Balozi Mahiga: Tanzania inaangalia namna ya kuipatanisha Sudan ya Kusini

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,253
Waziri-Mahiga.jpg

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa Balozi Augustine Mahiga amesema Tanzania na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wanaangalia namna ya kuisaidia Sudani ya Kusini katika kuleta upatanishi ili kusitisha mapigano yanayoendelea nchini humo kwa sasa.

Dkt. Mahiga ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam katika mahojiano maalum na ITV ambapo amesema baada ya mkutano wa SADC uliofanyika hivi karibuni Addis Ababa walitegemea utekelezaji wa makubaliano yaliyoafikiwa uanze.

Aidha Balozi Mahiga amesema juhudi za kuwapatanisha Rais wa Sudani ya Kusini Silva Kiir na makamu wake Bw.Riek Machar zilichukuwa zaidi ya mwaka mmoja na kwamba kuingia kwao kwenye jumuiya ya Afrika Mashariki kutachangia kuharakisha mapatano.

Zaidi ya watu 200 wameuawa katika mapigano yaliyoanza alhamisi iliyopita kati ya majeshi yanayowatii viongozi hasimu Rais Salva Kiir na makamu wake Bw Riek Machar.

Wakati huo huo Balozi Mahiga amepokea msaada wa Madawati kutoka jumuiya ya Maboora ambapo amesema utekelezaji wa elimu bure umeanza na changamoto nyingi ikiwemo ya madawati.


Chanzo: ITV

======

Kwa upande wangu naipongeza sana serikali kwa hatua hii kwani Tanzania tumekuwa kisiwa cha amani na utamaduni wetu ni kusaidia nchi nyingine toka uhuru.
 
South Sudan wasipokuwa na nia ya dhati wao wenyewe waishi peacefully hakuna ataweza wapatanisha. Hawa watu wanaendekeza sana ukabila, macho yao yamepofushwa hawaoni wanapoenda. Kila mtu anawaza power amtawale mwenzake....hatari.
 
Sehemu ya utatuzi wa mgogoro wa Sudan iwe ni kutoa elimu ya uongozi na diplomasia kwa Kiir na Machar , na pia kuwapa Mtaalamu wa uongozi aka wasaidia na mambo ya uongozi na conflict resolution
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa Balozi Augustine Mahiga amesema Tanzania na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wanaangalia namna ya kuisaidia Sudani ya Kusini katika kuleta upatanishi ili kusitisha mapigano yanayoendelea nchini humo kwa sasa.

Dkt. Mahiga ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam katika mahojiano maalum na ITV ambapo amesema baada ya mkutano wa SADC uliofanyika hivi karibuni Addis Ababa walitegemea utekelezaji wa makubaliano yaliyoafikiwa uanze.

Aidha Balozi Mahiga amesema juhudi za kuwapatanisha Rais wa Sudani ya Kusini Silva Kiir na makamu wake Bw.Riek Machar zilichukuwa zaidi ya mwaka mmoja na kwamba kuingia kwao kwenye jumuiya ya Afrika Mashariki kutachangia kuharakisha mapatano.

Zaidi ya watu 200 wameuawa katika mapigano yaliyoanza alhamisi iliyopita kati ya majeshi yanayowatii viongozi hasimu Rais Salva Kiir na makamu wake Bw Riek Machar.

Wakati huo huo Balozi Mahiga amepokea msaada wa Madawati kutoka jumuiya ya Maboora ambapo amesema utekelezaji wa elimu bure umeanza na changamoto nyingi ikiwemo ya madawati.


Chanzo: ITV

======

Kwa upande wangu naipongeza sana serikali kwa hatua hii kwani Tanzania tumekuwa kisiwa cha amani na utamaduni wetu ni kusaidia nchi nyingine toka uhuru.
Kama ni kisiwa cha amani mbona mmeshindwa kuwapatanisha wazanzibar ?
 
Mimi sio shida tukiwasaidia hao South Sudan kwani ni nia yetu na jumuia za kimataifa hua zinatuomba tufanye hivyo. Na sisi kwa Suala yetu mataifa ya nje yenye capacity na uweledi waje ku solve yetu, kumbuka mganga haji tibu au kinyozi hajinyoi
 
Back
Top Bottom