Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi yagaragazwa Bungeni

Enzi za ba Mkapa haya yangetokea bungeni? Nani wa CCM angesimama hasiunge mkono hoja? Mapinduzi haya japo madogo yameletwa na nani? Nijuze
<br />
<br />
Yameletwa na mwamko ulioasisiwa na operation sangaraBila upinzani makini haya yasingetokea.
 
anasema ikiwezekana tuendeshe kipande chetu cha tazara na wazambia waendeshe kipande chao, tazara inawanufaisha wazambia tu.
 
Amesema anajivunia kuongea kama mbunge wa CCM kwa kuwa watu wanasema wabunge wa CCM hawaikosoi serikali yao.

Zambi pia ameisifu kamati kuu ya CCM kwa kuitaka serikali ipunguze bei ya mafuta.
 
Wabunge wa CCM waliosema kuwa hawaipitishi bajeti walikuwa wanaimba ili kujifurahisha. In fact, mbunge wa CCM kutoisupport bajeti wanaitafsiri kama utovu wa nidhamu. Ya ngeleja yaliwashinda, lakini wangeipitisha tu
 
amemaliza Zambi anaanza Halima Mdee, anasema hili suala ni letu sote, halichagui chama, rangi wala kabila
 
Omary Chambo baba kapewa ukatibu wizara ile kisha anabolonga kishenzi eti kisa anauhusiano na rais, sehemu nyingi kaziboronga sana. Toka alipoondoka Bw. Msoma na Engineer Kijazi basi tabu tupu wizara hii, ni wakati sasa Rais kuteua katibu mkuu mpya wizara hiyo na ndo maana magufuli alimkataa katibu mkuu omary chambo ktk wizara yake.
 
Godfrey Zambi wa CCM ameamua kujivua gamba hapa. Anaiponda serikali kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake. UDA, ATCL, TRL na tume ya jiji ivunjwe. Amemtaka Waziri Mkuu aivunje Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kuwa kuna rushwa za wazi.

Pia amesema kwamba Managing Director wa sasa wa TAZARA ambaye ni Mzambia ana mpango wa kugombea urais huko kwao. Kwa hiyo anatafuta pesa kwa nguvu zote!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Amemtaja Juma Kapuya kama mwanahisa wa Kampuni ya Simons group iliyouziwa UDA, na anasema kamati ndogo iliyoundwa kuchunguza sakata lote Kapuya nae alikuwepo, kwa hiyo ni kama kesi ya nyani kumpelekea ngedere, amemtaka Kapuya kudeclare interest na kuomba radhi kwa kuidanganya kamati.
Amesema serikali haitaki kutoa tamko kazi yake ni kuomba miongozo tu na kuchukua hiyo hela na kujenga mahekalu Ulaya.

Iddi Simba ni mwenyekiti wa Body ya UDA,Prof. Juma Kapuya mdau wa Simons group iliyouziwa UDA, na yule mwenyekiti wa Simons group(jina limenitoka)-ni rafiki wa karibu wa kibiashara na RW1 KIKWETE. Taratibu tunaanza kupata network ya ili diri.Hawa wote ni wenyeji wa ikulu, ni biashara kutoka Ikulu. Masikini Nyerere alikua hajui ikulu kuna biashara gani-Biashara zenyewe ndio hizi.
 
Enzi za Mkapa angalau kazi ilikuwa inaonekana! Mkapa alikuwa mkali sana kwa mawaziri wake. Na hata ukiangalia pesa nyingi ya EPA na madudu mengine yalifanyika mwishoni kabisa wa utawala wake tena alipokuwa ameanza kuumwa miguu mara kwa mara. Serikali ya Mkapa ilikuwa inaweka malengo na inayasimamia kwa nguvu zote!

Hii serikali ya sasa ukiwauliza wameshafanya nini cha maana tangu waingie madarakani watajibu nini?

Hahhaaha dah mkuu umenichekesha sana. hapo kwenye mguu

Ina maana huwezi kupata rais bora kama hawezi kuteambea au ni mlemavu wa miguu.??? Ikulu ni jeshi?

Mkapa naye fisadi tu kwanza ile ndege aliyonunua lazima ilikuwa na 20% kubwa tu sema bado halijafumuka.........
 
Mdee amewapongeza wabunge wote kwa kutounga mkono hoja na yeye hauingi hoja.

Anasema aibu ya UDA ni aibu ya wabunge wote wa Dar. Ameita maamuzi ya kuiuza UDA kama ufedhuli, na wabunge wote wa Dar hawakushirikishwa.

Anasema kwa hili meya wa jiji hawezi kukimbia uwajibikaji.
 
Nadhani kuna issue mbili ambazo ni muhimu kuziangalia. Mwananchi/Citizen kama watu wengine wamelichukulia suala hili kwa mwanga wa "kutouzwa halali" kana kwamba ingeuzwa kwa bei ya juu na halali basi kusingekuwa na issue. Kwangu mimi, tatizo ni zaidi ya kuuzwa kwa bei ya chini, tatizo langu ni kwanini UDA haikuchukua majukumu ya DAR na kubadilishwa kuwa huo wakala wa Usafiri wa Haraka? Kiakili na kimantiki haikubaliki kuona kwamba UDA iiliyoundwa kusimamia usafiri wa umma jijini la Dar haikubadilishwa na kuifanya iwe ndio DART - yaani angalau wangeweka iwe UDART kuonesha mabadiliko hayo. Tatizo langu ni kuwa kwa jiji kama Dar lenye wakazi milioni karibu 4 wengi wao wakiwa ni wa kima cha chini na kati usafiri wa umma ndio suluhisho sahihi kwa wakazi hao. Haiwezekani kila sikuw awatu wanalalamikia usafiri na congestion lakini hawaoni kwamba kwa mtindo uliopo sasa wanalazimisha watu wengi kuwa na magari yao hata kama si lazima kiuchumi.

Ningefurahi sana kama kungekuwepo na watu kule Mwananchi/Citizen ambao wangeweza kuarticulate hii issue kwa mwanga huo. Tatizo siyo bei ya UDA ilivyouzwa bali gharama ambayo wananchi wanalipa na taifa linalipa hasa jijini Dar kwa UDA kuuzwa.

https://www.jamiiforums.com/hoja-nz...ashara-na-dart-siri-ya-kuuzwa-bei-chee-4.html

Naona wabunge nao wame narrow arguments zao.
 
Iddi Simba ni mwenyekiti wa Body ya UDA,Prof. Juma Kapuya mdau wa Simons group iliyouziwa UDA, na yule mwenyekiti wa Simons group(jina limenitoka)-ni rafiki wa karibu wa kibiashara na RW1 KIKWETE. Taratibu tunaanza kupata network ya ili diri.Hawa wote ni wenyeji wa ikulu, ni biashara kutoka Ikulu. Masikini Nyerere alikua hajui ikulu kuna biashara gani-Biashara zenyewe ndio hizi.
Yataibuka mengi
 
Wabunge wa CCM waliosema kuwa hawaipitishi bajeti walikuwa wanaimba ili kujifurahisha. In fact, mbunge wa CCM kutoisupport bajeti wanaitafsiri kama utovu wa nidhamu. Ya ngeleja yaliwashinda, lakini wangeipitisha tu


Mapinduzi haya yameletwa kutokana na upinzani kuwa strong, enzi za Mkapa hapakuwa na upinzani ulio imara kama sasa hivi istoshe hata hivyo mkapa alikuwa anajitahidi katika bajeti zake zote.
 
Mwakyembe ameomba mwongozo, mwenyekiti kamchinjia baharini.
 
Mdee anasema kama nchi hatuchoki kuwapa madaraka watu ambao sio waaminifu. Anahoji leo UDA imekuwa Pride, leo UDA imekuwa mtu fulani, lakini watu bado wezi hawa wanatembea mtaani, isipokuwa vibaka ndio wanaishia selo. Kwa nini hawachukuliwi hatua?
 
Anaiomba serikali ilichukulie suala la UDA kwa mapana yake, tunapoangalia maslahi ya nchi tuweke maslahi ya vyama pembeni.
 
Back
Top Bottom