Undava King
JF-Expert Member
- Aug 11, 2017
- 3,205
- 5,334
Kwa kipindi kirefu tumekuwa na tatizo sugu la ajali za barabarani chanzo kikuu kikiwa ni uendeshaji usiofuata taratibu na kanuni za usalama barabarani pamoja na ubovu au uchakavu wa vyombo vya moto huku tukifumbia jicho suala la utoshelevu na ubora wa miundombinu yetu.
Ajali za barabarani haziwezi epukika kamwe kwa njia moja tu ya kudili na madereva hili wasifanye makosa ya barabarani na kuhakiki uhalali wa leseni zao.
Ajali za barabarani zitaepukika pale tutakapo kiri kwa dhamiri zetu kama taifa kuwa tuna miundombinu duni na hafifu isiyoendana au kukidhi uhitaji wa wakati tulionao hivi sasa.
Ni ukweli usiopingika kwa takwimu kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye barabara zenye ubora duni lakini pia mtandao mdogo wa barabara za lami ukilinganisha na nchi zinazotuzunguka hapa Afrika ya mashariki na Afrika pia, kama taifa lenye amani na wingi wa maliasili hili si jambo la kujivunia.
Kiuhalisia ni wazi kuwa imefikia wakati barabara kuu ya Dar es salaam mpaka Mwanza itanuliwe na kuwa njia sita (6) kwani imeshazidiwa na idadi ya magari pamoja na watumiaji wengine wa barabara hii.
Ambapo ndani ya njia sita (6) hizo; njia mbili (2) zitumike kama njia za malori, njia mbili zingine (2) Mabasi na njia mbili zilizobakia (2) Magari madogo.
Hii itasaidia kuepusha overtaking zinazosababisha ajali za mara kwa mara katika barabara hii ambayo ina-accommodate kwa wakati mmoja mamia ya malori ya mizigo(yanayoendeshwa taratibu),mabasi ya masafa marefu (yanayohitaji kufika kwa wakati),magari madogo(yanayohitaji kuokoa muda na kufika haraka), bajaji, pikipiki, n.k ndani ya lanes 2 pekee ni vurugu mechi na kuweka maisha ya mtumiaji rehani licha ya umuhimu mkubwa wa barabara hii katika uchumi wa nchi.
Naamini kama serikali iliamua kufunga mkanda na ikaweza kujenga reli ya kisasa ya matrilioni ya shilingi kwa manufaa mapana ya uchumi wa nchi haiwezi kushindwa pia kulisimamia hili na likatekelezeka.
Ukweli ni kuwa suala hili la upanuzi wa barabara hii ambayo ni kitovu cha uchumi wetu alijapewa kipaumbele kinachostahili na serikali yetu pengine kwa kuchelea kuwa kwa kuwa tutakuwa na reli mpya basi pengine hatutokuwa na uhitaji wa barabara ya namna hii kwa wakati huu.
Hili linaonekana wazi katika utekelezaji wa kusuasua wa barabara ya njia nane ya Dar to Kibaha lakini pia utafutaji wa mwekezaji binafsi wa njia nne za pembeni ya zile mbili zilizopo sasa kwa njia ya Kibaha to Morogoro,
Kwa maoni yangu nilitamani serikali ilisimamie hili kwa rasilimali na nguvu zake yenyewe japo sikatai uwekezaji binafsi ila katika barabara hii umuhimu wake katika uchumi wetu ni mkubwa na unapaswa kuzingatiwa.
Idadi ya watu,idadi ya magari ya abiria na mizigo inazidi kuongezeka siku hadi siku huku miundombinu ikibakia ile ile na inaendelea kuzidiwa,
Huku ikionekana dhahiri kuwa serikali ina kasi ndogo na pengine inasuasua katika ujenzi wa barabara za lami kwa wakati na kuendana na uhitaji.
Mfano jiji la Mwanza lina uhitaji ulio dhahiri katika upanuzi wa barabara zake kuu kutoka njia mbili za hivi sasa hadi nne ndiyo kipaumbele na tiba ya foleni kubwa ya magari katika barabara zake muhimu lakini cha kushangaza itachukua karne mpaka serikali ichukue hatua katika hili.
Ajali za barabarani haziwezi epukika kamwe kwa njia moja tu ya kudili na madereva hili wasifanye makosa ya barabarani na kuhakiki uhalali wa leseni zao.
Ajali za barabarani zitaepukika pale tutakapo kiri kwa dhamiri zetu kama taifa kuwa tuna miundombinu duni na hafifu isiyoendana au kukidhi uhitaji wa wakati tulionao hivi sasa.
Ni ukweli usiopingika kwa takwimu kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye barabara zenye ubora duni lakini pia mtandao mdogo wa barabara za lami ukilinganisha na nchi zinazotuzunguka hapa Afrika ya mashariki na Afrika pia, kama taifa lenye amani na wingi wa maliasili hili si jambo la kujivunia.
Kiuhalisia ni wazi kuwa imefikia wakati barabara kuu ya Dar es salaam mpaka Mwanza itanuliwe na kuwa njia sita (6) kwani imeshazidiwa na idadi ya magari pamoja na watumiaji wengine wa barabara hii.
Ambapo ndani ya njia sita (6) hizo; njia mbili (2) zitumike kama njia za malori, njia mbili zingine (2) Mabasi na njia mbili zilizobakia (2) Magari madogo.
Hii itasaidia kuepusha overtaking zinazosababisha ajali za mara kwa mara katika barabara hii ambayo ina-accommodate kwa wakati mmoja mamia ya malori ya mizigo(yanayoendeshwa taratibu),mabasi ya masafa marefu (yanayohitaji kufika kwa wakati),magari madogo(yanayohitaji kuokoa muda na kufika haraka), bajaji, pikipiki, n.k ndani ya lanes 2 pekee ni vurugu mechi na kuweka maisha ya mtumiaji rehani licha ya umuhimu mkubwa wa barabara hii katika uchumi wa nchi.
Naamini kama serikali iliamua kufunga mkanda na ikaweza kujenga reli ya kisasa ya matrilioni ya shilingi kwa manufaa mapana ya uchumi wa nchi haiwezi kushindwa pia kulisimamia hili na likatekelezeka.
Ukweli ni kuwa suala hili la upanuzi wa barabara hii ambayo ni kitovu cha uchumi wetu alijapewa kipaumbele kinachostahili na serikali yetu pengine kwa kuchelea kuwa kwa kuwa tutakuwa na reli mpya basi pengine hatutokuwa na uhitaji wa barabara ya namna hii kwa wakati huu.
Hili linaonekana wazi katika utekelezaji wa kusuasua wa barabara ya njia nane ya Dar to Kibaha lakini pia utafutaji wa mwekezaji binafsi wa njia nne za pembeni ya zile mbili zilizopo sasa kwa njia ya Kibaha to Morogoro,
Kwa maoni yangu nilitamani serikali ilisimamie hili kwa rasilimali na nguvu zake yenyewe japo sikatai uwekezaji binafsi ila katika barabara hii umuhimu wake katika uchumi wetu ni mkubwa na unapaswa kuzingatiwa.
Idadi ya watu,idadi ya magari ya abiria na mizigo inazidi kuongezeka siku hadi siku huku miundombinu ikibakia ile ile na inaendelea kuzidiwa,
Huku ikionekana dhahiri kuwa serikali ina kasi ndogo na pengine inasuasua katika ujenzi wa barabara za lami kwa wakati na kuendana na uhitaji.
Mfano jiji la Mwanza lina uhitaji ulio dhahiri katika upanuzi wa barabara zake kuu kutoka njia mbili za hivi sasa hadi nne ndiyo kipaumbele na tiba ya foleni kubwa ya magari katika barabara zake muhimu lakini cha kushangaza itachukua karne mpaka serikali ichukue hatua katika hili.