.inawezekana thread imesheheni facts za kutosha lakini, pengine kwa nia ovu ya kutaka kuunganisha uchafu huu na utawala wa JPM,
Sophist, sikutegemea uweke kipande hiki 'condensed' na kizito hivi na kuondoka moja kwa moja!
Mimi ninakubaliana nawe katika uandishi na mtiririko wa makala ile. Niliposoma kwa mara ya kwanza nilichanganyikiwa, ikiwa na pamoja na kutokuwa na 'background' nzuri ya eneo hili.
Nikapewa elimu kidogo na mkuu JMushi. Nikasoma tena makala hiyo kwa uangalifu zaidi. Hapo ndipo nilipogundua udhaifu wa uwasilishaji wa taarifa yenyewe, kutokana na mchanganyo wa kwenda mbele na kurudi nyuma kulivyofanywa na mwandishi.
Lakini mchanganyiko huo bado haukuondoa ukweli wa taarifa iliyowasilishwa, na ninashukuru kwamba nawe unakubaliana na hilo.
Sasa turudi kwenye hii "
nia ovu" unayoizungumzia wewe.
Katika kusoma makala ile sikuona JPM akitajwa moja kwa moja. Ila mimi nimeona CCM ndio inayotajwa. Kwa hiyo kwa kuwa JPM ni sehemu ya CCM, labda ndio tuseme uhusiano utakuwa ndio huo.
Sasa kama hivyo ndivyo, mimi sioni 'nia ovu' kwa JPM, bali kama 'nia ni ovu' itakuwa ni juu ya CCM aliyomo JPM. Ukiniambia kuisema CCM ni 'nia ovu', siwezi nikakuelewa kabisa, kwa sababu sioni tofauti yoyote kati ya CCM aliyomo JPM na CCM ya Mkapa au CCM ya Kikwete. Tunazidi kuona washiriki wa matukio mengi ni wale wale, na kama hawashiriki, kinga zao ndio zinazidi kuimarishwa! Wewe unatueleza, kuna 'nia ovu', kivipi?
Kama wewe unaziona tofauti hizo, labda utaziweka hapa mda ukikuruhusu.
Mengi sana yamekwishaandikwa ndani ya mjadala huu yanayoonyesha CCM ilikotufikisha; na wewe katika ufafanuzi wako mzuri katika kipande kile kifupi, umetufungua macho zaidi kuliko makala ile ilivyokuwa imetuwezesha.