Bank teller alivyotapeliwa

Hii imetokea pia dodoma juzi Kati tu hapa. Mdada Kala hasara ya zaidi ya laki 6 kwa style hiyo. Matapeli sio watu wazuri
 
Stories ya kutunga haiwezekani. Yani upewe kibunda bila kuzifungua.
Otherwise tuambie ilitokea wapi?
Ilimtokea mfanyakazi wangu Mpesa. Kapewa laki sita, mara ghafla imegeuka laki moja. Buku mbili mbili tupu. Unapewa unahesabu, anaziomba ukimpa anarudisha sio zile za kwanza. Ukiwa mzembe imekula kwako
 
Hugo teller in mzembe , hela ikitoka dirishani hata km hazijafunguliwa ,ajirudisha tena lazima uhesabu......ajali kazini
 
Mingine inakuwa ni michongo wanafanya hao tellers...

Unapanga tu na mtu mchezo mzima, ushaidi utaonesha umetapeliwa kumbe ni sehemu ya igizo...
Utailipa tu,segerea inakusubiri
 
kwani siku hizi bank teller wanakaa ndani ya vioo vyenye tinted

visivyoonyesha hata mteja anachofanya nnje ya kioo?
Wale huwa wamejipanga mapema, hafanyii mchezo wake pale.

Zile halisi zinakuwa peke yake na fekelo peke yake.

Kitendo cha kumrejeshea, ndani ya sekunde tayari kamaliza kitendo cha ubazazi.

Ni vilevile kama wafanyavyo Kariakoo, unaoneshwa kitu halisi, kwenye kukabidhiwa ndo mchezo unapochezwa, ingawa hao lazima wawe wawili, lakini kwa teller mtu anaonekana kuanzia tumboni halafu anachofanya chini haukioni, hata wewe mkuu ungelizwa tu!

Dawa yake pale ni kuhakiki bila kuchoka, hapo tapeli yangelimfika ya shingo, utasikia linaanza kujitetea kijingajinga....'kaka nthamee'...!
 
Ilimtokea mfanyakazi wangu Mpesa. Kapewa laki sita, mara ghafla imegeuka laki moja. Buku mbili mbili tupu. Unapewa unahesabu, anaziomba ukimpa anarudisha sio zile za kwanza. Ukiwa mzembe imekula kwako
Hivi huyo mbwa ukimbainia kama hapo benki si atajidharau mwenyewe!
 
huyo teller ni mzembe kwa nini asingehesabu
Don't trust a customer yule teller ni mzembe, ile ni kazi yake alitakiwa ajiridhishe kwa kutumia mashine kujua kama zimetimia USD 10,000 na hapo hapo angegundua kuwa ni fake.Yeye kapokekea mzigo na kuuweka bila kuhakiki.Hili liwe funzo kwa ma-teller wengine.
 
Hawa mpaka siku waibiwe wao ndo wataelewa uwa watu wanaibiwa vipi
 
Kwa ujinga wake mwache atapeliwe ili wajinga na wazembe wazidi kupungua!!
 
Ilimtokea mfanyakazi wangu Mpesa. Kapewa laki sita, mara ghafla imegeuka laki moja. Buku mbili mbili tupu. Unapewa unahesabu, anaziomba ukimpa anarudisha sio zile za kwanza. Ukiwa mzembe imekula kwako
Kuna kua na mafungu mawili ya pesa! Fungu A linakua kamili na ndiyo unapewa ili uhakiki ukisha hakiki tu lazima afanye jambo lolote lile litakalo mfanya uumpe zile pesa tena na ukisha mpaa tu hapohapo anakwambia ok poa tufanye biashara na hapohapo ana kupa fungu B ambalo ndiyo kanjanja na ukiwa mvivu wa kuhakiki kwa mara ya pili ndiyo imekula kwako hiyo!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…