BAKWATA iliundwa na nani?

zubedayo_mchuzi

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2011
Posts
4,873
Reaction score
1,219
Habari zenu Wana JF,
1763032085755.png

Leo tujikite kwenye swala hili ambalo kimsingi ndio chimbuko la mgawanyiko wa maslahi ya watu fulani fulani. Nimekuwa nikipitia pitia vyanzo vingi ili kujua ni nani walioanzisha BAKWATA ambayo mpaka muda huu imekuwa ikilalamikiwa na Waislamu wengi kuwa ipo chini ya Serikali na inafata Masharti ya Serikali.

Katika Mahubiri ya Sheikh Ilunga kati ya moja ya DvD zake ameeleza bila woga kabisa kuwa BAKWATA iliundwa 1968 mjini Iringa, kwenye Ukumbi wa Sapuna Cinema Iringa na Usalama wa Taifa waliopata mafunzo MOSADI, Israeli.

Mwaka huo Mwl. Julius Nyerere ndiey aliyeagiza kuvunjwa kwa East African Muslim Welfare na kuwakusanya Usalama wa Taifa na kuwapeleka Iringa kuunda BAKWATA wakiongozwa na shushushu Rashidi Kayugwa pamoja na wenzake. Kwa maana hiyo BAKWATA haikuundwa na Waislamu wenyewe bali Iliundwa na Usalama wa Taifa Waislamu!

Hao ndio walikuwa waislamu wa kwanza kipindi cha Nyerere ambao aliwateua na kuwapeleka Israel kusomea ushushushu na ndio waliouunda BAKWATA.

BAKWATA ni ya nani?


Kimsingi hapa ndio chimbuko la matatizo yote ya BAKWATA na Waislamu.

Pia soma:
~ Ninachofahamu kuhusu BAKWATA
~ BAKWATA ni mwakilishi halali wa Waislam wote?
~ Maswali 11 yenye utata: BAKWATA ilianzishwa na nani?
 
Mbona Dr Ilunga Hassan Kapungu alishaongea ukweli wote,hiyo ilikuwa ni kazi ya mikono ya Nyerere ili kuwadhibiti waislam.Sasa hivi imeonekana waislam wa leo sio wale wa jana speed 240 hawadhibitiki.
 
Baraza Kuu la Waisilamu Tanzania (BAKWATA) ni Baraza/Taasisi Inayotambulika Kisheria Tanzania ambalo paoja na mambo mengine ina kazi ya kusimamia/kuratibu shughuli zote za Taasisi za Kiisilamu nchini!
 
Mbona Dr Ilunga Hassan Kapungu alishaongea ukweli wote,hiyo ilikuwa ni kazi ya mikono ya Nyerere ili kuwadhibiti waislam.Sasa hivi imeonekana waislam wa leo sio wale wa jana speed 240 hawadhibitiki.

Mkuu Zantsan:Kila kipindi kina mambo yake na udhaifu,udhaifu huo usitumike dhana hizi makosa ya kipindi hicho yarekebishe ili watu wawe na imani na vyombo vyao..
 
Baraza Kuu la Waisilamu Tanzania (BAKWATA) ni Baraza/Taasisi Inayotambulika Kisheria Tanzania ambalo paoja na mambo mengine ina kazi ya kusimamia/kuratibu shughuli zote za Taasisi za Kiisilamu nchini!

je hilo ndio lilikuwa dhumuni la BAKWATA???? kama ni kweli kwanini limekuwa liki lalamikiwa kila kona na waislamu wengi watoto kwa wakubwa??
 
Mi nafikiri umefikia wakati kwa hili baraza (BAKWATA) kuvunjwa na kuachiwa Waislam wenyewe kuunda Upya baraza lao wanalolitaka wao wenyewe kwasababu hakuna mantiki kundi fulani kuundiwa chombo cha kuwaendesha na watu wengine hivi tujiulize wameanzishiwa hicho chombo kwa malengo gani??
 
Mi nadhani hilo halikuwa lengo la waislam wenyewe kwa sababu kama waislam wenyewe kwa wakati ule wangeona kama kuna haja ya kuwa na chombo kama BAKWATA wangeiomba Serikali kuwafanyia hivyo lakin SERIKALI kwa wakati ule kwa utashi wake na kwa malengo yake ambayo impact yake tunaiona hivi sasa ndio ilijiundia yenyewe kwa lengo linalolijua yeye lenyewe sio Waislam,
waislam tulio wengi tunaiona na tunaamini BAKWATA si kwa malengo ya maslahi yao wao kama Waislam bali maslahi ya walioianzisha na kwa malengo yao
 
Habari zenu Wana JF.

BAKWATA NI YA NANI- SEHEMU YA KWANZA
Leo tujikite kwenye swala hili ambalo kimsingi ndio chimbuko la mgawanyiko wa maslahi ya watu fulani fulani.Nimekuwa nikipitia pitia vyanzo vingi ili kujua NI NANI WALIOANZISHA BAKWATA ambayo mpaka muda huu imekuwa ikilalamikiwa na WAISLAMU wengi kuwa ipo chini ya SERIKALI na inafata MASHARTI YA SERIKALI.

Katika Mahubiri ya SHEIKH ilunga kati ya moja ya dvd zake ameeleza bila woga kabisa kuwa BAKWATA iliundwa 1968 mjini IRINGA,kwenye UKUMBI WA SAPUNA CINEMA IRINGA na USALAMA WA TAIFA waliopata mafunzo MOSADI israeli.

Mwaka huo MWL.JULIUS NYERERE ndie alie agiza kuvunjwa kwa EAST AFRICAN MUSLIMS WELFARE na kuwakusanya USALAMA WA TAIFA na kuwapeleka IRINGA kuunda BAKWATA wakiongozwa na SHUSHU RASHIDI KAYUGWA pamoja na wenzake.Kwa maana hiyo BAKWATA haikuundwa na WAISLAMU wenyewe bali Iliundwa na USALAMA WA TAIFA WAISLAMU.

Hao ndio walokuwa waislamu kwanza kipindi cha nyerere ambao aliwateua na kuwapeleka ISRAELI kusomea ushushu na ndio waliouunda BAKWATA.

....BAKWATA NI YA NANI.........???????


Kimsingi hapa ndio chimbuko la matatizo yote ya BAKWATA NA WAISLAMU.

ANGALIZO;mods sitapenda lughs za kejeli,matusi na kukoseana heshima katika kujadiri hili na niombe atakae kiuka adhibitiwe mara moja,kila mchangiaji ajenge hoja nini ajuacho kuhusu BAKWATA na si vinginevyo.
Sasa kama kuna Usalama wa Taifa Waislamu na wakaunda BAKWATA ni kwa nini leo mnasema kuna mfumo Kristo???
Hii inaonyesha kuwa wapo watu ndani ya Usalama wa Taifa wana tetea dini ya Uislamu!!!!
Illunga ametoweka na ponda yupo njiani ....
 
Hebu Rudovic utoo pitia bakwata halafu tuletee taarifa yao ya mapato na matumizi
 
Sasa kama kuna Usalama wa Taifa Waislamu na wakaunda BAKWATA ni kwa nini leo mnasema kuna mfumo Kristo???
Hii inaonyesha kuwa wapo watu ndani ya Usalama wa Taifa wana tetea dini ya Uislamu!!!!
Illunga ametoweka na ponda yupo njiani ....

embu kuwa mwelewa kidogo hapo juu sijaandika chochote kuhusu mfumo kristo wala dini yoyote nimejadili kwa kifupi sana kuhusu uundwaji wa bakwata tu..kama hauna cha kukoment unakaa kimya tu..
 
BAKWATA ni kwa manufaa ya waislamu kwa sababu kwenye kuundwa waislamu walihusika huyo RASHIDI KAYUNGWA hakuwa mwislamu?
 
Kwa hiyo BAKWATA iliundwa na waislam wenye tamaa baada ya kushawishiwa refer RASHID Kayungwa!
Kwanini hawakukataa wakati huo au kuboresha mambo wakati wa utendaji.
Tatizo ninaloliona kwetu ni ile kupenda mambo yetu tufanyiwe na serikali. Mbona wenzetu wanakuwa na vyombo vyao nje ya serikali na vinaheshimika na vinafanya kazi. Toka awali sikuona mantiki ya kutaka mahakama za kadhi ziwekwe kwenye katiba. Tunaouwezo wa kuwa na vyombo vyetu vyenye kutoa maamuzi kama tukiamua na kujipanga vizuri. Vinginevyo tutaendelea kulalamika kama hili la BAKWATA. Nataka solution ya hili na si kulalamika. Je tumejipanga vizuri kuwa na chombo chetu kinachotuunganisha wote? Je tutaridhika au baadaye tutakuja nasababu zingine.
 
BAKWATA ni kwa manufaa ya waislamu kwa sababu kwenye kuundwa waislamu walihusika huyo RASHIDI KAYUNGWA hakuwa mwislamu?

Umeelewa swali??!! Hapa hatuzungumzii manufaa, tunazungumzia nani aliunda upo?
 
Back
Top Bottom