Bado nakupenda sana

Bado nakupenda sana

Joined
Nov 25, 2019
Posts
9
Reaction score
2
BADO NAKUPENDA SANA :05
Sikutaka kubishana sana na Hansy, nilikubali na kwakuwa nilikuwa nimechoka sana ilinibidi niage, nilitembea hatua chache akaniita kwa unyonge "Ney. " Nami nilisimama na kumgeukia, aliniambia "samahani Ney, Nisamehe leo sipo sawa niachie namba yako nitakupigia. "

Niliingiwa sana utu na hamu yakutaka kujua tatizo la Hansy hivyo nilimgeukia na kumtajia namba yangu ya simu "0754520438." "Asante sana. " alishukuru na mimi nikaendelea na safari yangu mpaka nikafika nyumbani.

Nilipofika nyumbani, mama yangu tayari alikuwa amemaliza kazi zote, nilimsalimia mama na kwakuwa ilikuwa jioni giza lilitanda tayari, niliingia chumbani nikaweka simu yangu katika sehemu ya kuchaji kwani tayari haikuwa na moto, nami nikabadili nguo na kuelekea kuoga, baada ya hapo nilirudi chumbani nikavaa nguo ya kulalia na nikatoka sebuleni nilipomkuta mama yangu anakula huku akiangalia runinga, nami nilipakua chakula nikaungana na mama, mama yangu alikuw mtu wa kuchekesha sana hivyo tulijikuta tunacheka sana na nikasahau kabisa maudhi ya aliyekuwa mpenzi wangu na makwazo yake, niliondoa vyombo nakuingia chumbani kwangu, nilipofika nilikuta taarifa kwamba aliyekuwa mpenzi wangu alinipigia yaani nilikuta (missed call) yake.

Nilikunja uso kwani nilijua wazi atanikera, wakati natafakari hilo alipiga nikapokea akaanza kwakusema "mke wangu niambie. "Nilijikuta nakasirika kwani ilikuwa tabia yake kunikera na kujifanya ananipenda akihitaji msaada kwani mpaka wakati ule sikuelewa.........
Screenshot_20191204-132724.jpeg

============
Sehemu ya sita

=============
Sehemu ya saba
============
Sehemu ya nane
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom