magufuli ana bana matumizi akitangaza mawaziri saivi gharama zitaongezeka so anasubiri haka kamwezi kaishe ili aanze kuwalipa mwezi ujao
Huku mikoani mambo shwari saaana. yaani kila ofisi wameanza kujiweka kwenye mstarii..wanajua panga linakuja.Mimi naona kama Dar es salaam ndo inaenda vizuri,maana uongozi umebaki Dar peke yake.
Habari zenu Wana JF,
Mimi si mjuzi sana wa mchakato mzima wa uteuzi katika nafasi mbalimbali mara baada ya Uchaguzi Mkuu kupita, lakini naona kama vile mara hii imechukua muda sana kwa baraza la mawaziri kuundwa.
Mi naona kama uvumilivu wangu unanishinda vile, nahitaji kweli kuona hao mini tingatingas watakaomsaidia Pombe. Ni lini atawatangaza?