Mshobaa
JF-Expert Member
- Apr 7, 2013
- 1,678
- 595
Habari wakuu,
Mnamo mwaka Jana zilikuja taarifa hapa juu ya hii barabara ya Goba mpakani ilivyokuwa hatarishi kupitika baada ya kupigiwa kelele hapa hapa jamvini wahusika mara moja wakaenda kuichonga.
Sasa basi hii barabara kwa kweli ina hali mbaya sana kwa sasa, wahusika ni Kama hawaioni kabisa. Baada ya kufatilia hili suala kwa kina nimegundua yafuatayo..,
Kuna bajaj zipo eneo la Tegeta A zinafanya rout kutoka hapo hadi mwisho yani Goba mpakani, ambazo ni mradi wa kigogo mmoja wa eneo hilo mwenye mamlaka.
Barabara haichongwi kwa maslahi yake binafsi maana gharama ya usafiri kutoka hapo Tegeta A hadi Goba mpakani ni tsh 1500 had 2000 wakati hapo mwanzo nauli ilikuwa kati ya 500 hadi 800 tu.
Ombi langu kwa Tarura na halmashauri ya manispaa ya Ubungo muwe mnatembelea hizi barabara kujionea wenyewe badala ya kukaa maofisini na kusubiria kuletewa taarifa, hivi majuzi kuna lori kubwa la mchanga lilidumbukia kwenye mojawapo ya mashimo hayo na kupinduka miguu juu.
Bahati nzuri ilikuwa ni usiku ingekuwa mchana tungesema mengine hapa maana eneo hilo kuna watu wengi wanapita na kufanya shughuli zao.. Pia kesho yake gari ya abiria ikapinduka na abiria wake.. Tusisubirie hadi yatokee maafa ndio tuje kupeana pole za kinafiki hapa.......
Mnamo mwaka Jana zilikuja taarifa hapa juu ya hii barabara ya Goba mpakani ilivyokuwa hatarishi kupitika baada ya kupigiwa kelele hapa hapa jamvini wahusika mara moja wakaenda kuichonga.
Sasa basi hii barabara kwa kweli ina hali mbaya sana kwa sasa, wahusika ni Kama hawaioni kabisa. Baada ya kufatilia hili suala kwa kina nimegundua yafuatayo..,
Kuna bajaj zipo eneo la Tegeta A zinafanya rout kutoka hapo hadi mwisho yani Goba mpakani, ambazo ni mradi wa kigogo mmoja wa eneo hilo mwenye mamlaka.
Barabara haichongwi kwa maslahi yake binafsi maana gharama ya usafiri kutoka hapo Tegeta A hadi Goba mpakani ni tsh 1500 had 2000 wakati hapo mwanzo nauli ilikuwa kati ya 500 hadi 800 tu.
Ombi langu kwa Tarura na halmashauri ya manispaa ya Ubungo muwe mnatembelea hizi barabara kujionea wenyewe badala ya kukaa maofisini na kusubiria kuletewa taarifa, hivi majuzi kuna lori kubwa la mchanga lilidumbukia kwenye mojawapo ya mashimo hayo na kupinduka miguu juu.
Bahati nzuri ilikuwa ni usiku ingekuwa mchana tungesema mengine hapa maana eneo hilo kuna watu wengi wanapita na kufanya shughuli zao.. Pia kesho yake gari ya abiria ikapinduka na abiria wake.. Tusisubirie hadi yatokee maafa ndio tuje kupeana pole za kinafiki hapa.......