni kwamba nilipita ile probation yao. Baada ya mwezi wa kwanza kupita, nikaanza kufuatilia mkataba wa kazi. HR akawa anizungusha kila siku kwamba mara sijui nauandaa, mara sijui mkurugenzi hajasaini, n.k. Nikawa mvumilivu.
Mshahara ulitakiwa kutoka tarehe 24 September, wakanipa mkataba tarehe 19 September huku wakiniambia saini mkataba ili tuweze kuendelea kuprocess mishahara ya wafanyakazi wote. As if mimi ndio kikwazo.
Kilichonifanya nikatae ile kazi ni kufuatia kushushwa mshahara kwenye mkataba tofuati na ule tuliokubaliana wakati wa interview. Na walishaniwekea mtego kwa sababu wanajua hela zinatoka, so ningeshawishika tu kusaini ule mkataba. Nikaamua kuandika barua hii ya kukataa kazi.
Niliondoka siku hiyo hiyo ya tarehe 20 September, saa 6 mchana. Hata huo mshahara wao nilikuwa siutaki tena.
Kuna watu wana courage ya kufanya hivi leo?
It was only possible during those years when men were men. Nawasilisha.