Barua Iliyotumwa kwa Waziri Mkuu kuhusu Makato ya Bodi ya Mikopo na Tozo ya Asilimia 6 kila Mwaka

Mk54

JF-Expert Member
Dec 29, 2016
1,997
3,933
Kasim Majaliwa,
Waziri Mkuu, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
S.L.P 980, Ofisi ya Waziri Mkuu,
DODOMA, TANZANIA


YAH; BODI YA MIKOPO NA MAKATO YA ASILIMIA 15 KUFUATIA SHERIA YA MWAKA 2016 PAMOJA NA TOZO YA ASILIMIA 6 AMBAYO BODI IMESHINDWA KUITOLEA UFAFANUZI SAHIHI JUU YA UTEKELEZAJI WAKE

Tafadhali rejea kichwa cha habari.

Malalamiko ya wanufaika juu ya makato ya asilimia 15 na ongezeko la thamani ya asilimia 6 iliyoanzishwa kwa mujibu wa Bodi ya Mikopo na kwamba kila mwaka kutakuwa na ongezeko la asilimia 6.

Aidha, baada ya Bodi ya Mikopo kuombwa kutoa ufafanuzi wa makato pamoja na ongezeko la asilimia 6 kila mwaka, Bodi ilijibu kupitia tamko lake kwa umma tarehe 6, Juni 2019 kama ifuatavyo;

(b)-ii; Kutamka kuwa Mnufaika aliyeajiriwa atakatwa asilimia 15 ya mshahara ghafi kwa ajili ya marejesho kwa HESLB. Awali, Sheria iliipa Serikali(Bodi) mamlaka ya kupanga kiwango cha makato. Tozo ya asilimia VRF (6%) ipo ndani ya makato ya asilimia 15. Rejea tamko hilo sambamba na barua hii.

Inashangaza kuona kwamba ongezo la asilimia 6 lipo ndani ya makato ya asilimia 15 ya kila mwezi lakini bado kila mwaka deni linaendelea kuongezeka kwa asilimia 6 kwenye salio lililobaki yaani outstanding loan Balance. Kwa maana nyingine, Bodi inakata tozo la asilimia sita mara mbili kinyume na sheria.

Kwa mfano daktari aliyesoma Tanzania katika chuo cha Bugando mwenye deni la shilingi milioni 30;

Kwa mshahara ghafi wa shilingi 1,500,000, makato ya Bodi yatakuwa 225,000/mwezi (Asilimia 15 ambayo ilielezwa kwamba ndani yake kuna tozo ya asilimia 6); Hivyo kwa muda wa miezi 12, mnufaika atalipa jumla ya shilingi 2,700,000. Deni linalotakiwa kubaki kwa mwaka unaopindukia ni shilingi 27,300,000, lakini kwa kuwa kuna tozo la asilimia 6, deni hilo litakuwa shilingi 28,938,000 ambalo ndio mnufaika ataendelea nalo.

Aidha mawasiliano yalifanyika na Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo yakimshauri kupitia upya kikokoto kinachotumika katika utekelezaji wa makato. Hakukuwa na mrejesho.

Kwa maelezo hapo juu, tunaomba na kushauri ofisi yako juu ya yafuatayo;

· Serikali ipitie upya sheria ya mwaka 2012/2013 yenye incremental ya asilimia 6

· Serikali iangalie namna ya kupunguza makato ya asilimia 15

· Uchunguzi ufanyike juu ya tozo ya asilimia 6 inayokatwa mara mbili

· Bodi ihakikishe kwamba wafanyakazi wote wa sekta binafsi wanafikiwa; na wale ambao hawakurudi Tanzania baada ya kumaliza masomo yao. Bodi iwasiliane na balozi za Tanzania kuwatambua na kuwatengenezea mfumo wa urejeshaji wakiwa huko nje. Kuna udhaifu katika utendaji wa Bodi ya Mikopo na makato yasiyokuwa na ufafanuzi sahihi, pia kuna kiasi kikubwa cha fedha wanashindwa kukusanya kutokana mapungufu ya mifumo yake. Matokeo ni nguvu nyingi hutumika kwa watumishi wa umma ili kufikia malengo ya makusanyo.

Asante.

Nakala; John Pombe Magufuli,
Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
S.L.P 1102, CHAMWINO
40400 DODOMA


View attachment 1406572View attachment 1406574View attachment 1406575
 
kuna mtu kwenye bahasha kaandika jina la rais utadhani anaandika jina la mjomba wake
 
Hii inakatisha tamaa sana..yaani kuajiriwa imekua adhabu..mshahara kiduchu,hakuna anayejali..tena hawa HESLB wadhulumati sana..hatukatai mmetukopesha na kulipa sio tatizo kwa wale walioajiriwa lakini wangewekautaratibu ambao utakua rafiki.
 
Nafuu tu nilinyimwa mkopo na hawa jamaa nikasoma kwa shida sana, sasahivi nakula mema ya Nchi ya maziwa na asali

Zala Na Nga

Kwanini unyimwe ?ni haki Yako ya msingi, ni kodi za wazazi wako na ndugu zako
 
Hii inakatisha tamaa sana..yaani kuajiriwa imekua adhabu..mshahara kiduchu,hakuna anayejali..tena hawa HESLB wadhulumati sana..hatukatai mmetukopesha na kulipa sio tatizo kwa wale walioajiriwa lakini wangewekautaratibu ambao utakua rafiki.

Ni wezi kwa maana isiyo rasmi. Na makato yao hayaeleweki hata ukifafanuliwa. Ukisoma hata tamko lao halieleweki pia.

Imefika wakati sasa hili suala liamuliwe high level.
 
Kasim Majaliwa,
Waziri Mkuu, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
S.L.P 980, Ofisi ya Waziri Mkuu,
DODOMA, TANZANIA


YAH; BODI YA MIKOPO NA MAKATO YA ASILIMIA 15 KUFUATIA SHERIA YA MWAKA 2016 PAMOJA NA TOZO YA ASILIMIA 6 AMBAYO BODI IMESHINDWA KUITOLEA UFAFANUZI SAHIHI JUU YA UTEKELEZAJI WAKE

Tafadhali rejea kichwa cha habari.

Malalamiko ya wanufaika juu ya makato ya asilimia 15 na ongezeko la thamani ya asilimia 6 iliyoanzishwa kwa mujibu wa Bodi ya Mikopo na kwamba kila mwaka kutakuwa na ongezeko la asilimia 6.

Aidha, baada ya Bodi ya Mikopo kuombwa kutoa ufafanuzi wa makato pamoja na ongezeko la asilimia 6 kila mwaka, Bodi ilijibu kupitia tamko lake kwa umma tarehe 6, Juni 2019 kama ifuatavyo;

(b)-ii; Kutamka kuwa Mnufaika aliyeajiriwa atakatwa asilimia 15 ya mshahara ghafi kwa ajili ya marejesho kwa HESLB. Awali, Sheria iliipa Serikali(Bodi) mamlaka ya kupanga kiwango cha makato. Tozo ya asilimia VRF (6%) ipo ndani ya makato ya asilimia 15. Rejea tamko hilo sambamba na barua hii.

Inashangaza kuona kwamba ongezo la asilimia 6 lipo ndani ya makato ya asilimia 15 ya kila mwezi lakini bado kila mwaka deni linaendelea kuongezeka kwa asilimia 6 kwenye salio lililobaki yaani outstanding loan Balance. Kwa maana nyingine, Bodi inakata tozo la asilimia sita mara mbili kinyume na sheria.

Kwa mfano daktari aliyesoma Tanzania katika chuo cha Bugando mwenye deni la shilingi milioni 32;

Kwa mshahara ghafi wa shilingi 1,500,000, makato ya Bodi yatakuwa 225,000/mwezi (Asilimia 15 ambayo ilielezwa kwamba ndani yake kuna tozo ya asilimia 6); Hivyo kwa muda wa miezi 12, mnufaika atalipa jumla ya shilingi 2,700,000. Deni linalotakiwa kubaki kwa mwaka unaopindukia ni shilingi 27,300,000, lakini kwa kuwa kuna tozo la asilimia 6, deni hilo litakuwa shilingi 28,938,000 ambalo ndio mnufaika ataendelea nalo.

Aidha mawasiliano yalifanyika na Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo yakimshauri kupitia upya kikokoto kinachotumika katika utekelezaji wa makato. Hakukuwa na mrejesho.

Kwa maelezo hapo juu, tunaomba na kushauri ofisi yako juu ya yafuatayo;

· Serikali ipitie upya sheria ya mwaka 2012/2013 yenye incremental ya asilimia 6

· Serikali iangalie namna ya kupunguza makato ya asilimia 15

· Uchunguzi ufanyike juu ya tozo ya asilimia 6 inayokatwa mara mbili

· Bodi ihakikishe kwamba wafanyakazi wote wa sekta binafsi wanafikiwa; na wale ambao hawakurudi Tanzania baada ya kumaliza masomo yao. Bodi iwasiliane na balozi za Tanzania kuwatambua na kuwatengenezea mfumo wa urejeshaji wakiwa huko nje. Kuna udhaifu katika utendaji wa Bodi ya Mikopo na makato yasiyokuwa na ufafanuzi sahihi, pia kuna kiasi kikubwa cha fedha wanashindwa kukusanya kutokana mapungufu ya mifumo yake. Matokeo ni nguvu nyingi hutumika kwa watumishi wa umma ili kufikia malengo ya makusanyo.

Asante.

Nakala; John Pombe Magufuli,
Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
S.L.P 1102, CHAMWINO
40400 DODOMA

View attachment 1406127View attachment 1406128View attachment 1406129
Na kwanini iwe 6% kila mwaka tena ya outstanding balance?. Kama ndivyo manaake mtumishi atakatwa maisha yake yote ya utumishi na hata maliza deni mwisho litahamishiwa kwenye fao lake la kustaafu.

Huu ni wizi na endapo lingekuwa ni shirika au mtu binafsi ndo anafanya hivyo, sasa hivi angekua jela.
 
Na kwanini iwe 6% kila mwaka tena ya outstanding balance?. Kama ndivyo manaake mtumishi atakatwa maisha yake yote ya utumishi na hata maliza deni mwisho litahamishiwa kwenye fao lake la kustaafu.

Huu ni wizi na endapo lingekuwa ni shirika au mtu binafsi ndo anafanya hivyo, sasa hivi angekua jela.

Yaani ukisoma maelezo ya tamko la Bodi, 6% ipo ndani ya 15% . Lakini ukiendelea kusoma inasema kwamba 6% ni Tozo la kwenye Outstanding balance kila mwaka.

Kifupi anayeweza kumaliza ni yule anayedaiwa chini ya 5 Mil na njia pekee ya kulimaliza ni kulipa kwa pamoja.

Sasa hawa kayumba waliosoma na kufika Mil 20 maana yake hawezi kulipa kwa pamoja, na hilo deni litaendelea kuongezeka kwa asilimia 6 kila mwaka huku kila mwezi anakatwa 15% ya basic salary yake.

Inakuwa ni hatari kwa waliosoma nje kama Urusi, India, China etc etc maana hao deni lao linakwenda hadi 60Mil .

Huyu mtu wa 60 Mil hawezi kulipa ni lazima astaafu akiwa na deni la bodi. Na kama
Wakishika mafao yake ndio imekula kwake.

Ni hatari sana na ndio maana tunaishauri serikali ipitie upya huu mfumo mzima wa makato ya bodi kwa maana 80% wanaonufaika na huu mkopo ni watu wa kipato cha chini.

Mzazi mwenye hela zake hamsumbui mtoto wake na mambo ya Bodi.

Asilimia 95 ya madakari na baadhi ya kada za Afya wamesomeshwa na Bodi.

Yes ni wakati wao Sasa kulipa, lakini wawekewe mfumo bora wa malipo ili isiwe mzigo kwao na wakashindwa kuendesha maisha yao.
 
Hiki chombo nichakuangalia sana! Nawapinzani hizi ndio zilikuwa hoja za kuzungumzia sasa badara yakukaa kutengeneza maandamano na vurugu!
Mfano.
1.loan board
2.Nyongeza ya mishahara
3.Bima ya afya
4.Bill za maji
5.Huduma za afya
6.Maripo ya wastaaf, uhamisho,posho za kujikim nk.

Mambo haya 6 pamoja na mengine bado serikari inaudhaifu mkubwa! Ukikaa ukachunguza vzr utaona kwa mapana yke jambo hili.
Hapo mnaweza kurudisha baadhi ya wabunge bungeni badara yakufanya siasa mlizo nazo ss.
 
PM anawaomba na kuwashauri .....?????
Nasubiri kiki masters kufanya yao pale 'mishe' itakapotiki.

HESLB wanafanya plundering!
"Aliyeshiba hamjui mwenye njaa'
 
Back
Top Bottom