Msanii tajwa fani ya muziki na filamu Baby Madaha aelezea changamoto zinazoua wasanii ktk fani zao ni za kimfumo.
Baby Madaha anashangaa kuwa msanii wa umri wa miaka 36 hapa Tanzania anahesabika ni kama gari la namba plate TZA wakati huko Marekani ya Kaskazini, Latin Amerika Ulaya, Mashariki ya Kati na Asia jambo la mtu kuwa na kipaji haliangalii umri bali uwezo wa kuitumikia fani ndiyo jambo la msingi.
Msanii wa kimarekani fani ya muziki Dolly Parton aliyezaliwa mwaka 1946 na sasa 2022 ana umri wa miaka 76 bado yupo juu katika fani na anaheshimiwa na kualikwa kufanya kazi za matamasha na wadau wa rika zote
Mbali ya wasanii waimbaji haya watayarishaji wa muziki yaani maproducer wa umri mkubwa kama Quincy Jones wanaheshimika huko mbele na wanatafutwa na wadau wa rika zote wafanye kazi na Quincy Jones
Baby Madaha anaongeza kuwa mchawi wa kupunguza kasi ya ubunifu wa kazi za wasanii wa kiTanzania kuendelea mbele ni sisi wenyewe. Wenzetu huko ma-mbele wanaendeleza waliotangulia na kuongezea walipofika na wa jana wanashirikiana na wale wa leo katika industry iwe artists, promoters, producers, sponsors, media platforms owners, audiences na kwa pamoja wanaendeleza industry kupanuka ndani na kimataifa kwa kazi bora zaidi .
Baby Madaha anasikitika sana na hali hii pamoja ya kuwa sasa dunia imefunguka kwa kuwepo media platform huru zisizo na mageti ya kufungia vipaji vya wasanii wa kiTanzania vilivyopo lakini kiroho bado kuna vita ya 'uchawi' kufifisha vipaji vya wasanii wetu Tanzania
Latino America : Buena Vista Social Club - Chan Chan
Industry ya kiTanzania ya music na entertainment pia inaenzi wanamuziki wa nje kwa kualika wanamuziki au bendi toka nje na kufifisha muziki wetu wa dansi ya kitambaa cheupe ambao unaheshimika sana hapa ndani na kimataifa lakini industry yetu tunaudharau kwa kuubania pia muziki wa dansi
"Kitambaa Cheupe" - King Kikii na Wazee Sugu