wanajf juz kuna mtu alianzisha thread kuhusu baraza la mitihani kuwafanyia uhuni wanafunzi waliomaliza kidato cha sita mwaka huu ambao walifanya somo la maarifa ya kiislam lakini kwasababu ya ubaguzi wa kidini walionao baadhi yetu walimshambulia sana bila kujua kuwa jamaa alikuwa na uhakika, sasa imedhihirika necta tayari wamebadilisha matokeo hayo lakini tayari wameathiri mpangilio mzima wa matokeo ya mithani kwani baadhi ya shule zilionekana kuwa na div 0 na kwa sasa hazina kabisa,sasa kweli necta walishindwa kugawanya hizo alama au ni hila za kuwakatisha tamaa wanafunzi wa kiislam na kuchafua shule za kiislaam?