Barak unfazed by criticism from Tanzania

Halafu hawa hawa Waisrael ndio baadhi ya Watanzania wanawapapatikia kuwa ni "taifa la mungu". bs.

hata nashangaa eti watu wanasema Tanzania ni nchi wakati ndani yake kuna mamlaka imebadili katiba, ikataja mipaka yake mipya, ikampa nguvu kiongozi wao na kuzinyang'anya za yule rais wa muungano, zikajiongezea viongozi wasiotambuliwa na katiba na kuilazimisha serikali ya muunganno kuwatambua na kuawapa heshima hao kama viongozi wa kitaifa.
Baada ya kudhalilika hivi bado nchi hii inataka kutambulika kama nchi na kupewa heshima sawa na nchi zinazojitambua.
 
Utawezaje kurudisha balozi wako toka Israel wakati unategemea Israel wakupe msaada kwa kilimo cha umwagiliaji kwenye nchi yako mwenyewe?

Pia unategemea Israel wakupe magari mawili matatu kwa bei ya kutupa kwa jeshi lako ili uonyeshe raia wako pale uwanja wa taifa kuwa jeshi liko ngangari kupasua mawe kwa vichwa kama Van damme na swazinigga ( Schwarzenegger) lakini yakitokea mafuriko jamaa wanaingia mitini na kuwaachia wavuvi wa Ferry...
:)..
Duh Nimecheka Mkuu Umesema bila kuacha Uongo...:biggrin:
 
Zamani nikiwa mdogo nilikuwa naaambiwa Tanzania ni ya pili kwa masuala ya upepelezi (intelijensia) nyuma ya Israel. Sasa ni zaidi ya miaka 25, bila shaka tulishaipita Israel siku nyingi sasa hivi sisi ni kwanza. Nadhani ndo maana huyu bwana anatuone wivu kwa kujaribu kutu ...debase...........Hata hivyo hapati kitu sisi tuko juu awaulize Amin na Uganda........................
Mkuu upo ok? au ndio Mwezi Mchanga?
 
Watanzania tuna matatizo sana, hatutaki kuambiwa ukweli. Barak kasema kweli sie ni irrelevant, mambo yetu ovyo kupita kiasi, angalia mchakato wa katiba mpya unavyoendeshwa kihuni, angalia sera ya kihuni ya kilimo kwanza, angalia jinsi tume ya uchaguzi ilivyo ya kihuni, angalia hata rais wa ccm anatumia urais kwenda kubembea, kutalii holywood na kuhongwa suti na waarabu, rais anasema hajui kwanini wananchi ni maskini, rais anasamehe wezi na hakuna anayemhoji. Sasa uongo wa Barak uko wapi? tena tushukuru amesema tuko irrelevant alitakiwa atuite machizi, wajinga na wapumbavu.
 
....It is a known fact that Israeli "entity" is a racist and facist one! The zionist entity does not think of other countries' rights except those that provide strategic and military support for its existence.There is no doubt that peripheral countries like Tanzania are lesser recognised and even not respected. It should be remembered that, Israeli is treating Palestine as an "Open Air Prison" and it kills people at the pretext of defending Israeli. If they (IDF) could kill at the "pretext" by the help of US and Allied military logistics; what Tanzania could offer to Israeli? It is high time now than ever for Tanzanians to stand firm and cherish her destiny...STOP LAMENTATIONS; IT IS THE TIME FOR TOUGH ACTIONS DESPITE OF OUR POLITICAL STANCE!
 
Ehud Barak , waziri wa ulinzi wa Israel, ametoa maneno ya kashfa dhidi ya Tanzania. Hayo yametokea pale waziri huyo asiye na heshima alipokuwa anahimiza Waisraeli wajishughulishe na nchi za Ulaya na kuzipuuza nchi za Kiafrika.
Huku akitumia, mtindo wa dharau na kebehi kubwa, Ehud Barak, ametolea mfano wa nchi zisizo na maana kuwa ni Tanzania, Mouritania na Tripolitania.
Wakati huo huo msimamizi wa ubalozi mdogo wa Tanzania nchini Israel, Bwana Altzanzy Noraal, kwa niaba ya serikali makini ya Tanzania, amepeleka barua rasmi ya malalamiko dhidi ya kebehi za Ehud Barak. Katika nakala za barua hiyo ambayo NIFAHAMISHE imebahatika kuona nakala yake, Mheshimiwa Altzanzy Noraal ameitaka serikali ya Israel ilaani vikali kauli za waziri Ehud.
Akiendelea kutoa malalamiko yake, Noraal, alimfafanulia waziri wa mambo ya nje wa Israel kuwa, Ehud ameamua kuidhalilisha Tanzania kwa kuifagilia Ulaya kiasi cha kuifanananisha Tanzania na nchi isiyokuwepo duniani, akimaanisha ile Tripolitania.
Noraal aliwahabarisha Waisrael kuwa Tanzania ni nchi kubwa kuliko zote za Afrika Mashariki ikiwa na idadi ya watu kama milioni 46. Huku akiikumbusha Israel uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Israel kiuchumi na kiusalama. “Tanzania ni nchi muhimu sana wala haipaswi kupuuzwa” amesema Bw. Noraal. “Nitafurahi sana nitakapotembelea Tanzania nikiwa na mwakilishi wa Israel ili aone uzuri wa Tanzania nchi yenye eneo kubwa na mazingira halisia na watu wanaopenda amani” amesisitiza kwa kuwakejeli kisiasa kwa namna wanavyopenda vita na Warabu kila kukicha.
 
Wale wazalendo wa Tanzania wako wapi Wajibu na kushughulikia jambo hili !!! Or they are busy ... Kuvuana Magamba ..yasiyovulika!!
 
Ni kweli walichosema Israel. We hebu ichunguze Tanzania vizuri bila bias, utaona ilivyo hovyo.
 
Ehud Barak , waziri wa ulinzi wa Israel, ... waziri huyo asiye na heshima alipokuwa anahimiza Waisraeli wajishughulishe na nchi za Ulaya na kuzipuuza nchi za Kiafrika.
... ametolea mfano wa nchi zisizo na maana kuwa ni Tanzania, Mouritania na Tripolitania.
...msimamizi wa ubalozi mdogo wa Tanzania nchini Israel, Bwana Altzanzy Noraal, kwa niaba ya serikali makini ya Tanzania, amepeleka barua rasmi ya malalamiko dhidi ya kebehi za Ehud Barak. Katika nakala za barua hiyo ambayo NIFAHAMISHE imebahatika kuona nakala yake, Mheshimiwa Altzanzy Noraal ameitaka serikali ya Israel ilaani vikali kauli za waziri Ehud.
... Ehud ameamua kuidhalilisha Tanzania kwa kuifagilia Ulaya kiasi cha kuifanananisha Tanzania na nchi isiyokuwepo duniani, akimaanisha ile Tripolitania.
Noraal aliwahabarisha Waisrael kuwa Tanzania ni nchi kubwa kuliko zote za Afrika Mashariki ikiwa na idadi ya watu kama milioni 46. Huku akiikumbusha Israel uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Israel kiuchumi na kiusalama. "Tanzania ni nchi muhimu sana wala haipaswi kupuuzwa" amesema Bw. Noraal. "Nitafurahi sana nitakapotembelea Tanzania nikiwa na mwakilishi wa Israel ili aone uzuri wa Tanzania nchi yenye eneo kubwa na mazingira halisia na watu wanaopenda amani" amesisitiza kwa kuwakejeli kisiasa kwa namna wanavyopenda vita na Warabu kila kukicha.

hahaha hana heshima kwako, wenzio wamempa uwaziri! nadhani ni haki waifagilie ulaya kwa kuwa ina wanafaidi kutoka huko, kwani hujui kuwa na sisi tunawategemea hao hao wa ulaya hadi ktk bajeti yetu? au unafikiri Kameruni alipata wapi ujasiri 'ule'? Tanzania ukiiweka kwenye mizani na ulaya sie tunainuka!
Ungeiweka basi hiyo barua ya Noraal hapa. Hapo cha maana alichofanya Noraal ni kuitangaza tu nchi yetu (kwenye bluu hapo juu). Kwa nini tung'ang'anie kusifiwa hata sifa tusizonazo? Tanzania na Ulaya wapi na wapi! tuwe wakweli jamani. Hapo kwenye red nawaachia wengine.
 
Ni kweli walichosema Israel. We hebu ichunguze Tanzania vizuri bila bias, utaona ilivyo hovyo.

Ni sawa kama mtu akutukanie mzazi wako. Hata kama wewe unajua kuwa mzazi wako ni hovyo, huwezi kukubali mtu mwingine amtukane. Lazima mkunjane mashati. Sasa unapoona nchi yako imekashifiwa lazima ukasirike. Ndiyo ubinadamu huo.
 
....Namkumbuka yule Mzanaki, hakupenda hata siku moja kuona au kusikia nchi yetu ikidhalilishwa kwa namna yeyote ile. Angemshasemea hovyo huyo Ehud Barak siku nyingi sana, lakini si huyu tuliyekuwa naye sasa hivi ambaye hata kutetea heshima ya nchi yetu tu anashindwa.
 
Ungetegemea baada ya safari za mkuu wa Tz zisizopungua 400 tangu aingie madarakani (JF data) kutembelea marekani na ulaya Tanzania ingekuwa inajulikana ipasavyo. Kumbe muisraeli Barak anatulinganisha na nchi ya kufikirika (imaginary) iitwayo TRIPOLITANIA. Wow.
 
Hajasema uongo,na tumeyataka wenyewe kwa kuachia wengine wavune rasilimali zetu watakavyo kama dhahabu nk, huku sie twazunguka dunia nzima na kibakuli cha kuomba! Tena twazunguka na misafara mikubwa ambayo hata wale wanene wa dunia hawatembei na robo yake! Yafaa matusi yaongezeke toka kila upande huenda tukazinduka kidogo na kuchukua hatua!
Nawasilisha!
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Acha tutukanwe Tanzania tumezidi upumbavu inakuwaje hawa waisrael watujengee UDSM, Bugando Hospital na taasisi mbalimbali pia kutoa mafunzo ya kijeshi kwa jeshi letu makanda wetu kama Luteni Jenerali Imran Kombe, Luteni Jenerali Silas Mayunga, Meja Jenerali Muhdini Kimario na wengine walipata mafunzo ya kijeshi Israel lakini tuliamua kuachana na Israel ili tujiunge na upande wa wapalestina wanaonyanyaswa na Israel tukidhania wapestina ni ndugu zetu na tunawalilia wajikomboe lakini matokeo yake wapestina hawatuthamini na wala hawatupi heshima inayostahili kwa kuwaunga mkono sisi na kujikuta tunapoteza manufaa mbalimbali kwa kuwa na urafiki na Israel.

Angalia Rais wa kwanza wa Tanzania aliyewapigania wapalestina alipofariki wapalestina hawakutuma ujumbe wowote wa juu ukiachilia Yasser Arafat mwenyewe kutohudhuria tulitegemea watu kama Mahmoud Dahlan, Ahmed Qurei, Sakri Habashi, Salim al-Zaanoun, Mahamoud Abbas au Saeeb Erakat mmoja wapo ahudhurie lakina hakuna isipokuwa balozi wa Palestina nchini Tanzania ndiye aliyehudhuria lakini wakati alipofariki Mfalme Hussein wa Jordan na Rais Hafidh Assad wa Syria ujumbe wa Palestina ulijazana kwenye mazishi kama njugu ndio nikagundua hawa jamaa hujali zaidi undugu wa kiarabu na sio undugu katika mapambano toka siku hiyo siwaoni wa maana tena, na kuwa upande wao Tanzania tunapoteza zaidi kuliko kupata manufaa nchi kibao na mataifa ya kiaarabu na kiislamu kama Mauritania, Niger, Misri, Jordan, Saud Arabia, Uturuki, Indonesia, Malaysia yana uhusiano wa karibu na Israel na yanafaidi kwanini sisi tujitenge na Israel kwa ajili ya watu wasio tunathamini matokeo yake tunaishia kuwa losers?

Kama haitoshi alipofariki Waziri Mkuu wa Israel Yizhaki Rabin bado wapalestina walituma ujumbe wa juu wa watu watatu sasa kama mtesaji wenu anafariki mnatuma ujumbe wa juu? kwanini anayewatetea anapofariki msitume ujumbe wa juu? lipi bora? jjbu hamthaminiki kivile kwa mnaowatetea.
 
wakati mwingine mtu hata kama hana nia ya kukutukana unakuta kwamba unatengeneza na kukaandaa mazingira ambayo kwa njia moja ama nyingine yanamlazimisha mtu huyo kukutukana! alichokisema waziri bila shaka kina ukweli ndani yake, heshima haiji kwa kumiliki ardhi au eneo kubwa bila kulitumia. . In fact, peace don't just means the absence of war! Watz wengi wamejuruhiwa, wana vidonda, & wanalia mioyoni mwao. Wengi wamekata tamaa ya maisha pamoja na uwepo wa rasilimali rukuki! Hapo mtu atashindwa kukutukana!
 
Acha tutukanwe Tanzania tumezidi upumbavu inakuwaje hawa waisrael watujengee UDSM, Bugando Hospital na taasisi mbalimbali pia kutoa mafunzo ya kijeshi kwa jeshi letu makanda wetu kama Luteni Jenerali Imran Kombe, Luteni Jenerali Silas Mayunga, Meja Jenerali Muhdini Kimario na wengine walipata mafunzo ya kijeshi Israel lakini tuliamua kuachana na Israel ili tujiunge na upande wa wapalestina wanaonyanyaswa na Israel tukidhania wapestina ni ndugu zetu na tunawalilia wajikomboe lakini matokeo yake wapestina hawatuthamini na wala hawatupi heshima inayostahili kwa kuwaunga mkono sisi na kujikuta tunapoteza manufaa mbalimbali kwa kuwa na urafiki na Israel.

Angalia Rais wa kwanza wa Tanzania aliyewapigania wapalestina alipofariki wapalestina hawakutuma ujumbe wowote wa juu ukiachilia Yasser Arafat mwenyewe kutohudhuria tulitegemea watu kama Mahmoud Dahlan, Ahmed Qurei, Sakri Habashi, Salim al-Zaanoun, Mahamoud Abbas au Saeeb Erakat mmoja wapo ahudhurie lakina hakuna isipokuwa balozi wa Palestina nchini Tanzania ndiye aliyehudhuria lakini wakati alipofariki Mfalme Hussein wa Jordan na Rais Hafidh Assad wa Syria ujumbe wa Palestina ulijazana kwenye mazishi kama njugu ndio nikagundua hawa jamaa hujali zaidi undugu wa kiarabu na sio undugu katika mapambano toka siku hiyo siwaoni wa maana tena, na kuwa upande wao Tanzania tunapoteza zaidi kuliko kupata manufaa nchi kibao na mataifa ya kiaarabu na kiislamu kama Mauritania, Niger, Misri, Jordan, Saud Arabia, Uturuki, Indonesia, Malaysia yana uhusiano wa karibu na Israel na yanafaidi kwanini sisi tujitenge na Israel kwa ajili ya watu wasio tunathamini matokeo yake tunaishia kuwa losers?

Kama haitoshi alipofariki Waziri Mkuu wa Israel Yizhaki Rabin bado wapalestina walituma ujumbe wa juu wa watu watatu sasa kama mtesaji wenu anafariki mnatuma ujumbe wa juu? kwanini anayewatetea anapofariki msitume ujumbe wa juu? lipi bora? jjbu hamthaminiki kivile kwa mnaowatetea.
.................. hapo bold (red) unaweza kufafanua zaidi ? .................. yaaani kuonyesha kwa ushahidi jinsi yalivyonufaika, haswa Saudia, Indonesia !
 
ShowImage.ashx

Photo by: Ariel Harmoni / Defense MinistryBy GIL HOFFMAN
12/27/2011 19:21

Refuses to apologize to African country after it protests being called "irrelevant."



Defense Minister Ehud Barak has declined to apologize to Tanzania, despite a letter from the African country protesting a Barak statement that its representatives in Israel found offensive, a Barak associate said Tuesday.

In an interview with Israel Radio's Ayala Hasson last Thursday, Barak criticized theForeign Ministry for warning that adopting the Palestinian position on how to advance diplomatic talks would make England, France, and Germany irrelevant.


"Germany, France and England are not Tanzania, Mauritania or Tripolitania [a region in Libya]," said Barak, noting places whose names rhyme with England in Hebrew. "These are very important, very relevant countries and we don't have an interest in increasing tensions with them or making them bitter enemies."

Tanzania's honorary consul in Israel, Kasbian Nuriel Chirich, wrote a letter to ForeignMinister Avigdor Lieberman condemning Barak's remarks and inviting a representative of Israel to visit his country.



In this effort to praise theimportance of key countries in Europe, he chose to put down Tanzania and compare it to a country that doesn't even exist," Chirich wrote. "Tanzania is the largest country in East Africa, rich in natural resources, with a population of some 46 million peace seeking people and a gross domestic product of more than 58 billion dollars.


Chirich noted that Israel andTanzania have had diplomatic, security, and economic relations since Tanzania's independence and that Prime Minister Binyamin Netanyahu has recently met African leaders in an effort to deepen ties with the continent amid the strengthening of Islamic extremism there.

"Tanzania is an important country that Israel should not ignore," Chirich wrote.

Barak's associates said he did not intend to express regret for his statements aboutTanzania, which they said Barak had made on multiple occasions.

"Maintaining relations with England, Germany, and France is indeed more urgent for Israel than with Tanzania, which has less influence from Israel's standpoint," a source close to Barak said.


Dharau hii kwa Tanzania pamoja na kutokubalika inaoenyesha kushuka kwa umahiri wa viongozi wetu katika suala la Foreign Policy.
Inaelekea Policy hii ambayo imejikita katika suala la "omba omba" ndilo linalotudhalilisha sana kama watanzania.
Tumejidharau na tuna dharaulika.
Mimi sidhani kama Waziri Mkuu hyo wa Israel kasema aliyosema bila ya kuwa na utafiti nyuma yake.
Waisrael wamekuwapo hapa Tanzania toka zamani, maea baada ya Uhuru miaka 50 iliyopita.Kuwaomba watutake radhi ni kazi bure, tatizo liko kwetu sisi wenyewe.
Pamoja na kuweka kipaumbele katika uhusiano wa kibiashara, inabidi Waziri Membe na timu yake na Serikali kwa ujumla wafungue macho na kupata Foreign Policy inayoeleweka.
Mimi sishangai maana Ehud Barak si wa kwanza kutoa dharau hizi.
Hata Cameron alishauri tuwe mashoga ili tumapate misaada!
Tufiche wapi sura zetu duniani kwa Dharau kama hizi!
 
Lazima ifike wakati tuwe wakweli,Ehud yupo sawa kabisa,nani leo anayeweza kusimama na kusema we are not irrelevant,who?Rais kila siku anasema ana kwenda nje kuhemea,akirudi anarudi na kibaba sawa, kwanini tuna shindwa kustahimili matusi wakati tumejitakia wenyewe!Hatukuwa na tabia ya kuomba omba,kwani hata Matonya huwa akizidi hutukanwa kila kona leo tunafoka nini.Tunagawa ardhi yenye kila utajiri kwa kupewa chandarua kweli!Kila siku migogoro ya ardhi inaibuka kati ya wananchi na wakoloni wawekezaji serikali inazungumza nini zaidi ya kulala usingizi kama vile nchi iko likizo.Mikataba feki kila siku kwa aajili ya kuwanufaisha wachumie tumbo wachache na familia yao.Kila aliyepewa dhamana ya kuongoza amegeuka kuwa chinja chinja na mbakaji wa mali ya umma.Na bado tuna subiri matusi zaidi.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
hata nashangaa eti watu wanasema Tanzania ni nchi wakati ndani yake kuna mamlaka imebadili katiba, ikataja mipaka yake mipya, ikampa nguvu kiongozi wao na kuzinyang'anya za yule rais wa muungano, zikajiongezea viongozi wasiotambuliwa na katiba na kuilazimisha serikali ya muunganno kuwatambua na kuawapa heshima hao kama viongozi wa kitaifa.
Baada ya kudhalilika hivi bado nchi hii inataka kutambulika kama nchi na kupewa heshima sawa na nchi zinazojitambua.

Mkuu, hili nalo neno.
ngoja tuone mjanja!
 
huyu barak aache dharau za kijinga kwani hata wao hawana msaada wowote kwetu.huwezi ukalinganisha umuhimu wa US,UK,SCANDINAVIAN COUNTRIES,CHINA kwa Tanzania ukilinganisha na Israel hivyo kama vipi watupotee tu na hatuwahitaji.Ngoja tuanze kuwaita Iran waje wavune Uraniaum ndo watajua umuhimu wetu kwao.


Umuhimu wa hizo nchi ulizotaja kwa Tanzania ni upi kama siyo sisi kuomba misaada? Tukidai tunawasaidia kiuchumi itakuwa ni through wao kuchukua (siyo kuiba) resources zetu kwa bei ya kutupa kwa sababu ya ujinga wetu. Alichosema Ehud ni kweli kwa kuwa Tanzania haina maslahi kwa Israel, huu ni ukweli unaofahamika, suala ni kuwa tulitaka awaze kimyakimya ila asiseme.

Ukiwa ombaomba utadharaulika tu. Msijidanganye na "Uzalendo" ilhali mnafanya mambo ya kujiaibisha. Kuomba si vibaya, kuombaomba ni vibaya.
 
Back
Top Bottom