Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,190
- 34,526
MTUNZI: NYEMO CHILONGANI
mwanadishi kutoka nchini Tanzania, Erick Justo akiwa amechaguliwa kuwa mwandishi bora wa habari kwa Bara la Afrika mwaka huo. Ukiachana na furaha za Watanzania hao, hata yeye mwenyewe alifurahia kwa kuona kwamba ndoto ambayo alijiwekea toka kipindi cha nyuma, kwa wakati huo ilikuwa imetimia.
Uso wake ulikuwa na furaha, moyo wake ulikuwa umefanana na furaha ambayo alikuwa nayo wakati huo. Kila alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari, Erick hakuificha furaha yake.
Watu ambao walikuwa wamekusanyika katika Ukumbi wa Blue Pearl uliokuwepo Ubungo Jijini Dar es Salaam ndani ya Jengo la Ubungo Plaza bado walikuwa wakimpongeza mwandishi Erick ambaye alichukua tuzo hiyo iliyokuwa ikitetewa na Boniface Youssour, mwandishi wa habari kutoka nchini Ivory Coast.
Kila alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari, ni watu watatu tu ndio ambao walikuwa wakisikika akiwazungumzia, wa kwanza alikuwa mama yake, Bi Magreth ambaye alifariki kwa ajali ya gari miama minne iliyopita, baba yake, mzee Justo ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi kwa bahati mbaya na wa tatu alikuwa mkewe mpendwa, Christina ambaye alikuwa mjauzito.
Machozi ya furaha yalikuwa yakimtoka, ushindi ambao alikuwa ameupata ulionekana kuwa mkubwa katika maisha yake. Waandishi wa habari wa Shirika la Habari la CNN ambao ndiyo walikuwa wameitoa zawadi hiyo wakaamua kuandaa kipindi maalumu cha kufanya na Erick, kipindi ambacho waliamini kingemfanya kuonekana duniani kote.
“Siamini mke wangu... siamini mpenzi...” Erick alimwambia mkewe mara baada ya kufika nyumbani.
“Amini mume wangu. Wewe ndiye mwandishi bora katika mwaka huu” Christina alimwambia mumewe kipenzi, Erick.
Siku ziliendelea kukatika, Watanzania waliendelea kujivunia kwa kumpata mwandishi aliyeonekana kuwa bora katika kipindi hicho. Watu wengine wakaanza kufuatilia makala mbalimbali ambazo alikuwa akiziandika Erick katika magazeti ya sehemu alipokuwa akifanyia kazi.
Kila mtu aliyezisoma makala zake alipigwa na mshangao. Hawakuweza kuamini kama kulikuwa na mwandishi ambaye alikuwa akiandika mambo mengi mazuri na ya kuvutia kama ilivyokuwa kwa Erick.
Baada ya siku tatu kupita Erick akatumiwa tiketi na viza kwa ajili ya kusafiri kuelekea nchini Marekani. Huko alihitajika kwa ajili ya kufanya mahojiano na mtangazaji maarufu duniani, Larry King wa Kituo cha CNN. Erick hakukuamini kama alitarajiwa kusafiri kuelekea nchini Marekani ndani ya siku chache zijazo.
Kila kitu kilichokuwa kikitokea katika maisha yake kwa wakati huo kilikonekana kuwa kama ndoto ambapo baada ya muda fulani angeshtuka kutoka usingizini na kujikuta kitandani akiwa na mkewe. Kila wakati macho yake yalikuwa yakiangalia saa yake, dakika zilionekana kwenda taratibu sana tofauti na siku nyingine.
Alitamani muda uende harakaharaka ili asafiri na kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano juu ya ushindi wake huo. Kila siku alikuwa akipokea pongezi mbalimbali kutoka kwa watu tofautitofauti huku wakiendelea kumtakia mafanikio katika maisha yake.
Baada ya siku tatu kumalizika Erick akaanza safari ya kuelekea nchini Marekani. Kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake bado kilionekana kuwa kama ndoto, hakuamini kama siku moja ingetokea kwake na kusafiri kuelekea nchini Marekani, nchi ambayo alikuwa akiisikia tu au kuiona katika televisheni.
Ndani ya ndege hakulala, kila wakati alionekana kuwa na mawazo tu. Aliifikiria sana nchi ya Marekani, kuanzia uzuri na hadi maendeleo yaliyokuwa yakipatikana nchini humo. Hakuamini kama katika kipindi hicho alikuwa akielekea katika jengo kubwa la habari la kimataifa la CNN lililokuwa katika jiji la Atalanta.
Kwake, ilionekana kama ndoto. Jina la Larry King mara kwa mara lilikuwa likisomeka kichwani mwake. Hakuamini kama alikuwa akielekea kuhojiwa na mwandishi huyo ambaye alikuwa akiwahoji masupastaa wengi duniani.
Ingawa mara kwa mara alikuwa macho lakini akajikuta akianza kulala mara baada ya ndege kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cairo nchini Misri. Ndege iliendelea na safari huku Erick akiwa amepitiwa na usingizi mzito.
Alikuja kuamka saa mbili asubuhi mara baada ya ndege kuingia katika Uwanja wa Amstadam nchini Uholanzi ambako walitakiwa kubadilisha ndege ili kuendelea na safari ya kuelekea nchini Marekani.
Erick akateremka kutoka katika ndege na kuanza kupiga hatua kuelekea katika vyumba vya kupumzikia. Baridi kali ambalo lilikuwa likipatikana katika nchi mbalimbali za Ulaya lilionekana kumpa tabu. Kila wakati alikuwa akitetemeka tu japokuwa alikuwa amevaa koti zito.
Aliyapitisha macho yake katika majengo mbalimbali marefu na yaliyokuwa yakivutia, hakuamini kama majengo yale yalikuwa yakipatikana katika dunia moja iliyokuwa ikipatikana nchi ya Tanzania.
Hali ya hewa ikaonekana kubadilika mara baada ya kuingia ndani ya jengo la uwanja wa ndege. Hali ya joto ikaanza kupatikana, hiyo ilitokana na viyoyozi ambavyo vilikuwa vinaendelea kutumika ndani ya jengo hilo.
“Do I know you? (Hivi nakufahamu?)” Erick alishtushwa na sauti ya mwanaume mmoja ambaye alikuwa amekaa katika kiti cha pembeni ndani ya jego lile.
Erick akageuza macho yake na kuanza kumwangalia mwanaume yule, alimwangalia kwa makini huku akijaribu kuvuta kumbukumbu kama alikuwa amekwishawahi kumuona sehemu fulani lakini jibu lilikuwa hapana.
“I don’t know. I mean, I don’t know you (Sifahamu. Namaanisha sikufahamu)” alijibu Erick.
“Are you a famous? Maybe a musician, footballer or someone else (Wewe ni maarufu? labda mwanamuziki, mchezaji mpira au mtu mwingine?)” Mwanaume yule aliendelea kumuuliza Erick.
“No. I’m just a journalist (Hapana. Mimi ni mwandishi wa habari)” alijibu Erick.
“Are you Erick Justo? The Best Journalist of Africa this year? ( Wewe ni Erick Justo? Mwandishi bora wa Afrika?)” Mwanaume yule aliendelea kuuliza.
“Yes,” alijibu Erick.
“I’m Brian Michael, a jouranalist from BBC (Mimi ni Brian Michael, mwandishi wa habari kutoka BBC)” Mwanaume yule alijitambulisha.
Huo ndio ukawa mwanzo wa mazoea baina ya Erick na Brian. Wakaanza kuongea pamoja mpaka kufikia kipindi kuonekana kama walikuwa wamekutana siku nyingi zilizopita.
Mara baada ya kupumzika kwa muda wa dakika thelathini, abiria wote wakatakiwa kuelekea katika ndege yao kwa ajili ya kuendelea na safari ya kuelekea nchini Marekani.
Brian na Erick wakakaa katika viti vya pamoja huku wakiongea mambo mengi kuhusiana na uandishi pamoja na maisha kwa ujumla. Mazoea yao yakaongezeka zaidi, mpaka inafikia muda wa kulala, walionekana kuwa kama watu waliofahamiana kwa miaka mingi iliyopit *****
Hakukuwa na mtu ambaye alijua kwamba walikuwa wamefika nchini Marekani mpaka pale sauti ya kike ilipoanza kusikika wakitakiwa kufunga mikanda yao. Ndege ikaanza kutua huku saa ya ukutani ndani ya ndege hiyo ikinyesha kuwa saa tisa usiku.
Mara baada ya ndege kusimama, abiria wote wakaanza kuteremka. Erick alibaki akiangalia majengo makubwa yaliyokuwa yakivutia ambayo yalikuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Atlanta. Baridi lilikuwa kali nchini Marekani tofauti na Uholanzi au Tanzania alipotoka.
Abiria wote wakaanza kutembea na kuelekea nje ya jengo la uwanja ule. Kila kitu kilichokuwa kikionekana mbele yake kilikuwa kigeni. Erick alijisikia kumuuliza Brian mambo mengi kuhusu nchi hiyo, alisita kufanya hivyo kwani alijua fika kwamba Brian hakuwa mwenyeji sana nchini Marekani.
‘ERICK JUSTO’ Bango moja lililoshikwa na kijana mmoja lilisomeka vizuri machoni mwake.
Erick akaanza kupiga hatua kumfuata kijana yule na mara baada ya salamu wote wawili wakaanza kuelekea nje ya jengo lile na kupanda ndani ya gari moja dogo na safari ya kuelekea hotelini kuanza.
Jiji lilionekana kupendeza mno, majengo mengi makubwa na marefu yalikuwa yakionekana machoni mwake. Kila alipokuwa akiangalia mandhari ya jiji lile na alipokuwa akifananisha na mandhari ya jiji la Dar es Salaam, aliona kulikuwa na sababu nyingi zilizowafanya vijana wengi kuzamia nchini humo.
Gari likasimama nje ya hoteli moja kubwa iliyoitwa Jupiter Hill. Mhudumu ambaye alikuwa akihusika katika hoteli ile, akalisogelea gari lile na kumfungulia Erick mlango. Akaanza kuelekea moja kwa moja mpaka mapokezi.
Kila kitu kilionekana kuwa tayari, akapelekwa katika chumba ambacho alitakiwa kukaa. Wala haukuchukua muda mrefu, chakula kikaletwa, alipokula akaelekea bafuni kuoga.
Huu ni mwanzo tu.
Je unajua nini kiliendelea?
mwanadishi kutoka nchini Tanzania, Erick Justo akiwa amechaguliwa kuwa mwandishi bora wa habari kwa Bara la Afrika mwaka huo. Ukiachana na furaha za Watanzania hao, hata yeye mwenyewe alifurahia kwa kuona kwamba ndoto ambayo alijiwekea toka kipindi cha nyuma, kwa wakati huo ilikuwa imetimia.
Uso wake ulikuwa na furaha, moyo wake ulikuwa umefanana na furaha ambayo alikuwa nayo wakati huo. Kila alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari, Erick hakuificha furaha yake.
Watu ambao walikuwa wamekusanyika katika Ukumbi wa Blue Pearl uliokuwepo Ubungo Jijini Dar es Salaam ndani ya Jengo la Ubungo Plaza bado walikuwa wakimpongeza mwandishi Erick ambaye alichukua tuzo hiyo iliyokuwa ikitetewa na Boniface Youssour, mwandishi wa habari kutoka nchini Ivory Coast.
Kila alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari, ni watu watatu tu ndio ambao walikuwa wakisikika akiwazungumzia, wa kwanza alikuwa mama yake, Bi Magreth ambaye alifariki kwa ajali ya gari miama minne iliyopita, baba yake, mzee Justo ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi kwa bahati mbaya na wa tatu alikuwa mkewe mpendwa, Christina ambaye alikuwa mjauzito.
Machozi ya furaha yalikuwa yakimtoka, ushindi ambao alikuwa ameupata ulionekana kuwa mkubwa katika maisha yake. Waandishi wa habari wa Shirika la Habari la CNN ambao ndiyo walikuwa wameitoa zawadi hiyo wakaamua kuandaa kipindi maalumu cha kufanya na Erick, kipindi ambacho waliamini kingemfanya kuonekana duniani kote.
“Siamini mke wangu... siamini mpenzi...” Erick alimwambia mkewe mara baada ya kufika nyumbani.
“Amini mume wangu. Wewe ndiye mwandishi bora katika mwaka huu” Christina alimwambia mumewe kipenzi, Erick.
Siku ziliendelea kukatika, Watanzania waliendelea kujivunia kwa kumpata mwandishi aliyeonekana kuwa bora katika kipindi hicho. Watu wengine wakaanza kufuatilia makala mbalimbali ambazo alikuwa akiziandika Erick katika magazeti ya sehemu alipokuwa akifanyia kazi.
Kila mtu aliyezisoma makala zake alipigwa na mshangao. Hawakuweza kuamini kama kulikuwa na mwandishi ambaye alikuwa akiandika mambo mengi mazuri na ya kuvutia kama ilivyokuwa kwa Erick.
Baada ya siku tatu kupita Erick akatumiwa tiketi na viza kwa ajili ya kusafiri kuelekea nchini Marekani. Huko alihitajika kwa ajili ya kufanya mahojiano na mtangazaji maarufu duniani, Larry King wa Kituo cha CNN. Erick hakukuamini kama alitarajiwa kusafiri kuelekea nchini Marekani ndani ya siku chache zijazo.
Kila kitu kilichokuwa kikitokea katika maisha yake kwa wakati huo kilikonekana kuwa kama ndoto ambapo baada ya muda fulani angeshtuka kutoka usingizini na kujikuta kitandani akiwa na mkewe. Kila wakati macho yake yalikuwa yakiangalia saa yake, dakika zilionekana kwenda taratibu sana tofauti na siku nyingine.
Alitamani muda uende harakaharaka ili asafiri na kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano juu ya ushindi wake huo. Kila siku alikuwa akipokea pongezi mbalimbali kutoka kwa watu tofautitofauti huku wakiendelea kumtakia mafanikio katika maisha yake.
Baada ya siku tatu kumalizika Erick akaanza safari ya kuelekea nchini Marekani. Kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake bado kilionekana kuwa kama ndoto, hakuamini kama siku moja ingetokea kwake na kusafiri kuelekea nchini Marekani, nchi ambayo alikuwa akiisikia tu au kuiona katika televisheni.
Ndani ya ndege hakulala, kila wakati alionekana kuwa na mawazo tu. Aliifikiria sana nchi ya Marekani, kuanzia uzuri na hadi maendeleo yaliyokuwa yakipatikana nchini humo. Hakuamini kama katika kipindi hicho alikuwa akielekea katika jengo kubwa la habari la kimataifa la CNN lililokuwa katika jiji la Atalanta.
Kwake, ilionekana kama ndoto. Jina la Larry King mara kwa mara lilikuwa likisomeka kichwani mwake. Hakuamini kama alikuwa akielekea kuhojiwa na mwandishi huyo ambaye alikuwa akiwahoji masupastaa wengi duniani.
Ingawa mara kwa mara alikuwa macho lakini akajikuta akianza kulala mara baada ya ndege kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cairo nchini Misri. Ndege iliendelea na safari huku Erick akiwa amepitiwa na usingizi mzito.
Alikuja kuamka saa mbili asubuhi mara baada ya ndege kuingia katika Uwanja wa Amstadam nchini Uholanzi ambako walitakiwa kubadilisha ndege ili kuendelea na safari ya kuelekea nchini Marekani.
Erick akateremka kutoka katika ndege na kuanza kupiga hatua kuelekea katika vyumba vya kupumzikia. Baridi kali ambalo lilikuwa likipatikana katika nchi mbalimbali za Ulaya lilionekana kumpa tabu. Kila wakati alikuwa akitetemeka tu japokuwa alikuwa amevaa koti zito.
Aliyapitisha macho yake katika majengo mbalimbali marefu na yaliyokuwa yakivutia, hakuamini kama majengo yale yalikuwa yakipatikana katika dunia moja iliyokuwa ikipatikana nchi ya Tanzania.
Hali ya hewa ikaonekana kubadilika mara baada ya kuingia ndani ya jengo la uwanja wa ndege. Hali ya joto ikaanza kupatikana, hiyo ilitokana na viyoyozi ambavyo vilikuwa vinaendelea kutumika ndani ya jengo hilo.
“Do I know you? (Hivi nakufahamu?)” Erick alishtushwa na sauti ya mwanaume mmoja ambaye alikuwa amekaa katika kiti cha pembeni ndani ya jego lile.
Erick akageuza macho yake na kuanza kumwangalia mwanaume yule, alimwangalia kwa makini huku akijaribu kuvuta kumbukumbu kama alikuwa amekwishawahi kumuona sehemu fulani lakini jibu lilikuwa hapana.
“I don’t know. I mean, I don’t know you (Sifahamu. Namaanisha sikufahamu)” alijibu Erick.
“Are you a famous? Maybe a musician, footballer or someone else (Wewe ni maarufu? labda mwanamuziki, mchezaji mpira au mtu mwingine?)” Mwanaume yule aliendelea kumuuliza Erick.
“No. I’m just a journalist (Hapana. Mimi ni mwandishi wa habari)” alijibu Erick.
“Are you Erick Justo? The Best Journalist of Africa this year? ( Wewe ni Erick Justo? Mwandishi bora wa Afrika?)” Mwanaume yule aliendelea kuuliza.
“Yes,” alijibu Erick.
“I’m Brian Michael, a jouranalist from BBC (Mimi ni Brian Michael, mwandishi wa habari kutoka BBC)” Mwanaume yule alijitambulisha.
Huo ndio ukawa mwanzo wa mazoea baina ya Erick na Brian. Wakaanza kuongea pamoja mpaka kufikia kipindi kuonekana kama walikuwa wamekutana siku nyingi zilizopita.
Mara baada ya kupumzika kwa muda wa dakika thelathini, abiria wote wakatakiwa kuelekea katika ndege yao kwa ajili ya kuendelea na safari ya kuelekea nchini Marekani.
Brian na Erick wakakaa katika viti vya pamoja huku wakiongea mambo mengi kuhusiana na uandishi pamoja na maisha kwa ujumla. Mazoea yao yakaongezeka zaidi, mpaka inafikia muda wa kulala, walionekana kuwa kama watu waliofahamiana kwa miaka mingi iliyopit *****
Hakukuwa na mtu ambaye alijua kwamba walikuwa wamefika nchini Marekani mpaka pale sauti ya kike ilipoanza kusikika wakitakiwa kufunga mikanda yao. Ndege ikaanza kutua huku saa ya ukutani ndani ya ndege hiyo ikinyesha kuwa saa tisa usiku.
Mara baada ya ndege kusimama, abiria wote wakaanza kuteremka. Erick alibaki akiangalia majengo makubwa yaliyokuwa yakivutia ambayo yalikuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Atlanta. Baridi lilikuwa kali nchini Marekani tofauti na Uholanzi au Tanzania alipotoka.
Abiria wote wakaanza kutembea na kuelekea nje ya jengo la uwanja ule. Kila kitu kilichokuwa kikionekana mbele yake kilikuwa kigeni. Erick alijisikia kumuuliza Brian mambo mengi kuhusu nchi hiyo, alisita kufanya hivyo kwani alijua fika kwamba Brian hakuwa mwenyeji sana nchini Marekani.
‘ERICK JUSTO’ Bango moja lililoshikwa na kijana mmoja lilisomeka vizuri machoni mwake.
Erick akaanza kupiga hatua kumfuata kijana yule na mara baada ya salamu wote wawili wakaanza kuelekea nje ya jengo lile na kupanda ndani ya gari moja dogo na safari ya kuelekea hotelini kuanza.
Jiji lilionekana kupendeza mno, majengo mengi makubwa na marefu yalikuwa yakionekana machoni mwake. Kila alipokuwa akiangalia mandhari ya jiji lile na alipokuwa akifananisha na mandhari ya jiji la Dar es Salaam, aliona kulikuwa na sababu nyingi zilizowafanya vijana wengi kuzamia nchini humo.
Gari likasimama nje ya hoteli moja kubwa iliyoitwa Jupiter Hill. Mhudumu ambaye alikuwa akihusika katika hoteli ile, akalisogelea gari lile na kumfungulia Erick mlango. Akaanza kuelekea moja kwa moja mpaka mapokezi.
Kila kitu kilionekana kuwa tayari, akapelekwa katika chumba ambacho alitakiwa kukaa. Wala haukuchukua muda mrefu, chakula kikaletwa, alipokula akaelekea bafuni kuoga.
Huu ni mwanzo tu.
Je unajua nini kiliendelea?