NyaniMzee
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 396
- 727
Wapendwa wanajamii,
Mimi nimekuwa ni mteja wa CRDB Bank kwa miaka si chini ya 12. Mwanzoni nilijivunia kuwa mteja wa CRDB kwa jinsi walivyokuwa wakiboresha huduma kila mara. Lakini kwa sasa CRDB ni benki ya hovyo kuliko mfano. Usijaribu kuamini kuwa ATM zao zina fedha muda wote utaadhirika! Usijaribu kununua bidhaa kwa kutunia credit card zao utaumbuka.
Usiamini huduma yao ya "Simbanking" utaboreka maana kila mara wanarekebisha mitambo! Siku za weekend ndio balaa kabisa ATM zinaenda " kupumzika Coco beach " hadi weekend ipite hivyo usijisumbue kutafuta pesa Jumamosi au Jumapili. Cha ajabu CRDB ina wafanyakazi wengi tu ambao vitendea kazi vyao ni "Smartphones" na kila muda "wanazichungulia na kuzipangusa" zisichafuke. Shame on you CRDB! Nawapongeza NMB maana wameamua kuwapiku hawa wanaochezea biashara.
Huduma za NMB zinaridhisha ila labda kama wewe una kadi ya CRDB na unataka kuitumia katika ATM za NMB. Kitakachokupata ni kuambukizwa magonjwa ya CRDB ukiwa katika ATM ya NMB. Nimeamua nahama sitaki kuteswa na pesa zangu na nimechoka kuadhirika na kikadi kilichoandikwa CRDB Tembo card na nyingine ya ovyo kuliko wanaita Premium Gold Visa Card. Kazi kwenu mnaoipenda CRDB.
Mimi nimekuwa ni mteja wa CRDB Bank kwa miaka si chini ya 12. Mwanzoni nilijivunia kuwa mteja wa CRDB kwa jinsi walivyokuwa wakiboresha huduma kila mara. Lakini kwa sasa CRDB ni benki ya hovyo kuliko mfano. Usijaribu kuamini kuwa ATM zao zina fedha muda wote utaadhirika! Usijaribu kununua bidhaa kwa kutunia credit card zao utaumbuka.
Usiamini huduma yao ya "Simbanking" utaboreka maana kila mara wanarekebisha mitambo! Siku za weekend ndio balaa kabisa ATM zinaenda " kupumzika Coco beach " hadi weekend ipite hivyo usijisumbue kutafuta pesa Jumamosi au Jumapili. Cha ajabu CRDB ina wafanyakazi wengi tu ambao vitendea kazi vyao ni "Smartphones" na kila muda "wanazichungulia na kuzipangusa" zisichafuke. Shame on you CRDB! Nawapongeza NMB maana wameamua kuwapiku hawa wanaochezea biashara.
Huduma za NMB zinaridhisha ila labda kama wewe una kadi ya CRDB na unataka kuitumia katika ATM za NMB. Kitakachokupata ni kuambukizwa magonjwa ya CRDB ukiwa katika ATM ya NMB. Nimeamua nahama sitaki kuteswa na pesa zangu na nimechoka kuadhirika na kikadi kilichoandikwa CRDB Tembo card na nyingine ya ovyo kuliko wanaita Premium Gold Visa Card. Kazi kwenu mnaoipenda CRDB.