JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Kikao cha Maafisa Waandamizi wa SADC ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Biashara za Kimataifa wa Zimbabwe, Balozi Albert Chimbindi alipokuwa anasoma hotuba ya ufunguzi ya kikao hicho jijini Antananarivo Agosti 06, 2025.
Balozi Chimbindi alisema katika kipindi cha uenyekiti wake, mtangamano wa SADC umeendelea kuimarika na mafanikio makubwa yamepatikana katika nyanja za ulinzi na usalama, utawala bora, maendeleo ya rasilimali watu, viwanda na huduma za jamii.
Alisema licha ya Kanda ya SADC kukumbwa na changamoto mbalimbali kama vile, ugonjwa wa UVIKO-19, ukame, maradhi, mabadiliko ya siasa za kimataifa na mabadiliko ya tabianchi, bado eneo hilo limeendelea kuwa imara kiuchumi.
Ametoa wito kwa nchi wanachama kuongeza jitihada za pamoja kujenga miundombinu ya barabara, reli, nishati na maji ili kuchochea shughuli za kiuchumi na biashara katika kanda.
kwa ajili ya kukuza uchumi na kuondoa tatizo la ajira kwa vijana", Balozi Chimbindi
alisema.
Kikao cha maafisa waandamizi ni moja ya vikao vya utangulizi kuelekea Kikao cha Baraza la Mawaziri Agosti 12 na baadaye Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliopangwa kufanyika Agosti,17, 2025.