Bahlul na mfanya biashara

KABAVAKO

JF-Expert Member
Apr 5, 2011
229
32
Siku moja mfanya biashara wa Baghdad alimwendea Bahlul kwa kutaka ushauri wake. Alimwambia:

"Ewe Sheikh Bahlul! Naomba ushauri wako katika ununuzi wa bidhaa ambazo zitanipatia faida nyingi."

Bahlul alimjibu:
"Chuma na Pamba" (mapokezi mengine yanataja tende na pamba).”

Mfanyabiashara huyo aliyafuata mashauri hayo, na akapata faida kubwa sana katika kipindi kifupi. Ikatokea tena kukutana na Bahlul. Hapo alirudia ushauri wake kwa kusema:
“Ewe Bahlul Mwehu! Je ninunue bidhaa zipi ili nipate faida nyingi?"

Safari hii Bahlul alimjibu: “Vitunguu na matikiti maji."


Hapo mfanya biashara huyo alitumia fedha zake zote kwa kununulia bidhaa hizo akitarajia kupata faida zaidi. Baada ya kupita siku chache, bidhaa hizo zikaanza kuoza na hivyo kusababisha hasara kubwa mno. Hapo alitoka kumtafuta Bahlul na alipomwona alimwambia "Nilipokutaka ushauri mara ya kwanza ulinishauri kununua chuma na pamba (tende na pamba) kwa hiyo nilifaidika mno lakini mara ya pili, umenishauri kununua vitunguu na matikiti maji, maboga yote yameoza kwa hivyo nimefilisika kabisa........."

Bahlul alimkatiza na kumwambia, "Mara ya kwanza wewe uliniita "Ewe Sheikh Bahlul!" na kwa kuwa uliniamini mimi ni mtu mwenye akili hivyo nilikupatia mashauri ya akili. Na kwa kuwa mara ya pili uliniita 'Ewe Bahlul mwehu' na kwa kuwa uliamini mimi ni mwehu, basi nilikujibu kiwehu.....!.


Hapo mfanya biashara alibung'aa kwa majibu hayo na alielewa maana na kujiondokea kimya kimya.

Fundisho: Islam inasisitiza ushauri kama alivyosema Mtume s.a.w.w.:- "Ushauri ni kinga dhidi ya tabu na usalama wa kutolaumiwa na watu...... na Atakaye ushauri husaidiwa......"
 
Back
Top Bottom