Barua hizi zinaonyesha Wahusika wakuu wa wizi wa ESCROW funds,l tuzichambue kwa umakini

Wakuu nimejaribu kutafuta mwelekeo wa hili jambo inaonekana liko vibaya kiutendaji.
Wapo waliouliza maswali mazuri hapa kwenye jukwaa ambayo nami ningependa niongeze kidogo.

1. Hivi hatuna Kamati za kitaalamu kwenye hizi Wizara ambazo zinashughulikia mambo kama haya? Sidhani ni jambo zuri sana Singh kwenda kumwona Gavana na kukubaliana naye kuwa a-release fedha ya mgogoro kama hiyo.
2. Je AG anayo nguvu ya yeye mwenyewe ya kuelekeza malipo kama haya yafanyike bila hata kuonyesha dondoo za kikao kilichoamua jambo kama hilo. Ikiwa na majina ya waliokaa kikao? Je mtu mmoja si ataweza kuuza nchi kwa mapango kama huu?
3. Kwanini huu uamuzi ulipochukuliwa na hata barua zenyewe zinaonyehsa, wahusika wakuu TANESCO hawakuhusishwa hapo mwishoni? Kwanini sioni Meneja Mkuu wa TANESCO akipewa nakala? Au hata akitajwa kuwa alikuwepo kwenye kikao chochote kilichofikia maamuzi hayo? Huu si uongozi na utendaji wa kudharauliana?
4. Kwanini sioni mahali ambapo TRA imetajwa kwamba katika kuuzwa kwa hisa za Mechmar na VIP, na PAP kuwa mmiliki wa share nyingi kuwa TRA ilikusanya kodi stahili kutoka kwenye mkataba wa mauziano?
5. Kwanini sijaona mahali AG ameipa taarifa TRA kuhusu mauziano hayo na kwamba ni kiasi gani ili TRA waweze kuokokotoa kiwango cha kodi stahili?

Hayo tu ndiyo nataka majibu yake kwa sasa.

Asanteni kwa michango yenu inaelimisha sana.
 
Nimesoma attachment zako zote mbili, sijaona tatizo lako ni nini?

Ulitaka Maswi asielekeze kuwa kutokana na AG, mgogoro umekwisha na BOT wawachie fedha ziliwekwa escrow na wao waendelee kupata huduma au vipi?

Mkataba uliouweka "umagumashi" wake uko wapi?


Hata kama barua hazionyeshi tatizo walau imeweza kuleta tezi dume. Si mbaya. Nafikiri mwenye tezi dume anaujua ukweli sawa na barua hizi za siri na tezi dume sirini.
 
Hata kama barua hazionyeshi tatizo walau imeweza kuleta tezi dume. Si mbaya. Nafikiri mwenye tezi dume anaujua ukweli sawa na barua hizi za siri na tezi dume sirini.

Naona huna hoja na unahororoja na kubwabwaja bila mpango.
 
Kama kuna darasa la wanafunzi 45, wakielewa wanafunzi 44, wewe utakuwa bado hujaelewa. Kipimo cha mwalimu kujua kama wanafunzi wote wameelewa somo itakuwa kuelewa kwako aidha hakuna uwezekano kama unaweza kuelewa kabla ya wengine. Wala siyo kusema huelewi kwa makusudi, la hasha! Hivyo ndivyo uliivyo na wala hupaswi kulaumiwa na yeyote kwani aliyewapa wengine ndiye aliyekunyima wewe. Ungalikuwa huchangii sana tusingalijua ushungi wako unafunika nini, ila kwa sababu unajieleza mwenyewe unaudhihirishia umma kuwa ushungi wako unafunika ombwe (vacuum). Lakini kwa upande mwingine unaweza kuwa na uwezo maalum kwa mambo ambayo pengine wengine kwao yakawa magumu,kwako ni mepesi kama vile kutunza mume, kupika, kulea watoto, umbea saloon na mitaani, kuiba waume za watu. Mambo yapo mengi hapa duniani sio lazima kuyajua yote, yanatosha unayoyajua mengine waachie wenzio.
Nimesoma attachment zako zote mbili, sijaona tatizo lako ni nini?

Ulitaka Maswi asielekeze kuwa kutokana na AG, mgogoro umekwisha na BOT wawachie fedha ziliwekwa escrow na wao waendelee kupata huduma au vipi?

Mkataba uliouweka "umagumashi" wake uko wapi?
 
Kama kuna darasa la wanafunzi 45, wakielewa wanafunzi 44, wewe utakuwa bado hujaelewa. Kipimo cha mwalimu kujua kama wanafunzi wote wameelewa somo itakuwa kuelewa kwako aidha hakuna uwezekano kama unaweza kuelewa kabla ya wengine. Wala siyo kusema huelewi kwa makusudi, la hasha! Hivyo ndivyo uliivyo na wala hupaswi kulaumiwa na yeyote kwani aliyewapa wengine ndiye aliyekunyima wewe. Ungalikuwa huchangii sana tusingalijua ushungi wako unafunika nini, ila kwa sababu unajieleza mwenyewe unaudhihirishia umma kuwa ushungi wako unafunika ombwe (vacuum). Lakini kwa upande mwingine unaweza kuwa na uwezo maalum kwa mambo ambayo pengine wengine kwao yakawa magumu,kwako ni mepesi kama vile kutunza mume, kupika, kulea watoto, umbea saloon na mitaani, kuiba waume za watu. Mambo yapo mengi hapa duniani sio lazima kuyajua yote, yanatosha unayoyajua mengine waachie wenzio.

Mkuu unajuwa kufukuza shetani bila kumkemea kwa nguvu hongera sana
 
Mimi naona dhahiri hapa kuna tatizo, nashukuru kwa sababu nimeona mengi, sasa nangoja nione litakaloendelea baada ya ripoti kukabidhiwa kamati ya bunge. Niwashuri hao waliokabidhiwa hiyo ripoti pamoja na wale wenye tabia ya kutetea hata uovu kwamba hapa siyo mahali pake, na ole wao maana 2015 si mbali ni mwakani tu, tutafanya mageuzi hawajawahi kuyaona. Nchi hii ni yetu sote, ni fedheha kwa wajanja wachache kujifanya wao ndiyo Tanzania, hii haikubaliki.
 
Tuombe mungu mengi yajulikane ili kila mmoja tumjue maana Watanzania hatuwezi kukasirika na kuchukua hatua bali tutasahau tu muda mfupi ujao wakishajulikana!
 
Kwa huu upu^pu ulioandika sina shaka kabisa kuwa uelewa wako mdogo sana. Kwahiyo tukatane mapanga sababu ya kampuni binafsi kulipwa haki yake baada ya kutoa huduma ya umeme ambao tuliutumia? Kwahiyo IPTL wasilipwe?

Mkuu mleta mada tayari ana mawazo hasi na serikali hivyo anachowaza ni kuiponda tu serikali.

Mkuu you have not understood the letter kindly revisit the contents. There is nothing like PAP in the agreenent rather PPA. Hii issue huifahamu mzee kaa pembeni, pap ilinunua hisa za vip na mechmar ikijumuisha faida na madeni yake so ilikua na haki ya malipo ya escrow simple

Labda kwa kuangalia vigezo vingine lakini kwa kigezo cha barua, Maswi hana kosa hapo... yeye alikuwa anafuata maelekezo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali... sasa kazi kwake Werema kama alifanya hivyo kwa vile ndivyo ilivyotakiwa kufanyika au kama alifanya hivyo kutokana na maelekezo aliyopewa na wakubwa wake!

Nimesoma nimeelewa na sijakiona cha maana zaidi kuhororoja na kubwabwaja.

Mazuzu kazini!
 
Nimesoma attachment zako zote mbili, sijaona tatizo lako ni nini?

Ulitaka Maswi asielekeze kuwa kutokana na AG, mgogoro umekwisha na BOT wawachie fedha ziliwekwa escrow na wao waendelee kupata huduma au vipi?

Mkataba uliouweka "umagumashi" wake uko wapi?
Mimi nadhan kusoma sio shida hata mtoto Wa nursery anaweza kusoma.Issue ni kumake sense of what has been written in those attachments.
Sina shaka sasa kuwa tatizo lako kubwa sio kushindwa kusoma wewe una poor analytical thinking au una uelewa finyu. Wadau watu Wa hivi tusiwe tunawajibu mana wanatupa kazi isiyo yetu. Wanatakiwa warudi shule wakajifunze namna ya kupambanua mambo.
 
Hii hii issue imekuwa ya kisiasa zaidi kuliko inavyotakiwa kuwa. Kisheria. Baada ya kuibuka mgogoro wa tafsiri ya mkataba iliamuliwa fedha kwa ajili ya malipo ya iptl ziwekwe kwenye akaunti ya pamoja ili ufumbuzi unapopatikana malipo yafanyike kwa mhusika halali. Baada ya maamuzi ya mahakama. Pap ikanunua hisa za vip na mechmar hivyo kuwa major shareholder baada ya makubaliano ya pande zote katika mgogoro ikaonekana kuwa fedha zilizokuwa kwenye akaunti ya pamoja zilipwe kwa mmiliki mpya aliyekuwa na haki ya faida na madeni yote ya iptl
Hivi unafahami aliyeshinda katika hiyo kesi?? au aliyekuhadithia hajakueleza mahakama ya kimataifa ambayo ndiyo iliyotakiwa kusimamia shauri la iptl na tanesco kisheria imeamuaje? au pia hujajua mkanganyiko uliotokea mahakaman? je wewe mwenzetu unafaham kwann mahakama kuu ya tz imeamua kuamua kesi isiyo yao?ungefwatilia haya kwa umakin nadhan usingepotezea watu muda wao.
 
Mazuzu kazini!

Hata kichaa huwaona wale wasio vichaaa kama wana mapungufu. Suala linabaki pale pale kwamba kama kuna faulo ilichezwa basi wanaopaswa kulaumiwa ni mahakama na siyo Maswi na wenzake. Maswi alikuwa anatekeleza maamuzi ya mahakama full stop. Hata hivyo hiyo pesa hata ingekaa miaka mia moja bado ingelipwa kwa wahusika. Serikali haikuwa na haki ya kutumia pesa hiyo.
 
Sijaelewa wiz uko wap
Huwezi kuona neno Wizi limeandikwa kwenye hizi attachments Dada Yang. You have to analyze yaloandikwa ndo utaona hizo irregularities ambazo wenzio wanazitranslate km wizi!We mccm nn mbona km unakichwa kizito?
 
Back
Top Bottom