Ole Shider
Member
- Oct 17, 2014
- 16
- 15
Kutoka Dodoma;
Pamoja na kutumia zaidi ya Milioni 50 Baraza kuu la Umoja wa Vijana wa CCM linaloendelea Dodoma Limemkaata kwa kauli moja Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Mizengo Pinda.
Pinda kakataliwa kuwa Naibu Kamanda wa Vijana Bara huku kwa upande wa Zanzibar Balozi Seif Iddy Makamu wa pili wa Raus akichukua nafasi hiyo na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akiendelea kutetea nafasi yake ya Kamanda Mkuu wa Vijana Taifa.
Jambo hili kimsingi limeonekana kuwa fedheha kubwa na aibu ya kufunga mwaka kwa Waziri Mkuu wa Taifa hili hasa ukizingatia kiasi cha pesa alichomwaka kwa Vijana Mkoani Dodoma.
Mwenyekiti wa Vijana kutoka Mkoa wa KATAVI Ndgu. Kelvin Mbogo ambaye ndiye anayetumika na Pinda kurubuni Vijana alisikika akilalamika kwa jazba na hasira hasa akielekeza lawama zake kwa Viongozi wakuu ambao ni Sadifa, Sixtus na bwana mmoja aliyemtaja kwa jina la Omary Sleiman; malalamiko ya Mbogo ni kwamba hao mabwana wamepewa fedha nyingi tena zingine kawakabidhi yeye mwenyewe ila wameshindwa kumtetea Pinda katika swala la Unaibu Kamanda hivyo wamemsaliti Mzee wao Asali.
"Hawa kina Sadifa na Sixtus na Sleiman ni washenzi na wapuuzi kweli kweli haiwezekani wachukue fedha zote hizo halafu washindwe kumtetea mzee. Ni wasaliti na wanafiki wakubwa na watarudisha fedha zote washenzi hawa" Alisikika akilalama bwana Mbogo.
Wajumbe wa Baraza hilo wengi wakionekana wenye Mapenzi mema na Lowassa walisikika wakisema katika hili lazma hili Baraza livunjwe hakuna mtu wa kulambishwa asali kisa Unaibu Kamanda...... Pinda abaki kuutaka Uraisi na Jumuiya hii aieche kabisa. Kuna waliotujengea Vitega Uchumi vya maana lakini wameshindwa kuwaona hao wanatuletea majina ya watangaza nia wa Uingereza na wa maembe.
Wachambuzi wa maswala ya kisiasa wamewapongeza sana Vijana kwa kulikataa jina la Pinda lakini vile vile wamesema hili ni aibu kubwa sana kwa mtu wa Kada ya Pinda ni bora wangemwacha mzee na nafasi zake za heshma kuliko kadhia na fedheha waliyomsababishia Pinda.
Kwa upande mwingine kuna baadhi ya Vijana walisikika wakisema Sadifa atakuwa amefanya hivyo kwa makusudi ili kumuumiza Pinda. "Jamani ni nani asiyejua mrengo wa Sadifa?? Halafu ngoja niwaambie watu huwa wanamwona Sadifa kama chizi lakini huyo jamaa na shidaaa ana akili zake mwenyewe. Sisi tunajua Sadifa ni wa Lowassa asilimi 1, 000 eti leo ampe Pinda Unaibu!! Sadifa kacheza Umafia na nakwambia Sadifa akitaka jambo lake lazma liwe sasa hili kalishindwa je?? Nyie acheni bana strategy za Lowassa Nchi hii hakuna mwenye uwezo nao....... Ona sasa walivyomtia aibu Mzee wa watu pamoja na Uwaziri wake Mkuu" Walisikika baadhi ya Vijana hapa Dodoma.......
Pinda alialikwa majuzi kufungua Semina ambapo pamoja na mengi Vijana wameshambatiza jina la mzee wa Maembe kutokana na kushawishi Vijana kumuunga mkono ktk upandwaji wa Maembe..........
Hili ni Aibu kubwa kwa Pinda ni Fedheha kubwa kwake, Ni kadhiha kubwa kwake na nafasi yake pia ukijumlisha na swala la IPTL mwelekeo wake kwisha........
UPDATE:
Pamoja na kutumia zaidi ya Milioni 50 Baraza kuu la Umoja wa Vijana wa CCM linaloendelea Dodoma Limemkaata kwa kauli moja Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Mizengo Pinda.
Pinda kakataliwa kuwa Naibu Kamanda wa Vijana Bara huku kwa upande wa Zanzibar Balozi Seif Iddy Makamu wa pili wa Raus akichukua nafasi hiyo na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akiendelea kutetea nafasi yake ya Kamanda Mkuu wa Vijana Taifa.
Jambo hili kimsingi limeonekana kuwa fedheha kubwa na aibu ya kufunga mwaka kwa Waziri Mkuu wa Taifa hili hasa ukizingatia kiasi cha pesa alichomwaka kwa Vijana Mkoani Dodoma.
Mwenyekiti wa Vijana kutoka Mkoa wa KATAVI Ndgu. Kelvin Mbogo ambaye ndiye anayetumika na Pinda kurubuni Vijana alisikika akilalamika kwa jazba na hasira hasa akielekeza lawama zake kwa Viongozi wakuu ambao ni Sadifa, Sixtus na bwana mmoja aliyemtaja kwa jina la Omary Sleiman; malalamiko ya Mbogo ni kwamba hao mabwana wamepewa fedha nyingi tena zingine kawakabidhi yeye mwenyewe ila wameshindwa kumtetea Pinda katika swala la Unaibu Kamanda hivyo wamemsaliti Mzee wao Asali.
"Hawa kina Sadifa na Sixtus na Sleiman ni washenzi na wapuuzi kweli kweli haiwezekani wachukue fedha zote hizo halafu washindwe kumtetea mzee. Ni wasaliti na wanafiki wakubwa na watarudisha fedha zote washenzi hawa" Alisikika akilalama bwana Mbogo.
Wajumbe wa Baraza hilo wengi wakionekana wenye Mapenzi mema na Lowassa walisikika wakisema katika hili lazma hili Baraza livunjwe hakuna mtu wa kulambishwa asali kisa Unaibu Kamanda...... Pinda abaki kuutaka Uraisi na Jumuiya hii aieche kabisa. Kuna waliotujengea Vitega Uchumi vya maana lakini wameshindwa kuwaona hao wanatuletea majina ya watangaza nia wa Uingereza na wa maembe.
Wachambuzi wa maswala ya kisiasa wamewapongeza sana Vijana kwa kulikataa jina la Pinda lakini vile vile wamesema hili ni aibu kubwa sana kwa mtu wa Kada ya Pinda ni bora wangemwacha mzee na nafasi zake za heshma kuliko kadhia na fedheha waliyomsababishia Pinda.
Kwa upande mwingine kuna baadhi ya Vijana walisikika wakisema Sadifa atakuwa amefanya hivyo kwa makusudi ili kumuumiza Pinda. "Jamani ni nani asiyejua mrengo wa Sadifa?? Halafu ngoja niwaambie watu huwa wanamwona Sadifa kama chizi lakini huyo jamaa na shidaaa ana akili zake mwenyewe. Sisi tunajua Sadifa ni wa Lowassa asilimi 1, 000 eti leo ampe Pinda Unaibu!! Sadifa kacheza Umafia na nakwambia Sadifa akitaka jambo lake lazma liwe sasa hili kalishindwa je?? Nyie acheni bana strategy za Lowassa Nchi hii hakuna mwenye uwezo nao....... Ona sasa walivyomtia aibu Mzee wa watu pamoja na Uwaziri wake Mkuu" Walisikika baadhi ya Vijana hapa Dodoma.......
Pinda alialikwa majuzi kufungua Semina ambapo pamoja na mengi Vijana wameshambatiza jina la mzee wa Maembe kutokana na kushawishi Vijana kumuunga mkono ktk upandwaji wa Maembe..........
Hili ni Aibu kubwa kwa Pinda ni Fedheha kubwa kwake, Ni kadhiha kubwa kwake na nafasi yake pia ukijumlisha na swala la IPTL mwelekeo wake kwisha........
UPDATE:
Salaam, kumekua na maneno mengi ya upotoshwaji kipindi hiki dhidi ya Mh. Pinda,yote yanatokana na hofu ya Lowassa na watu wake, Baraza kuu la umoja wa vijana halijajadili wala kuongelea swala la unaibu kamanda na wala halijafikishwa kwenye baraza kuu la vijana ni upotoshaji na uoga wa watu wa lowassa kutoka kukubalika kwa Pinda na kuonekana vijana wanamkubali na wanaweza kumpendekeza kuwa Naibu kamanda.
1) kama ukamanda UVCCM Taifa unauwezo wa kumpa mtu Urais basi mzee Kingunge angekuwa rais
2) Wajumbe wa baraza Kuu Taifa( Jumuiya zote ) hawaingii kwenye kikao cha kuweza kumtetea,kumzungumzia mgombea yeyote yule aliyetoswa na Chama Bali huingia kwenye kikao kimoja kinachowataka kuchagua mmoja kati ya watatu watakaofikishwa kwenye mkutano mkuu.
Hivyo kama kuna wajumbe wenye nguvu za kumjenga, kumuokoa ama kumtetea mgombea yeyote yule ni Kamati Kuu" CC" na "Nec"
Hivyo ni busara kutorubuni wasiojua wakati sote tunajua ukweli.
Ugawaji wa milioni 50!!
Haiingii akilini bali inadhihirisha ni kwa namna gani aliejitahidi kusambaza uvumi huo dhahifu amefirisika kifikra na ni mgeni hata wa kumiliki milioni moja.
Mbio za Urais ndio kwanza zimeanza, wenye vikao na wenye kura za maamuzi watathibitisha wanaemtaka.