Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Balozi Dkt. Abdallah Possi, amezitaka jumuiya za kimataifa kutumia njia za mashauriano yenye tijabadala ya kutoa hukumu zisizo na uwiano pindi wanapotathmini hali ya kisiasa na kiuchumi nchini.
Akihojiwa Agosti 19, 2026 kwenye kipindi cha Jana na Leo cha Wasafi Media, Balozi Posi amebainisha kuwa diplomasia ya kweli inapaswa kujengwa katika msingi wa mazungumzo yenye nia ya kujenga na sio kubomoa.
Akitolea mfano wa suala la haki za binadamu na uhuru wa kujieleza, Balozi Posi ameeleza kuwa uhuru wowote unapaswa kuendana na mipaka ya kisheria na usivunje amani au kuathiri haki za wengine.
"Ni kutotutendea haki kutotambua wapi tulipotoka na hatua tulizopiga mpaka sasa. Zamani ilikuwa kawaida kuona watoto wanakwenda shule bila viatu, lakini leo hii miundombinu na huduma zimeboreshwa kwa kiasi kikubwa. Kuna maendeleo ya wazi ambayo hayapaswi kupuuzwa,"
Akihojiwa Agosti 19, 2026 kwenye kipindi cha Jana na Leo cha Wasafi Media, Balozi Posi amebainisha kuwa diplomasia ya kweli inapaswa kujengwa katika msingi wa mazungumzo yenye nia ya kujenga na sio kubomoa.
Akitolea mfano wa suala la haki za binadamu na uhuru wa kujieleza, Balozi Posi ameeleza kuwa uhuru wowote unapaswa kuendana na mipaka ya kisheria na usivunje amani au kuathiri haki za wengine.
Balozi Possi amesema washirika wa kimataifa kushirikiana na Tanzania kwa uwazi, kusikiliza mazingira ya ndani ya nchi, na kutoa tathmini zenye haki badala ya kulinganisha mazingira ya Tanzania na nchi zilizoendelea sana bila kujali muktadha wa maendeleo."Ni kutotutendea haki kutotambua wapi tulipotoka na hatua tulizopiga mpaka sasa. Zamani ilikuwa kawaida kuona watoto wanakwenda shule bila viatu, lakini leo hii miundombinu na huduma zimeboreshwa kwa kiasi kikubwa. Kuna maendeleo ya wazi ambayo hayapaswi kupuuzwa,"