Baraza mseto la mawaziri

Baraza mseto la mawaziri

Chadema wanatakiwa kusubiri wakati wao 2015. Mseto ni UNAFIKI.
 
Wewe Malecela woga wako ni kuwa CDM ikikubali nafasi yeyote ya uwaziri chance ya mama yako kupata uwaziri itapungua kwa taarifa yako CDM hawataki nafasi kwenye hiyo serikali legelege
 
Kaka umerudi USA au ndo unakesha katika mkakati wa kumtoa kibajaj? Vipi siasa za bongo?sema na Mzee wako amuombe JK akuteue kamanda maana duh naskia EALA hukuwa hata na mia ya Kuhonga ukaambulia Kura za CHADEMA lini unarudi huku?


Come on man, give William a breakl! At least he is trying to do something for his country. He did not do well at EALA but must you insult him like that? I may not agree with William's views all the time, but I give him respect for expressing them and standing up to be counted. If you are so passionate about our country, you should try to take part in its development!!
 
Kwa katiba yetu ya sasa haiwezekani kwa kuwa inamtaka rais kuchagua mawaziri miongoni mwa wabunge wa chama chenye wabunge wengi.
 
Kwa katiba yetu ya sasa haiwezekani kwa kuwa inamtaka rais kuchagua mawaziri miongoni mwa wabunge wa chama chenye wabunge wengi.
si kweli. waziri mkuu tu ndio anatakiwa atoke kwenye chama chenye wabunge wengi. mathalani slaa angeshinda urais 2010 huku chama chake hakina wabunge wengi angelazimika kuchagua waziri mkuu toka ccm na kukaa naye kuunda baraza la mawaziri. hivyo katiba ya sasa inaruhusu mseto.
 
jk ni mjanja sana,imagine zitto anapewa nafasi ya mkullo..je atakataa uteuzi wa rais?


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
- Sio lazima tuige kila kitu cha US na infact wao siasa sio uadui kama sisi, sasa ukiingia mseto tu maana yake sasa mnakuwa CUF, yaani dead! Tunahitaji upinzani ili kurekebisha mambo kama ilivyo sasa!


William.
nakubaliana na wewe 100% pia sheria ya sasa haionyeshi njia/uwiano wa serikali ya mseto
 
CDM wanapaswa kusubiri kutwaa madaraka kamili 2015.
Tatizo sio kuwa waziri, ni mfumo mzima.
Wakiwa sehemu ya weak&corrupt system sasa, watakosa hoja baadae.
 
Wewe Malecela woga wako ni kuwa CDM ikikubali nafasi yeyote ya uwaziri chance ya mama yako kupata uwaziri itapungua kwa taarifa yako CDM hawataki nafasi kwenye hiyo serikali legelege

- ha! ha! ha! ha! Mkuu Great Thinker, anatakiwa kufikiri na kujadili taifa sio wazazi wa members wengine ni dalili ya kutokuwa na hoja, au?


William.
 
Come on man, give William a breakl! At least he is trying to do something for his country. He did not have do well at EALA but must you insult him like that? I may not agree with William's views all the time, but I give him respect for expressing them and standing up to be counted. If you are so passionate about our country, you should try to take part in its development!!

- Don't worry bro everything is under control so relax mkuu wangu!

William.
 
Kaka mbona we hukusubiri wakati wako wa kuingia EALA wakati unajua mama ako wa kambo na kibajajihawapatanibna CCM(magamba)wenzako ? Au ndo funika kombe...'Kuwa na subira pia maana Kibajaj nae kakukalia mbaya, anasema aishindwa babu hata mjukuu haezi
mkuu taratibu kidogo.
 
hili ni jambo linalotakiwa kufanyiwa kazi na CDM.vyeo vitamu lakini tukumbuke watu wanataka system overhaul na sio viongozi wachache kupewa vyeo na kujiondoa kwenye kundi la wapambanaji.mfano ni SITTA, MWAKYEMBE,SEIF
 
kibonzo 26 and 27 april.jpg
Nani atakubali mseto na huyu jamaa?
 
IFIKE MAHALI TUWE NA HILI KUWA UWAZIRI SI KAZI YA KUPEWA NA RAIS MTU AGOMBEE BUNGENI AWEKWE KWENYE KIYI MOTO ATUELEZE NI KWA NINI ANAOUMBA KUWA WAZIRI FULANI WAGOMBEE WATUELEZE MIKAKATI YAO YA KUONGOZA HIZO WIZARA,
Nadharia nzuri, lakini ukifika wakati wa utekelezaji kwa hili ndio mtalia zaidi kwani ikiwa chama kina wingi wa wabunge, kama ilivyo CCM hivi sasa, unaweza kukuta chama hicho kimeweka "mawe" na bado wanapita kwa kuwa wao ndio wenye wingi wa kura. Labda kuwe na kipengele cha "asilimia ngapi ya kura kutoka chama tawala na ngani toka upinzani".

Tatizo si uteuzi, nchi zote raisi/waziri mkuu huwa ndiye anayeteua mawaziri wake, tatizo ni kukosekana au kutotumiak sheria ya kuwawajibisha wanapofanya madudu. Mfumo wa China ninaupenda, kwanza ananyang'anywa kila senti aliyoiba halafu kitanzi. Sisi tungeweza kumsamehe na hicho kitanzi, kumnyang'anya tu alivyoiba ni sawa na kumpa kitanzi akajinyonge mwenyewe.
 
Wewe Malecela woga wako ni kuwa CDM ikikubali nafasi yeyote ya uwaziri chance ya mama yako kupata uwaziri itapungua kwa taarifa yako CDM hawataki nafasi kwenye hiyo serikali legelege
Kwa nini Mkuu hujadili hoja za William badala yake unamjadili yeye na wazazi wake? Kwenye siasa hiyo ni dhambi, lakini kule Chit Chat unaweza kufanya hivyo (ikiwa wenyewe watalikubali).

Samahani Mkuu lakini nadhani huo si ustaarabu, hasa kwa JF na kwa Great Thinkers.
"Let's dicuss motions not emotions"
 
  • Thanks
Reactions: Uda
Back
Top Bottom