Barabara ya Bumbuli jimboni kwa January Makamba

Barabara ya Bumbuli jimboni kwa January Makamba

Hizi thread zingine mnazianzisha ilimradi muweze kujifirahisha na kurusha mawe. Mtu yoyote mwenye uelewa kidogo zaidi ya punje ya mchele anajua kazi kubwa iliyofanyika Bumbuli ndani ya miaka 4 iliyopita.

Yaani, kwa mtazamo wangu kitendo cha thread zinazohusu maendeleo ya Bumbuli kuongelewa sana, inaonyesha tu January amefanikiwa kuiweka Bumbuli kwenye ramani. Maana watu hawajadili Monduli, Karatu, Hai, Arusha mjini, Mtama, Mpanda, nk. Big up JM.

mkuu selemani HIVI KAMA BARABARA IKO NAMNA HII KWA MVUA HIZI ZA MAEMBE , JE ITAKAPOFIKA MASIKA ITAKUWAJE ?
 
mkuu jamaa alimaanisha jimbo lilianzishwa na Shelukindo miaka 15 iliyopita, hakutaja habari ya kuwa halmashauri, Janauary ndo alianza na ikawa halmashauri miaka 4 iliyopita,

zumbe hujamuelewa yeye anadai kuna wilaya zee zaidi ya hiyo na hali ni duni kwa maana kuwa ccm hawafanyi lolote.
 
1. bumbuli haikuwa halmashauri kabla ya kuingia January na sasa ni halmashauri na unajua ni kiasi gani sehemu inapokuwa na halmashauri watu wanafaidika. Walimu ilikuwa ni vurugu kila mara kukimbilia Lushoto mjini wanapokuwa na matatizo lakini sasa hivi mambo yote ni BUMBULI.
2 Kuna ATM machine inaaa anzishwa palepale kwahiyo adha ya kukimbia hadi Lushoto itapungua.
3.Amewasaididia vijana wengi kukosoma kwa kupitia mfuko wa jimbo.
4. Amekuwa mhamasishaji mzuri katika mabmo ya elimu kwa walimu na wanafunzi.
5. Barabara ya soni Bumbuli ipo ktk kiwango kizuri sana ispokuwa sehemu ndogo tu ya kutoka Kwehangala hadi kibaoni na hiyo sehemu ya pasua na tatizo kubwa pale pasua ni molamu iliotumika.
6. Bado yupo katika harakati za kufugua kiwanda cha Mponde ambacho SHELUKINDO kwa dhulma kabisa akiwa ameungana na mwekezaji wanawakomoa wananchi wa mponde.
7. Kuna BDC ambayo inahusika sana na maendeleo ya jimbo la BUMBULI.

HAYO NI BAADHI TU.

Ndugu yangu CHAMVIGA
1. Hilo Suala la halmashauri January amelikuta na limeasisiwa na Shelukindo ndiye aliyeanzisha mchakato wa Kuifanya halmashauri.
2. Hayo mengine yote uliyotaja nafahamu hata wewe mwenyewe unajua kuwa ni porojo kwa sababu hizo ATM sio za serikali. Ishu za elimu, afya etc kwa kifupi ndio zinazidi kurudi nyuma badala ya kuboreshwa, mponde kachamka, hiyo BDC ni chombo cha kupigia dili tu 2ala haina msaada wowote kwa mwananchi wa kawaida wa Bumbuli.
 
Last edited by a moderator:
Yaani hili ni JIMBO JIPYA halina hata MIAKA 15; Lilianzishwa na Mzee Shelukindo; Sasa unataka liwe na kila kitu sababu tu MAKAMBA ni MBUNGE?

What a JOKE... inaonyesha ni baadhi ya sisi wananchi ndio tumechoka hatujui Maendeleo ni nini



c.c NOT FOUND
tukikupa mfano wa jimbo kama hilo lenye barabara safi za lami utanena nini?
 
Mkuu nngu007
Sitaki kuamini kama uwezo wako wa kufikiria umefikia hapo, wewe unavyoona hiyo bara bara huoni kunahitajika kitu kifanyike? So kigezo chako ni miaka 15, real? :sad:

Utekelezaji wa shughuli za ujenzi wa miundombinu ya barabara inapatikana kwenye mpango wa taifa wa miaka mitano hivyo barabara ya mbumbuli itajengwa chini ya mpango huo si kwa sababu makamba anataka kugombea urais! Aidha, unaonesha jamii kuwa wewe unajenga hoja usiyoiamini. Hatuwezi kusema kwamba makamba atagombea urais siku matatizo ya wana-mbumbuli yakiisha, anagombea ili apate fursa ya kutoa mchango wake dhidi ya changamoto zilizopo.
 
Utekelezaji wa shughuli za ujenzi wa miundombinu ya barabara n.k inapatikana kwenye mpango wa taifa wa miaka mitano hivyo barabara ya mbumbuli itajengwa chini ya mpango huo si kwa sababu makamba anataka kugombea urais! Aidha, unaonesha jamii kuwa wewe unajenga hoja usiyoiamini. Hatuwezi kusema kwamba makamba atagombea urais siku matatizo ya wana-mbumbuli yakiisha, anagombea ili apate fursa ya kutoa mchango wake dhidi ya changamoto zilizopo.
 
....anagombea ili apate fursa ya kutoa mchango wake dhidi ya changamoto zilizopo.

Sasa kama changamoto za jimbo la Bumbuli zinamshinda ataweza changamoto za Tanzania nzima??
 
Yaani hili ni JIMBO JIPYA halina hata MIAKA 15; Lilianzishwa na Mzee Shelukindo; Sasa unataka liwe na kila kitu sababu tu MAKAMBA ni MBUNGE?

What a JOKE... inaonyesha ni baadhi ya sisi wananchi ndio tumechoka hatujui Maendeleo ni nini



c.c NOT FOUND

Inachumua muda gani kuweka vitu muhimu kwa maendeleo kama vile barabara katika jimbo jipya ?
 
Yaani hili ni JIMBO JIPYA halina hata MIAKA 15; Lilianzishwa na Mzee Shelukindo; Sasa unataka liwe na kila kitu sababu tu MAKAMBA ni MBUNGE?

What a JOKE... inaonyesha ni baadhi ya sisi wananchi ndio tumechoka hatujui Maendeleo ni nini



c.c NOT FOUND
Kwani hilo jimbo limetoka mbinguni au lilikuwepo Enzi zote za utawala wa CCM?
 
Kuna wakati wowote toka Tanzania i pâté Uhuru kumtengenezwa Barabara nyingi zaidi ya huu wa Kikwete?Serikali inayoongozwa na Kikwete iliweka wazi ms imams wake kuhusu mawasiliano ya barabara, kwanza za kuunganisha mikoa, halafu za kuunganisha wilaya, halafu za kuunganisha vijiji.Naam, tumeona mafanikio makubwa sana, sasa hivi karibia mikoa yote inaunganishwa kwa barabara za kiwango cha lami na ambazo bado basi wakandarasi wako kazini.

Na hakuna wakati wowote toka Tanzania ipare uhuru nchi imeingia kwenye madeni makubwa yasiyolipika zaidi ya huu wa Kikwete.

Na hakuna wakati wowote toka Tanzania ipate uhuru rasilimali za nchi zimechotwa na wageni kama nchi haina mwenyewe wala serikali zaidi ya huu wa Kikwete.

Na hakuna wakati wowote toka Tanzania ipate uhuru ufisadi wa wizi wa mali ya umma umekithiri kwa kiwango cha juu zaidi ya huu wa Kikwete.

nakadhalika, nakadhalika.....
 
Yaani hili ni JIMBO JIPYA halina hata MIAKA 15; Lilianzishwa na Mzee Shelukindo; Sasa unataka liwe na kila kitu sababu tu MAKAMBA ni MBUNGE?

What a JOKE... inaonyesha ni baadhi ya sisi wananchi ndio tumechoka hatujui Maendeleo ni nini



c.c NOT FOUND


Mkuu acha utani ina maana miaka kumi tana iliyopita Bumbuli kulikua hakuna watu kabisa au ndio hilo jimbo lilishuka kutoka Mbinguni? miaka 15 ni michache kujenga barabara? mnahitaji miaka mingapi ili hiyo kazi ifanyike?
 
these are africa problems, huwezi taka within a very short time akaweka lami kila barabara, kina mtaa kila kona , tuko africa yenye changamoto na umasikini wetu, usimuhukumu Makamba kwa matatizo ya kitaifa na africa na umasikini wetu
 
Yaani hili ni JIMBO JIPYA halina hata MIAKA 15; Lilianzishwa na Mzee Shelukindo; Sasa unataka liwe na kila kitu sababu tu MAKAMBA ni MBUNGE?

What a JOKE... inaonyesha ni baadhi ya sisi wananchi ndio tumechoka hatujui Maendeleo ni nini
sasa unataka january afanyaje?jimbo amelikuja na lilikuwa na mbunge lakini hakufa chochote na hivi sasa ndio kalichukua makamba ndio yupo analifanyia kazi.


c.c NOT FOUND

january ndio jembe lao bumbuli.
 
Tatizo la huyu kijana naye anajifananisha na akina Zitto, Mnyika, Silinde nk, huyu yeye amebebwa na usije kuta hata alivalishwa 'pampers' udogoni lakini hawa wenzake ni vijana halisi wa Kitanzania na walivalishwa vipande vya kanga mbovumbovu kama napkins. Pia hawa vyeo vyao na ubunge wameupigania yeye kazawadiwa. Hatutaki aibu zaidi ya tuliyoipata nchi hii!
 
Budget zipo je? Wakatai wanashinda angani na kulala angani? Wanapiga deal za maana wewe unaulizia habari za Budget ndani la SERIKALI CORRUPT YA MACCM???????!
Navyojua mimi mpumbavu ni yule asie elewa sasa umeshaambiwa usimamizi wa barabara upo chini ya wizara ya ujenzi, zingine zipo chini ya ofisi ya waziri mkuu na serikari za mitaa unajuaje mipango na budget zao hizo sehemu na mikakati yao au unafikiri mmbunge anatakiwa ajenge kwa hela zake mwenyewe hizo barabara kama jamaa hawapo tayari mwerevu wewe?
 
Tunajua kilicho kichwani mwako mkuu..ila wakati mwingine usijistahi.."tunakuheshimu uje" usifanye tukakukosea abdabu bure!!
mkuu hujapatikana (not found), kijana anafanya kazi nzuri sana, na tena kwa 2015, atatufaa sana kule juu!, kama kigezo ndio hiyo barabara, ulipaswa kuipiga picha wakati alipoingia na kuipiga tena sasa!, unaona wazi kabisa, barabara hiyo imechongwa angalau sasa mabasi yanapita!, kabla ya hapo si nimlikuwa mnalazimika kugeuzwa mizigo kwa kupanda mikokoteni?!.

Barabara imechongwa na bahati mbaya mungu kaleta mvua mapema kabla haijakomaa!, hii ni dalili nzuri ya uletaji maendeleo, inabidi yaletwe kidogo kodogo ili mummpe miak mitano mingine ya kumalizia hiyo barabara!.

Tukiamua kuwapima wagombea wetu kwa kigezo cha kutuleta maendeleo kwa kipimo wamefanya nini, hakuna mgombea yoyote wa kushindana na yule "jamaa yangu!", ila ili kuleta kipimo cha haki, inabidi tuletewe humu precedence ya mwinyi alifanya nini kabla kustahili ofisi ile?!, mkapa alifanya nini kabla kustahili ofisi ile?!, na jakaya alifanya nini kabla kustahili ofisi ile?!, ndipo tulinganishe na huyu kijana amefanya nini kustahili ofisi ile!.

Nasisitiza kijana namfahamu, anafaa!.

Pasco
 
DAH!! inanikumbusha mbali sana enzi hizo miaka ya 89-93 hapo tarime kwenye kadaraja magari yalikuwa yanatereza yaani siku mvua ikinyesha mnaenda kujionea sinema ya bure.

Mbunge inabidi upige kelele sana watu wako wanasafa eti.
 
Badala ya kwenda kuwauliza TANROADS mnamuuliza January haya sasa ndio matatizo. Au labda tumezoea kufanya mambo bila ya taratibu si ndio hoja ya January hiyo.

Kwa utaratibu huu mwishowe tutawauliza watu wamungu mbona majumba yao ya ibada ayajai kisa mtaa unawaumini wasioudhuria Ibada.

Sasa wlimchagua ili afanye nini huyu shoga.
 
Kama mbunge huwa anajua barabara si kazi yake iweje wakati wa Kampeni huwa wanawahidi wananchi barabara nzuri? ina Maana ahadi za mbunge wakati wa kampeni zilikuwa za Uongo?
Ulisikia akisema atapeleka barabara Bumbuli isitoshe wananchi wanavipaumbele vingi cha muhimu ni yale mahitaji basic na watu wameanza kuridhika hapo kwa mujibu wa selemani.

Jumlisha the fact taifa lina limited resources na maamuzi ya wengi kwenye serikari za mitaa sasa kama wengine wana priority zingine za jimbo unawashawishi vipi mtu mmoja na wote ni stakeholder ndani ya jimbo?

Next time kama barabara ndio kipaumbele chao kuliko ubora wa elimu, masoko wanayolilia na mahitaji mengine wahakikishe viongozi wa serikari za mitaa kuanzia kwenye uchaguzi unaokuja na serikari kuu mwakani wanaelewa kabisa kuwa wanabumbuli wanahitaji lami kwanza or else viongozi watajaribu kutatua kero kuu za wanajimbo kutokana na mahitaji muhimu ya maisha yao na kuwa endeleza according to what they see fit within their boundaries of control.
 
Back
Top Bottom