Granite
JF-Expert Member
- Jul 6, 2016
- 290
- 648
Taifa lolote ama jamii yeyote ina njia mbili za kufanya mageuzi ya mfumo wa kujitawala, Njia ya kwanza ni njia ya Amani kwa majadiliano, maridhiano na mapatano yanayoweka mizania ya kujiongoza. Njia ya pili ni vurugu au nguvu baina ya makundi mawili.
Kundi linalotawala linataka kuendelea kufurahia matunda ya nafasi ya utawala na kundi lisilorizishwa na Wanao tawala. Njia ni mbili, ni jambo la heri Taifa letu halijawahi kupitia njia ya 2, toka tunapata uhuru tumekua na mabadilishano ya Amani, vurugu zimekuwepo miaka yote lakini sio vurugu kama ambazo mataifa jirani yamezipitia na yakapelekea kutoa mifumo iliyokuwepo.
Watanzania hawajafika hatua ya kuona gharama ya mageuzi ni ndogo kuilipia kuliko kuendelea na hali waliyonayo. Bado watanzania walio wengi hawapo Tayari, Wapo Watanzania wanaotamani mageuzi, wanakiu ya kuona falsafa Mpya ya Uongozi wa Taifa letu lakini ni Wachache miongoni mwao wapo Tayari kulipa hiyo gharama wengi bado ni nafuu waendelee kuwa hivi tulivyo.
Hatujui ni lini lakini lpo siku watakuwa tayari, tunaweza tusiishuhudie wengine ila wapo watakaoshuhudia. Taifa hili watu hawajaanza kutekwa, kupotea, kubambikiwa kesi, kuuwawa haijaanza leo. Wa koloni waliua, awamu zote zimefanya hayo matendo utofauti ni miaka na maendeleo ya teknolojia, wakati leo tunashangaa watu kupotea na kutekwa, tumesahau Uchaguzi wa 2000 waliuwawa watu zaidi ya 30 siku 1 mchana kweupe na maisha yaliendelea.
Kundi linalotawala linataka kuendelea kufurahia matunda ya nafasi ya utawala na kundi lisilorizishwa na Wanao tawala. Njia ni mbili, ni jambo la heri Taifa letu halijawahi kupitia njia ya 2, toka tunapata uhuru tumekua na mabadilishano ya Amani, vurugu zimekuwepo miaka yote lakini sio vurugu kama ambazo mataifa jirani yamezipitia na yakapelekea kutoa mifumo iliyokuwepo.
Watanzania hawajafika hatua ya kuona gharama ya mageuzi ni ndogo kuilipia kuliko kuendelea na hali waliyonayo. Bado watanzania walio wengi hawapo Tayari, Wapo Watanzania wanaotamani mageuzi, wanakiu ya kuona falsafa Mpya ya Uongozi wa Taifa letu lakini ni Wachache miongoni mwao wapo Tayari kulipa hiyo gharama wengi bado ni nafuu waendelee kuwa hivi tulivyo.
Hatujui ni lini lakini lpo siku watakuwa tayari, tunaweza tusiishuhudie wengine ila wapo watakaoshuhudia. Taifa hili watu hawajaanza kutekwa, kupotea, kubambikiwa kesi, kuuwawa haijaanza leo. Wa koloni waliua, awamu zote zimefanya hayo matendo utofauti ni miaka na maendeleo ya teknolojia, wakati leo tunashangaa watu kupotea na kutekwa, tumesahau Uchaguzi wa 2000 waliuwawa watu zaidi ya 30 siku 1 mchana kweupe na maisha yaliendelea.