Invigilator
JF-Expert Member
- Aug 16, 2016
- 3,219
- 6,080
Mkuu una uwezo mkubwa sana wa kuwasilisha jumbe M.Mungu kakutunuku kipaji cha pekee mno,keep on brother!!.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app
Nashukuru sana mkuu DukesonMkuu una uwezo mkubwa sana wa kuwasilisha jumbe M.Mungu kakutunuku kipaji cha pekee mno,keep on brother!!.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kisa au mkasa?
Ni kweli. Na pia huambiwa kuwa ni asilimia ndogo sana ya yale yaliyomo baharuni ndiyo yanafahamika kwa binadamu.Kijiji flani Kusini ya Zanzibar wavuvi wanaandaa zana zao tayari kwenda kutarazaki, Baada ya muda Ngalawa ndogo ikawasafirisha umbali mrefu kidogo tayari kwa kuanza shughuli zao za uvuvi, wawili kati yao wanafungwa kamba ndefu kwa kila mmoja mguu wa kushoto pamoja na vioo maalum usoni na mitengo wakapiga mbizi kwenye kina kirefu tayari kwa kuanza kazi. Ndani ya dakika 5 mmoja akaibuka akiwa mzima lakini asieweza kuongea mwengine akaibuka ndani ya dakika saba akiwa hajiwezi taabani, kazi ya uvuvi ikaishia hapo. Yule wa pili alifariki asubuhi ya siku inayofata, mwengine aliugua kwa miezi sita akiwa hajitambui kabisa, baada ya jitihada kubwa kuchanganya madawa asili na madawa ya hospitali taratibu alianza kupata nafuu. Baadae alikuja kuhadithia kuwa walipopiga mbizi chini kabisa waliona wasichana wawili wakiwa na maumbili ya kibinaadamu kabisa (sio Nguva) mmoja akimsuka nywele mwenzake, kuchanganyikiwa yeye akawahi haraka kurudi juu kukawa na interval ya dakika 2 na hajui mwenzake kilimtokea nini mpaka kufikia kufariki siku iliyofuata. Bahari ina siri nyingi sana.