Kama ulikwenda kwa Babu pole, subiri zamu yako.Wajinga ndio waliwao.Tulisema ushenzi anaoufanya mpuuzi yule, una mkono wa shetani mkakaza shingo,mtavuna mlichopanda.
Siasa hizo mkubwa.
Babu Kikombe alikuwa turufu ya Kisiasa?
Miezi minne iliyopita Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Ambilikile Masapila aliiomba Serikali imsaidie kupata gari la kubeba dawa, vyombo vya kunywea, kuni na vyombo vikubwa vya kuchemshia dawa hiyo ili kukabili wingi wa Wagonjwa waliokuwa wakijitokeza kupata Tiba katika kijiji cha Samunge huko Loliondo.
Maoni ya wagonjwa waliopata Tiba kila mmoja alijibu kwa staili ya aina yake, wengine walisema "Sijui kama nimepona kabisa au la, lakini sasa najisikia vizuri tofauti na mwanzo,"
Baadhi ya watu wenye Virusi Vya Ukimwi (VVU), ambao wamepewa dawa hiyo, licha ya kudai kuwa sasa wana hali nzuri, bado hawajapima kuthibitisha uponyaji huu wa ajabu.
Utashangaa ndani ya kipindi hiki kifupi cha ndani ya miezi minne kutoka maombi hayo ya Babu hadi tamko la Waziri Mkuu, Kasi ya kwenda Loliondo bado ipo lakini si kwa kiwango cha juu kama kipindi hicho,kwa sasa barabara ni nyeupe na ukifika muda huo huo unapata tiba na kuondoka.
Ni kweli wagonjwa wamekwisha? wamepungua kwa kiasi hicho? au hali ngumu ya ukata kuweza kugharamia safari hadi Loliondo? Maswali yote haya majibu yanabaki kuwa katika mioyo wa watanzania.
Kiini cha hoja yangu ni ukimya uliopo kwa baadhi ya taarifa za kufedhehesha kuhusu mamia ya watanzania waliopoteza maisha licha ya kugonga kikombe kwa matumaini makubwa kabisa kuwa afya zao zingetengemaa kama awali.
Naandika haya nikiwa na uthibitisho wa zaidi ya vifo kumi huku simulizi kutoka kwingineko zikinukuu vifo vingi zaidi, kibaya ni mlipuko wa vichaa wengi kutokana na kukatiza ARVs, ushahidi wa kitabibu unaonyesha mgonjwa anayekatiza ARVs ghafla ana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa hilitafu ya akili.
Wengi wamekimbizwa mahospitalini kwa hofu kwa malaria zimepanda kichani kumbe tayari walikwishakatiza dozi kwa matumaini ya kupata ahueni kupitia kikombe cha miujiza.
Hivi kwa nini serikali iliingia kichwakichwa katika hili, na kwa nini wanahabari hawaandiki madhara haya ya kikombe zaidi ya Ushabiki, hii ni ajenda ya nani hasa na nini mwisho wake kwa matokeo haya ya kudhoofisha kabisa katika jamii ya watanzania.
Sasa hoja iliyopo mezani wenyewe mnaijijua babu kasahaulika kabisa. Mchezo huu mchafu hadi lini??
Adios
muulize baba batilda biriani