BAKWATA na Mauaji Arusha

MOU bado upo mkuu.Na kwasasa wa2 wamesahau2.Je,wajua yaliyomo ndani ya MOU?

Kwa hiyo kama unakiri kuna MoU kati ya Church na Gvt, then motive ya tamko la maaskofu sio udini bali ni moral obligation, kitu ambacho BAKWATA wanakosa kwa sababu kila mara wanakuwa biased kidini.
 

Mimi pia siafiki kuwalazimisha kutoa tamko BAKWATA kwa vile tu Maaskofu wa Arusha wametoa tamko. Tena hata Maaskofu waliotoa tamko siyo maaskofu wote, ni wa Arusha tu, wa mikoa mingine yote hawajasema kitu. Nina imani kuwa hizi taasisi za dini zinaongozwa na kanuni zao, tusiwalazimishe. Hao mnaofikiria kuwa hawajafanya kitu, wakati fulani ndiyo huwa na msaada mkubwa katika kutumika kama watu wa kati kwa vile hawajaonesha kuegemea upande wowote.

Kama alivyosema Tunalazimika, tukiendekeza sana mijadala ya namna hii tutawakwaza baadhi ya watu wenye mapenzi mema na CHADEMA na nchi hii. Anayeleta hisia za kidini kwa mambo yanayohusiana na CHADEMA asifikirie anaisaidia CHADEMA. Mimi najua CHADEMA haipo kwaajili ya dini fulani, inahitaji kuungwa mkono na watanzania wote. Katika nchi hii hakuna chama chochote kinachoweza kuongoza kwa kutegemea watu wa dini moja au kabila moja. Katika watanzania wale wawili waliouwawa na polisi kule Arusha, mmoja alikuwa mkristo na mmoja alikuwa muislam, huyo mtu anayedharau dini nyingine ujasiri huo anaupata wapi? Anaweza kujilinganisha na huyo mkristo au muislam aliyekufa katika kutetea haki za wananchi wa Taifa hili?

Kama ningekuwa na uwezo, hoja zote zinazoendekeza udini ningekuwa naziondoa kabla ya kuanza kujadiliwa, pamoja na kuwafungia wanaozileta.
 

Kama chadema hawatowaangalia watu wa namna hii na kuwa rub-out uanachama, changes haitatokea na kama itatokea haitadumu. Kwa ufupi mnawakatisha tamaa jamii ya waislam! Mwishowe kila muislam itabidi awe kama Malaria sugu,Dar es salaam, topical etc. Rethinking the changes we desire bro!
 

u are right 100%. Udini unaoonyeshwa humu na wanachadema unatishia mustakabali wa nchi hii. Yaan ukiwa humu, kama wewe ni Muslim, utajikuta tu unaona bora CCM. Mkuu watu wa humu hawawez kuacha, kwan ni watu wazima+elimu, sio watoto hivyo huwez kuwabadilisha mtazamo, labda kama wataamua kuact.
Mimi sikuwahi kuwa mdini, ila humu kumenipa hasira sana... I will never choose Chadema.

Utawaona hapa watavyonishambulia.
 

Asante sana umenisaidia kusema tunawajua Chadema na ajenda ya Kanisa Katoliki ni kuona anakaa katika kiti cha urais mkristo ila hawatudanganyi tutabanana hapa hapa. Wanaotaka tamko la Bakwata hawajatosheka tu na tamko la paroko wao tu wa Kanisa Katoliki Arusha. Sasa mnatufata nini waislamu kutoa Tamko? Niwaulize Kanisa Katoliki lilitoa tamko pale MWEMBECHAI!!!!!
 

Hatukushambulii kalamuzuvendi, tunakupenda tu.
 
BAKWATA wana hiari ya kutoa tamko.
 

Mkuu hawa jamaa wameshameza maji ya bendera ya Chadema na Kanisa na ndio maana mie sijajunga chadema wala sina chama maana sikubaliani na baadhi ya mambo ya baadhi ya vyama vya siasa. Ila kukashifu dini ya mwenzio ni jambo baya sana. Huna haja ya kukasirika ndugu wakipiga msumari na wewe unatafuta msumari unashindilia basi ndio tunaenda hivyo utaumia bure kumkasirikia mtu usiyemuona.
 
Kweli unyonge wa fikra ni tatizo kubwa sana! Yaani kuna watu bado mnaogopa kuumeza ukweli kisa umetokea upande wa dini fulani??? Mbona kuna viongozi wakubwa wa waislam, MZEE RUKSA akiwa mojawapo, wamewahi kutamka hadharani kwamba waislam tujikomboe ktk elimu na akasema wakristo wamewekeza huko, kuna aliyenyanyuka hapa kupinga au kukosoa?? Tuache unyonge na ubutu wa fikra...
 
Shame ou you too kwa kusema maaskofu wana ubia na Cdm. Tena ulaaniwe km hao polic wali2mwa kuwaua raia wasio na hatia. Shame on you tn na tn!
Mwehu kilakitu huzungumza na hawezi kukaa kimya.Maaskofu si wanaubia na cdm ndo maana hawishi maneno.Wakati huohuo mnasisitiza tusichanganye dini na siasa.Hapa mtoa hoja hana jipya zaidi ya kuleta mpasuko wa kidini.SHAME ON YOU.
 
Jamani naombeni tusiwe kama bendera... Tusisahau issue sio bakwata bali ni matendo ya polisi na serikali kutumia risasi za moto dhidi ya wananchi wasio na silaha..use of excessive force...and not religion...
 

Hukukipenda toka mwanzo. Na hautashambuliwa kwa sababu ni muislamu, utashambuliwa kwa kutoa hoja dhaifu. Kama haja yako ni kwenda mahali ambapo waislamu hawashambuliwi, hapa si pako. Kila mtu anashambuliwa bila kujali dini yao.

Amandla....
 

Hivi vi boy boy viko vingi humu .. Someting like charityboy.. cityboy.. Why insisting that you are a boy?
 
Jibu la hii kitu ni rahisi. Bakwata hawajatoa tamko la kulaani. Je ni lazima watoe tamko? Si lazima. Jee ingependeza wangetoa tamko. Naam, ingependeza lakini si lazima maana kuna waislamu wengi ambao wamelaani kitendo hicho. Hao ni muhimu zaidi kuliko Bakwata. Kama ambavyo wakristu wengi walilaani mauaji ya Mwembechai bila kusubiri tamko la Maaskofu wao. Tatizo liko wapi?

Amandla.......
 

Mdau sio unyonge wa kifikra ila tu waislamu wa sasa sio wajinga kama wale wazamani hatufuati mkumbo kama walivyokuwa wazee wetu sasa hivi tunataka umakini wa jambo. Kama kanisa katoliki lilitaka ushirikiano kutoka kwa waislamu lingelianza kwanza kwa kuwaomba waislamu radhi kwa kutokemea mauaji ya mwembechai ndipo likalaani hayo ya arusha. But venginevyo ni UNAFIKI TU HUO NA HAKUNA MTU ATAKUUNGENI MKONO!!!!!
 
Hivi vi boy boy viko vingi humu .. Someting like charityboy.. cityboy.. Why insisting that you are a boy?

...kama nakuelewa vile?? You never know hawa city,charity,etc ni kina nani, wengine ni high placed individuals*...it is important to remember that there are certain unnatural homohabilis activities which render a male human being incompetent to act under self-control due to enforced back-influence of another male being....(intentional grammar/syntaxical disarrangement??? never mind...)
 

Kwa hiyo haulaani mauaji ya Arusha kwa vile tu wakatoliki wamelaani? Halafu unajigamba kuwa haufuati mkumbo!

Amandla.....
 


There you are>>>>> changamsha ubongo ndugu, MWEMBECHAI hayakua maandamano ya waTanzania wapenda mabadiliko chanya kisiasa, ilikua ni suala la imani, katiba ya nchi iliyopo haitambui mambo ya Uislam wala Ukristo, inatambua kila mtu kwa imani yake...zaidi, kama Wakristo hawakutoa tamko kuhusu MWEMBECHAI wakati damu ya waTanzania ilimwagika, SHAME on them!!! Kosa na upumbavu wao isiwe sababu ya BAKWATA kunyamaza, kwanza CDM sio wakristo, ni Watanzania bila kujali imani....BAKWATA-Arusha wakinyamaza katika hili, na Wakristo wenye akili finyu wataanza kusema Serikali iliyopo ni ya Kiislam, tunaelekea wapi sasa?? Acha mawazo mgando, think BIG!!!
 

Usidharau Waislam pia,unaweza kutuambia tofauti ya Waislam wa sasa na wa Zamani??? Ujinga wa zamani ni upi na Ujanja wa sasa ni upi?? Nitajie wazee waliofuata mkumbo zamani...Acha kuandika utumbo...
 

You are right man.I kind like find common character with these type of dudes(not sure all them are males though). Its all about complaining and whining all the time hiding behind the religion issues.. Umasikini wa mtanzania hautaondolewa na kwa kulia-lia na kulaumiana hasa kwa kutumia kivuli cha dini.Adui yetu ni ufisadi,ujinga,maradhi na umasikini.Anayesababisha na kushindwa kutukwamua katika hayo wote mnamjua. Ni CCM.So quit whining here like ......es!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…