Bakhressa na Boats za Dar -Zanzibar

Bakhressa na Boats za Dar -Zanzibar

Na Subirini,kuna issue ilisita kwanza.
Ingebutuka ile watu mgesikia habari.
Alitaka kuleta Mabasi mapya 200 Luxury Coaches kwa safari za masafa marefu.Hapo ndio mtajua balaa la huyu mtu.

Watu walee utawajua tu,ndio haooo hawataki tu kujitambulisha.Aliepewa kapewa tu.

Hoja nyingine hazina hata mashiko,wenzio mbona waliowahi walipata tickets.Abiria wengine nyie watata kweli.
Mmeletewa train mpya mmeharibu,kwenye boat mnataka pia mpange mnavyotaka nyie

Angalizo:Wale washamba msiwe mnakuja Zanzibar,mnatutia aibu.Maana wengine mnauziwa tickect na mateja kwa kitambulisho cha Jina la kike,sasa laana zake ndio hizi za kubwatuka hovyo kwa kuvalishwa Gagulo.
Na kama umenunua Ticket kwa kulangua na lazima jina linakuwa sio lako basi umefanya kosa la jinai.Tutawatafuta
Cc.Kamanda Kova
 
Mzee wa Spice kule kwenye marashi ya karafuu punguza jazba kwenye haya mambo madogomadogo tu ya michango na ukataka kumkufuru Mungu kwa hili, hapa kila mmoja anatoa mchango wake kama yamemkuta au ni uwono tuu.

Ninasafiri sana na nimeanza mda mrefu sasa hivi kupakia kizigo kidogo sana hata cha kilo10 kwenye hizi boti ni bora ukapakie kwenye ndege ukweli ndio huo.

Na huyu Bahresa fitna za biashara amezitumia kuwazamisha wenzake hata kama ni kweli kuwa vyombo vyake vipya ila na vikongwe vitupwe? hujawahi kuziona boti zilizotembea miaka 100 kwenye bahari?

Huyu sio Tajiri ni mnafiki upande mmoja na ninakwambia tena huyu jamaa mpaka leo bado hajatoka kimaisha
.

Hahaha Mgeni mie nimeipenda hiyo hapo juu.
Sina Jazba mkuu ila tatizo ni kwamba hoja haina mashiko,na lengo lake linajulikana.
Wewe kama unapesa lete boat nzuri uone kama hupati wateja.Washindani wake wananunua boat kisha wanazipaka rangi mombasa halafu wanatuzuga mwisho wa siku boat inavuma kama dege la jeshi.

Hii biashara ni huru,au ndio mmezoea ile mishipa iliyouwa watu tele hapa.We mtu aliltea boat ile ye Seagul inachukua abiria mamia ya watu lakini kumbe System yake yoote imeandikwa lugha ya kikwao huko wala sio Kiingereza.Mambo ya used hayo.
Ufupi sijaona mshindani wake,na hao washindani wake ndio wanaopiga kelele hizi.Ila upande wa pili tuangalie ubora wake.Sasa unaposema fitna ni sawa na wale waliosema kwamba Diamond muda sio mrefu atashuka kiwango,wakati ndio kwaaanza kasi inazidi kupanda.Ubora ni ubora tu kamanda.Sio kukurupuka kwenye mipango,watu wanatulia kwenye kuwekeza a kujituma.
 
Kwani SUMATRA wanafanya kazi gani au ndio wanakula kodi yetu .Tatizo la kampuni ya Bakhresa ni CC yao nimbovu sana kila sehemu hata huko Azamtv ni vivyo hivyo,sijui sababu ya kuzoea kuuza juisi sielewi ,huduma kwa wateja kwao ni kama maji na mafuta,nadhani wanjiona wao washakuwa brand kwa hiyo hawahitaji kumhudumia mteja bali mteja ndie awahudumie wao,wameshajisahau tayari.
 
Kwa swala la ulanguzi wa ticket kweli ni tatizo haswa kipindi cha sikukuu au wikiend,kwa ushauri tu jitahidi kuwahi kukata ticket pale kituoni kwao mapema au ikiwezekana hata siku moja kabla ya safari utapunguza usumbufu,na kwenye swala la mizigo hapo sasa inabidi tusaidiane kuripoti tu maana kweli yule jamaa anaetoza pesa kwa mizigo tena kwa kuikadiria huwa ananyanyasa watu
 
Kama umetumwa Basi ushindwe na utepete.

Ningeomba tu kwamba watu wasifikirie Boat hizi ni kama zile Bus za Ubungo unakata ticket hata ukifika pale Terminal.
Zanzibar ipo vizuri kwenye utalii na pia usafiri wa boat ni watu wengi kuliko Ndege.
Sasa kila siku inashauriwa ukate Ticket mapema,sasa wewe ukitegemea kuenda kukata Tickect muda wa kuondoka unategemea nini?Na tena unabahati sana kuna watu pale nje wanauziwa tickets fake kila siku.

Mie mwenye nikitaka kusafiri kama ni weekend basi nataka siku moja kabla,kuepuka usumbufu.
Na wale wanaonunu ticket kwa kulangua hiyo sio kazi ya Kampuni hata hapo Dar kwenye Train walikuwa wanafanya hivyo kwa wale wazembe.
Miaka yote nipo Zanzibar sijawahi kukata ticket kwa kulangua kwakuwa najua wasafiri ni wengi hasa kwa boats muda fulani na siku fulani.
Kuhusu Uelewa wa Usafiri:-
Hembu uliza Kampuni ya Ndege unayosema juu ya kusafirisha hiyo Oven uone bei zao na Terms zao ni balaa.Lazima ujue namna ya kutofautisha aina ya mizigo.Ulipwaji huo ni wa kawaida na wote tunalipa kwenye baadhi ya bidhaa.
Halafu pia unaweze ku Book Tickect online bila tatizo.Sasa sioni unacholalamikia nini.

Kampuni hiyo kwa taarifa yako imejipanga vizuri kwa abiria wake,na huduma zote kwa ujumla.Na Kauli umeotoa kwamba umeambiwa sio lazima utumie boat hizo ni Uongo na utakuwa umevamia wale mateja pale mlangoni ndio wakakuzingua ili utumie Boat nyingine au wakubane.
Sasa inawezekana kwenye kusafiri na Fastjet ukafanya vituko zaidi ya hivyo.Kuna siku unaweza kusafiri Na Bata au kuku ukasema anauzito wa Handbag ili usilipe wakati kuna utaratibu wa namna ya kusafirisha.

Unavyoipeleka fikra yako basi siku zote itakukaririsha jambo au mtizamo huohuo.
Tubadilike,dunia inaenda kwa kasi sana kuliko wengi tunavyofikiria

Ndugu Zanzibar Spices nashukuru kwamba umekiri kwamba huo ulanguzi wa tiketi upo Zanzibar na hasa unapotaka kukata tiketi kwa siku hiyo hiyo ya safari. Hili ndilo tatizo tunalolisema kwenye hii mada. Hebu jiulize, inakuwaje mtu ambaye hasafiri, aweze kuwa na umiliki wa tiketi zaidi ya tano kisha kuziuza kwa bei anayotaka yeye na si ile iliyopangwa na mwenye meli kwa kushirikiana na mamlaka za usafiri? Tena, ukiisha nunua anakupeleka dirishani kubadilisha jina, hapa kama sio kuna mchezo mchafu ni nini? Kumbuka ili kusafiri kati ya Zanzibar na Dar ni lazima mtu atoe kitambulisho, sasa hao walanguzi wanazipataje? Unadhani wale wafanyakazi wa zile boti hawahusiki? Hawa wanajuana kabisa mpaka kwa majina na huwa wanapeana mgawo!

Ninakushangaa unaposema kwamba hao walanguzi wapo hata hapa Dar, wrong+wrong does not imply it is a right thing to do! Pia asante kwa kukiri kwamba utapeli wa kuuziwa tiketi fake upo sana hapa Zanzibar. Hili ni tatizo na ndipo ambapo mamlaka zinazohusika zinapaswa kuingilia kati ili kukomesha tabia hiyo. Lakini pia watu wako hapa kukemea hizo tabia na pia kuwe na justification kama sio maelezo elekezi kwamba unapotakiwa kusafiri ni kiasi gani cha mzigo + ujazo (volume) kinachoruhusiwa abiria kusafiri nacho bure kama kwenye ndege (Hand luggage). Vinginevyo tatizo litaendelea na wajanja watatumia mwanya huo kuibia wasafiri na kuharibu sifa nzuri ya kampuni.
 
Last edited by a moderator:
Acha ushamba WAPONA ndio maana umeibiwa,boat haina Driver,na walikuona Zoba ndio maana ukapigwa pesa hiyo.
Labda kwa kukutaarifu tu kwa sie wazoefu wa Boats hizi,kuna siku ticket zinauzwa za boat moja na ikijaza kuna siku zinaondolewa Boats mbili kwa wakati mmoja.
Sasa kama tu unapigwa pesa hiyo 40 - 50 si bora ungeongeza kidogo ukapanda Precision Air.

We nawe ushakunywa wanzuki huko unakuja kutuchafulia hali ya hewa, hujaelewa halafu povu LA mdomo linakutoka bure, mwenzio kasema diver, we unakurupuka "kwenye meli hakuna driver" sasa diver na driver wapi na wapi. Picha linaanza umeingia chaka, jamaa nmeona anaitwa wapoma na sio wapona, type error ni kosa dogo tu LA kibanadam zaid lakin kwa kuwa umetuchanyia madawa driver na diver, litahesabika ni kosa kubwa na ni kawaida yako mkuu
 
Acha ushamba WAPONA ndio maana umeibiwa,boat haina Driver,na walikuona Zoba ndio maana ukapigwa pesa hiyo.
Labda kwa kukutaarifu tu kwa sie wazoefu wa Boats hizi,kuna siku ticket zinauzwa za boat moja na ikijaza kuna siku zinaondolewa Boats mbili kwa wakati mmoja.
Sasa kama tu unapigwa pesa hiyo 40 - 50 si bora ungeongeza kidogo ukapanda Precision Air.

Kwani Nauli ya Precision Dar Zanzibar kiasi gani mkuu?
 
Siwewi kukujibu,maana mtu mwenye unajiita Kigoli.sie watu wa pwani tunaitwa Mwali mchanga.
Nikikujibu nitakuwa nakuonea.Ngoja aje Lady Furaha au Masai Dada wa jinsia yako
Wala hunsumbui kichwa ww hondohondo unayeishi mkoani zanzibar
 
We kweli mnafiki wa Mungu.
Hivi unajua ni nani analeta Boats Brand New kwa safari ya Dar-Znz-Pba zaidi ya AZAM MARINE.
Watu wanashindana kwa ubora na sio porojo kama zako.Kwani umelazimishwa kupanda?
Kuna Sea Express na Seastar nk,mbona hamuendi kwenye boat zao.
Ubora unajiuza nyie acheni maisha ya kubahatisha.
Ni sawa na kuona baada ya muda Kituo Cha AZAM TV kinafunika utakuja kusema anafanya fitna,wakati amegharamia more than 50 Billions kuwekeza kwenye AZAM MEDIA.Sasa unategemea hao wa vituo vyetu vya kuungaunga watagusa.
Kuna watu kwenye Biashara zao wanatumia muda mwingi kujipanga kuja tofauti,wana keep time kwanza kukusanya nguvu.
Nyie mmeozoea kupanda boat za usiku mkijambiana usiku mzima mnatabu sana.Hii ndio side effect yake sasa
Kwa kifupi ni kwamba, ukiambiwa tatizo, na watu karibu wote wanakubali kweli kuwa hilo ni tatizo, lakini we pekee yako ndio huoni kama hilo ni tatizo, basi tambua wewe mwenyewe ndiye tatizo. Sijaona kinachokutoa mishipa hapa wakti ni kweli hilo suala lipo na linafanywa bila uficho. Kwa nature ya mahusiano na maingiliano ya Dar-Zanzibar, ni wazi kuwa uwezekano wa kupatwa na tatizo hili ni mkubwa, si suala la u-mjini, ujuaji au ushamba au vinginevyo. Sio safari zote kati ya maeneo hayo mawili ni planned. Kuna safari za misiba watu wanaenda kuzika, kuna safari za kusafirisha wagonjwa kutoka Mnazi Mmoja hospital kwenda Dar tena zinatokea hafla; ni saa ngapi mtu utaweza kukata tiketi siku 2 au 3 nyuma?

Kinachotakiwa ni kifuatilia na kukomesha utaratibu huu wa "mmateja" ambao kiuhakika pasipo shaka upo. Tiketi zikiisha ziwe zimeisha. Ushawahi kuona tiketi za ndege ukaambiwa zimeisha halafu anatokea mtu from nowhere akakuuzia na still ukapata nafasi ndani ya ndege hiyo? Labda Air Tanzania! Na matokeo yake si sote tunayaona? Sasa ndugu yangu Zanzibar Spices wacha blabla, zile boti za Da-Zanzibar hauzijazi wewe pekee kiasi ya kujihisi ndiye pekee unayejua au mwenye uzoefu sana wa kusafiri baina ya maeneo hayo mawili. Tiketi za mateja zipo, wanaouza wapo, polisi wanajua, walinzi wa yale mageti wanajua kwani wakati mwingine wanaouziwa hizo tiketi za kulangua wanapita kwa majina tofauti na IDs zao, aidha wakati mwingine kweli hubadilishiwa na wahusika wa Azam. Aidha kuhusu customer care zao, haina ubishi kwamba ni mbovu. Mara kadhaa unaweza kwenda kupata huduma, hakuna anayejali wala mwenye shauku ya kumhudumia mteja-wamekaa katika madirisha yao, wala hawashughulishwi na ukiuliza wanajibu kwa taabu huku wakiwa bizzy na simu zao wakichati. Tunatarajia kuona wakiwa pale, waache kuchat na watumie Extension line tu kwa mawasiliano ya kikazi.

Kwa kusema hivi, si kwamba tuna nia mbaya na Bakhressa, tuna nia ya dhati kabisa kwani mi binafsi ni mnufaika wa ajira kutoka makampuni ya Bakhresa. Vilevile, unapowakashfu wanaopanda zile boti za usiku, ima utakuwa ni mtoto sana au ni limbukeni wa usafiri baina ya Zanzibar na Dar. Hebu jiulize, hizi boti za kisasa za Bakhresa zimeanza lini na usafiri kati ya maeneo hayo umeanza lini? Tujiweke kuwa wakweli na kusema kweli tupu bila ya kumuogopa mtu yeyote kwa kupata fadhla za Mola Muumba. Huo ndiwo ubinadaam.
 
Last edited by a moderator:
Acha ushamba WAPONA ndio maana umeibiwa,boat haina Driver,na walikuona Zoba ndio maana ukapigwa pesa hiyo.
Labda kwa kukutaarifu tu kwa sie wazoefu wa Boats hizi,kuna siku ticket zinauzwa za boat moja na ikijaza kuna siku zinaondolewa Boats mbili kwa wakati mmoja.
Sasa kama tu unapigwa pesa hiyo 40 - 50 si bora ungeongeza kidogo ukapanda Precision Air.

Nimeandika Diver sio driver!! Usikurupuke Bro!!!!!!!!!!!
 
Kwa mtazamo wangu naona mleta mada anasema kitu kinachojiri mwenye maisha ya kila siku na hili washakutana nalo wengi kutokana na michango yao na mimi binafsi nakubaliana na yeye kwasababu nilishakutana na hili tena wakati nasafiri kutoka zanzibar kwenda dar.Tuliambiwa ticketi zimeisha ikisha mtu mwengine akatuuzia zenye majina tofauti kwa gharama ya juu zaidi na akaongea na askari getini tukapitishwa tu na mimi ilikuwa mara yangu ya pili kwenda zanzibar,hii ni aibu kwa kampuni inabidi hatua miliki zichukuliwe kwasababu inaharibu reputation ya Bakhressa na yeye ndo mwenye mamlaka ya kampuni anapaswa ajue hili.Inawezekana ndio wateja ni wengi kwasababu Azam ni kampuni kubwa na kitu kingine watanzania walio wengi wanafikra mgando na kila mtu keshazoea ana mwenzake wa kumbana kwenye hongo kwa njia moja au nyingine ndio maana walio wengi wanaona ni sawa.Lakini fact ni kwamba si sawa na haimaanishi wenye sauti zao wasipige vita suala hili tukikaa kimya maanake tunaliendekeza.Kitu kizuri tunatakiwa tukiimarishe na tukitunze sio tukae tukiangalie kikiharibika.Thats not the way things work.
 
Kituo kikuu cha Polisi malindi kipo meter 100 kutoka Bandarini.
Sasa mlionunua tickets za magendo na waliowauzia nani wa kulaumiwa?
Yaani nisawa na mtoa rushwa na mpokeaji.
 
Kituo kikuu cha Polisi malindi kipo meter 100 kutoka Bandarini.
Sasa mlionunua tickets za magendo na waliowauzia nani wa kulaumiwa?
Yaani nisawa na mtoa rushwa na mpokeaji.

Unajitahidi sana kutetea hii issue kiongozi, lakini kwanini usiruhusu uchunguzi wa hizi tuhuma.
Najua ni haki yako kutetea kibarua chako, ila penye tatizo hatutaacha kuongea kaka...

NASHAURI TENA, NENDA KAULIZE WASAFIRI 10 TU, MATATIZO YALIOPO KATIKA USAFIRI HUO NDIO UTAPATA JIBU..USITETEE TU KIONGOZI, CHUNGUZA
 
Hii ndo Africa usjali maisha yanaendelea tatizo la nauli kupanda lipo wala si jambo geni tena sio Zanzibar wala Dar es salaam kikubwa unatakiwa uwe mjanja wakwenda na waswahili kata ticket kabla na kuhusu huyo bakhresa si kwamba halijulikani linajulikana maana halijaanza leo wala jana tabia hizi toka miaka minne nyuma sijui kama haizidi.

Kuhusu mzigo ww lipa tu huna budi maana kutokulipwisha inakuwa km bahati kuna siku nilipita na baiskel ya mtoto kwenda dar majamaa wakataka niwape buku kumi kwa hasira nikawambia hamuoni aibu nikawatolea nikawapa ila wakaona aibu wakaikataa.
 
Wana JF kama nitakosea naomba kuelimishwa, ninavyojua mimi abiria iwe wa ndege au boat hizi,

Mzigo hitajika ni kg isiyozidi 20, sasa mimi nimesafiri toka Zanziber kwenda Dar nimenunua oven yangu ndogo tu na isiozidi kg 15, nikahitajika kulipia elf 10.

Na ukifika hata asubuhi pale ofisini kutaka ticket ya bei ya kawaida 23,000 unaambiwa zimeisha, ila zipo zinauzwa nje kwa Tshs 50,000, yaani ni watu wamezinunua kisha wanauza kwa magendo.

Nilivyo lalamika zaidi nilijibiwa sio lazima kutumia chombo hicho...

Haya kwangu niliona ni manyanyaso makubwa...na sijui kama mmliki ambaye ni Bakharesa anafahamu unyama huu wa wafanyakazi wake..

Naomba Bakheresa pale ulivyo chunguza tuhuma hizi, imekuwa ni kero sana.
Halafu haohao ndio wanasema Dini yao ni ya haki ilihali hawatendi haki

Hiyo ni DHULUMA na wanajua.
 
Wana JF kama nitakosea naomba kuelimishwa, ninavyojua mimi abiria iwe wa ndege au boat hizi,

Mzigo hitajika ni kg isiyozidi 20, sasa mimi nimesafiri toka Zanziber kwenda Dar nimenunua oven yangu ndogo tu na isiozidi kg 15, nikahitajika kulipia elf 10.

Na ukifika hata asubuhi pale ofisini kutaka ticket ya bei ya kawaida 23,000 unaambiwa zimeisha, ila zipo zinauzwa nje kwa Tshs 50,000, yaani ni watu wamezinunua kisha wanauza kwa magendo.

Nilivyo lalamika zaidi nilijibiwa sio lazima kutumia chombo hicho...

Haya kwangu niliona ni manyanyaso makubwa...na sijui kama mmliki ambaye ni Bakharesa anafahamu unyama huu wa wafanyakazi wake..

Naomba Bakheresa pale ulivyo chunguza tuhuma hizi, imekuwa ni kero sana.
Hili la TICKET hata kwenye mabasi linafanyika wakati wa high seasons ambazo zina wasafiri wengi... NIMEWAHI KUFANYIWA HIVYO DAR - ARUSHA na KAHAMA - DAR

Kikubwa KAMPUNI.IWEKE MFUMO RAFIKI KWA ABIRIA KAMA ILIVYO KWA NDEGE
 
Back
Top Bottom