GE2025 Balozi Ali karume amvaa Humphrey Polepole

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Bagamoyo

Platinum Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
29,869
Reaction score
34,025
Balozi Ali Karume amkosoa vikali Humphrey Polepole

View: https://m.youtube.com/watch?v=sN6hZvI5faYMheshimiwa Polepole ni mwanasiasa shughuli ya ubalozi hakuwa anaufahamu kuielewa wala hakutaka kujifunza ndo maana tunaona haya yaliyotokea, balozi Karume anapigilia msumari harakati za Polepole


Ali Karume aliyewahi kutumikia wadhifa wa kidiplomasia kama balozi kwa miaka 27 amesema Humphrey Polepole mazungumzo yake amekiuka imani aliyopewa na mteuliwa wake balozi namba moja aliye rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Balozi Ali Karume anafafanua balozi kamili wa ukweli ni wale walioanza kazi katika wizara ya mambo ya nje na kufikia ngazi ya minister plenipotentiary grade one katika mafaili yao ya utumishi ndani ya wizara kabla ya kupewa ubalozi, tofauti na kina Polepole wanaopachikwa juu kwa juu kuwa mabalozi wasio na uzoefu wizarani

Balozi Ali Karume anaongeza kuwa tuchukulie mfaño mahusiano mema na ya aina ya kipekee katika ya Cuba na Tanzania, hivi kweli balozi wa Cuba nchini Tanzania angeweza kujiuzulu na kuanza kuishambulia nchi yake ya Cuba ?

Balozi Ali Karume amesema yu tayari kuanzisha mazungumzo na Humphrey Polepole katika jukwaa lolote liwe katika televisheni, ZOOM, YouTube ili kuongelea masuala mbalimbali wabadilishane mawazo

Balozi Ali Karume anasema hali hii ya Polepole kuanza mazungumzo yake ipo haya mamlaka za uteuzi za nani anakuwa balozi wetu nje kuwa na njia bora zaidi za kuchuja nani anafaa kuwa balozi ili taifa liepukane na aina ya mheshimiwa Humphrey Polepole kupenya na kuwa balozi isitokee.
 
Another idiot!
 
BALOZI ALI KARUME WASIFU WAKE
Kama minister plenipotentiary grade one pale wizarani foreign affairs tofauti na wanaotunukiwa juu kwa juu

View: https://m.youtube.com/watch?v=kODF2obk-3QUTUMISHI KAMA BALOZI MIAKA 27: marais 4 wa Jamhuri ya Muungano walimteua kuwa balozi :

Mwaka 1984, Karume alihitimu kutoka Chuo Kikuu cha Columbia, USA kisha akaingia katika utumishi wa serikali.

Mwaka mmoja baada ya kuhitimu masomo yake, Karume alijiunga na Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania na kuanza utumishi wake kwa miaka minane katika ubalozi huko Brussels, Ubelgiji (1985-1989) halafu kama Naibu Balozi huko Washington, D.C., Marekani (1989– 1993).

Alirudi Tanzania na kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa jijini Dar es Salaam, Tanzania kuanzia mwaka 1993 hadi 1996.

Baadaye aliteuliwa na Rais Benjamin William Mkapa kuwa balozi wa Tanzania huko Ubelgiji, Uholanzi na Luxemburg (Benelux) na Umoja wa Ulaya (EU) ambako alihudumu kuanzia 1996 hadi 2002.

Baadaye, hadi mwaka 2006, Karume alihudumu kama balozi nchini Ujerumani, Uswizi na Polandi na kuwakilisha Tanzania wakati huohuo pia huko Vatikani, Austria, Jamhuri ya Ucheki, Slovakia, Hungary, Romania na Bulgaria.

Kwenye Julai 2006 Karume aliteuliwa na Rais Kikwete kuwa Balozi nchi za Italia, Uturuki, Ugiriki, Slovenia, Kupro na Malta.

Mwaka 2015 alirudi Tanzania
 
Mhuni mwenzao...

Mheshimiwa Polepole afanye namna siku ya mazungumzo yake balozi Ali Karume naye awemo ili hizi teuzi za kina IGP Simon Sirro n.k ambao hawakuwa wamefikia ngazi ya juu ya minister plenipontentiary gradi ONE ndani ya wizara ya mambo ya nje kwanini hawafai kutunikiwa ubalozi kama hisani huku nchi itaumia kimahusiano ndiyo maana Ezekiel Kamwaga hadi leo hajapata jibu la balozi wa Cuba nchini Tanzania kama mtungi wa gesj Cuba ni Tshs ngapi

TOKA MAKTABA :
01 September 2025

EZEKIEL KAMWAGA ADAI KUTINGA UBALOZI WA CUBA KUPATA BEI ELEKEZI YA GESI NCHINI CUBA

View: https://m.youtube.com/watch?v=y4VZHopbaSAPengine balozi wa Cuba nchini Tanzania hakumpokea Charles Kamwaga kutokana na anayosema balozi Ali Karume kuwa balozi hatakiwi kuvuruga mahusiano.
 
Polepole hashambulii nchi anashambulia mafisadi. Wajibu hoja zake

Na ndugu Polepole alijiuzulu ili aongee bila kubanwa na nyadhifa ya ubalozi ili awe huru kufanya mazungumzo juu ya wahuni, hili wanamtandao na wahuni bado wanadhani Humphrey Polepole ni balozi.

Pia mheshimiwa Rais Samia Hassan aliye balozi namba moja *(maneno ya Prof. Kabudi kuwa rais ni balozi namba moja) alichukua hatua na alimvua wadhifa wa ubalozi Polepole ili isionekane anavuruga mahusiano ya kipekee ya kihistoria ya baina ya nchi ya Cuba na Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…