Baba wa Taifa na tatizo la Udini

King...
Nimeona baada ya Sesten kuweka ushahidi ule wa yanayofanyika na watendaji wa serikali dhidi ya Waislam ukumbi umekuwa kimya sana.

Nimerusha ule ushahidi wake na umesomwa kwa kupasiana na umewafikia watu wengi.
Hili sikutegemea.

Nimehamasika na nimeingia Maktaba kutafuta yale ambayo yanafanana na aliyotueleza Sesten.

Hebu someni kisa kingine hicho hapo chini:

View attachment 2105736
Mwalimu Athmani Khalfan Mrindoko Mwalimu wa Shule ya Msingi

Mwalimu Athmani Khalfani Mrindoko Mwalimu wa Shule ya Msingi Lwande Handeni Kosa Lake Kusomesha Wanafunzi Qur'an na Kukataa Kuchakachua Mitihani

Mwalimu Athmani Khalfani Mrindoko alikuwa mwalimu wa shule ya msingi Lwande moja ya vijiji ambavyo mwaka wa 2013 vilivyoshambuliwa kwa tuhuma za ugaidi.

Mwalimu Athmani alikuwa mwalimu mwajiriwa na serikali kusomesha masomo ya kisekula lakini kwa mapenzi yake katika Uislam kwa kuwa walimu wa somo la dini ya Kiislam Shule za Msingi hakuna yeye alijitolea kuwasomesha wanafunzi hawa dini ya Kiislam na kuwatungia mitihani.

Kisa chake ni kisa cha kusikititisha na kuhuzunisha.

Siku za nyuma Mwalimu Athmani alifatwa na walimu wenzake akaelezwa kuwa imetoka amri juu kuwa walimu washirikiane kuwafaulisha watoto darasa la saba kwa kuwakokotolea wanafunzi majibu ya mtihani wa mwisho wa darasa la saba ili kunyanyua ufaulu wa shule na hatimaye wilaya.

Mwalimu Athmani akakataa hili kwa misingi ya Uislam kuwa hicho kitendo ni ghushi yaani udanganyifu.

Akawaeleza kuwa imani ya dini yake inakataza mambo kama hayo.
Udanganyifu huu ukakwama na sababu ikawa ni yeye Mwalimu Athmani.

Hapa ndipo zilipoanza chuki dhidi yake.

Sasa lilipotokea sakata la Lwande askari waliovamia kijiji kwa madai ya kupambana na Al Shabab Mwalimu Athmani akakamatwa, kupigwa na kufunguliwa kesi ya kujeruhi Mahakama ya Handeni.

Mwalimu Athmani sasa hivi ni masikini.

Alipoachiwa gerezani kwa dhamana alikuta nyumba yake imevunjwa na vitu vyake vyote vimeibiwa.

Huyu ndiye ''gaidi'' anaesemekana alikuwa akishirikiana na Al Shabab.
Hapakuwa na ushahidi wa ugaidi hivyo akaachiwa na kazi akaachishwa.

Mwalimu muadilifu anaesomesha watoto kitabu cha Allah na kuwafunza maadili mema kwa mfano, Mwalimu Athmani Khalfan Mrindoko akazuliwa kuwa ni ''Al Shabab,'' bila ya ushahidi.

Haya ni machache.
Yapo mengi katika dhulma hii ya kumfanya mtu akabubujikwa na machozi.

Sasa imepita karibu miaka 9 sijapata taarifa za Mwalimu Mrindoko.
Allah uwahifadhi waja wake.Bila shaka atakuwa mahali salama.
 
King...
Nimeona baada ya Sesten kuweka ushahidi ule wa yanayofanyika na watendaji wa serikali dhidi ya Waislam ukumbi umekuwa kimya sana.

Nimerusha ule ushahidi wake na umesomwa kwa kupasiana na umewafikia watu wengi.
Hili sikutegemea.

Nimehamasika na nimeingia Maktaba kutafuta yale ambayo yanafanana na aliyotueleza Sesten.

Hebu someni kisa kingine hicho hapo chini:

View attachment 2105736
Mwalimu Athmani Khalfan Mrindoko Mwalimu wa Shule ya Msingi

Mwalimu Athmani Khalfani Mrindoko Mwalimu wa Shule ya Msingi Lwande Handeni Kosa Lake Kusomesha Wanafunzi Qur'an na Kukataa Kuchakachua Mitihani

Mwalimu Athmani Khalfani Mrindoko alikuwa mwalimu wa shule ya msingi Lwande moja ya vijiji ambavyo mwaka wa 2013 vilivyoshambuliwa kwa tuhuma za ugaidi.

Mwalimu Athmani alikuwa mwalimu mwajiriwa na serikali kusomesha masomo ya kisekula lakini kwa mapenzi yake katika Uislam kwa kuwa walimu wa somo la dini ya Kiislam Shule za Msingi hakuna yeye alijitolea kuwasomesha wanafunzi hawa dini ya Kiislam na kuwatungia mitihani.

Kisa chake ni kisa cha kusikititisha na kuhuzunisha.

Siku za nyuma Mwalimu Athmani alifatwa na walimu wenzake akaelezwa kuwa imetoka amri juu kuwa walimu washirikiane kuwafaulisha watoto darasa la saba kwa kuwakokotolea wanafunzi majibu ya mtihani wa mwisho wa darasa la saba ili kunyanyua ufaulu wa shule na hatimaye wilaya.

Mwalimu Athmani akakataa hili kwa misingi ya Uislam kuwa hicho kitendo ni ghushi yaani udanganyifu.

Akawaeleza kuwa imani ya dini yake inakataza mambo kama hayo.
Udanganyifu huu ukakwama na sababu ikawa ni yeye Mwalimu Athmani.

Hapa ndipo zilipoanza chuki dhidi yake.

Sasa lilipotokea sakata la Lwande askari waliovamia kijiji kwa madai ya kupambana na Al Shabab Mwalimu Athmani akakamatwa, kupigwa na kufunguliwa kesi ya kujeruhi Mahakama ya Handeni.

Mwalimu Athmani sasa hivi ni masikini.

Alipoachiwa gerezani kwa dhamana alikuta nyumba yake imevunjwa na vitu vyake vyote vimeibiwa.

Huyu ndiye ''gaidi'' anaesemekana alikuwa akishirikiana na Al Shabab.
Hapakuwa na ushahidi wa ugaidi hivyo akaachiwa na kazi akaachishwa.

Mwalimu muadilifu anaesomesha watoto kitabu cha Allah na kuwafunza maadili mema kwa mfano, Mwalimu Athmani Khalfan Mrindoko akazuliwa kuwa ni ''Al Shabab,'' bila ya ushahidi.

Haya ni machache.
Yapo mengi katika dhulma hii ya kumfanya mtu akabubujikwa na machozi.

Sasa imepita karibu miaka 9 sijapata taarifa za Mwalimu Mrindoko.
Umekuwa kimya maana tukiuliza maswali unajibu kwa picha.
Mtoa mada ukienda kinyume nae Hana majibu.
Ila stori kama hizi ndo ulikuwa unazihitaj.Enjoy now

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
 
SAKATA LA KILINDI NA MAUAJI YA KILINDI NA MAUAJI YA KIJIJI CHA MADINA - HANDENI, KUPOTEA (KUULIWA) KWA RAJAB OMARI MTANA

Rajab Omar Mtana alikuwa ni mwanakijiji wa kawaida tu akiishi kijijini Lulago, Handeni kama wanavijiji wengine wanavyoishi na alikuwa na biashara yake kuuza hiliki kama mkulima wa zao hilo.

Siku moja akaja mnunuzi mfanyabiashara ya hiliki nyumbani kwake kununua hiliki na akamuuzia.

Yule mfanyabiashara alipokuwa anatoka na gari yake akasimama kwenye kizuizi cha kulipia ushuru.

Alipotakiwa kulipa ushuru akasema kuwa si hiliki yote amenunua katika kijiji hicho kwa hiyo hawezi kulipa ushuru wa hiliki yote.

Hapo palitokea ubishi na mfanyabiashara yule akagonga lile geti na akaondoka.

Hii ikapelekea kwa wakusanyi ushuru kwenda nyumbani kwa Rajab Omar Mtana kumkamata na kumweka chini ya ulinzi katika ofisi ya serikali ya kijiji hadi hapoatakapolipa ushuru ambao yule mfanyabiashara alitakiwa alipe.

Ndugu zake Rajab Omar Mtana wakenda pale ofisini kwa nia ya kumtoa ndugu yao na hapo pakatokea vurugu na mapigano.

Katika mapigano hayo, mgambo ambae ndiye aliyekuwa akishughulika na kudai ushuru akauawa.

Kisa hiki cha ushuru wa hiliki ndicho kilichozua balaa kubwa la mauaji na uchomwaji moto nyumba za Waislam wa Madina na kuvunjwa kwa misikiti na vijiji ambavyo vilikuwana idadi kubwa ya wakazi wake Waislam.

Baada ya haya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa akatoa amri kuwa hapana ruhusa tena ya sehemu ile kuwa makazi kwakisingizio kuwa hizo ni kambi za ugaidi.

Huyu bibi alisema mengi ambayo takriban yote yamedhihirika kuwa hayana ukweli mathalan kuwa kuna Al Shabab, mahandaki ya vita, silaha za kutungulia ndege nk. nk.

Alizungumza na Radio Nuur, Tanga nami nilikwenda hadi Radio kuomba nipatiwe hayo mazungumzo yake lakini Radio Nuur waliogopa kunipa juu ya kuwaeleza kuwa Bi. Chiku kazungumza radioni kwa hiyo kazungumza na dunia nzima.

Hawakuthubutu kunipa lakini nilizungumza na watu waliomsikia.

Katika Waislam waliokamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani Handeni ni huyu kijana Rajab Omari Mtana.

Baada ya kukaa rumande alipata dhamana yeye pamoja na wenzake na akawa nje.

Mwezi uliopita Rajab Omar Mtana alirejea kijijini kwake.

Wakati anakaribia kuingia kijijini alisimamishwa na askari wa kijiji akapekuliwa na akanyang'anywa simu yake na fedha taslimu.

Baada ya mkasa huu walimwachia na yeye akaendelea na safari yake.
Lakini nyumba yake ilikuwa imevurugwa haifai kuishi mtu kwa hiyo alifikia kwa dada yake.

Akiwa nyumbani kwa dada yake alifatwa na watu wa serikali ya kijiji usiku akatolewa ndani na kuanza kupigwa kwa bakora na kisha kwa mapanga.

Kujitetea kijana huyu alikimbia huku akifukuzwa.
Asubuhi kulipokucha palionekana damu nyingi sana.

Taarifa ilitolewa polisi lakini hakuna kilichofanyika.

Polisi walitoa taarifa (SON/RB346/2014) Dada yake na mumewe walikamatwa na kushitakiwa katika ''mahakama'' ya hapo kijiji na wakapigwa faini ya kila mtu shs. 20.000.

Kosa lao ni kumleta kijijini mtu asiyetakiwa.

Sasa ni mwezi mmoja Rajab Omar Mtana hajulikani alipo na inasadikiwa ameuawa na wale waliokuja kumtoa nyumbani kwa dada yake.

Ndugu yetu Rajab ametafutwa kote hadi leo hajapatikana na waliompiga na kumjeruhi wako huru nje hawajaguswa wala kuhojiwa na polisi.

Wakati Sheikh Chambuso alipokuwa akinihadithia mkasa huu ilinijia picha ya kisa cha vijana watatu waliouliwa na Klu Klux Klan Mississippi katika miaka wa 1960 wakati wa ubaguzi wa rangi Marekani.

Waliuliwa kama vile mtu kauwa paka msumbufu na hakuna lolote lililofanyika hadi zilipotiwa juhudi za ziada kutoka nje ya Mississippi ndipo wauaji wakatiwa mbaroni.

Mauaji ya Madina yamepita hivi hivi hakuna aliyesimamishwa mbele ya vyombo vya dola.

Uwezekano mkubwa ni kuwa na mauaji haya yatafata mkondo ule ule. Jambo la kusikitisha ni kuwa mauaji haya yamelenga watu wa dini moja.

Je, viongozi wetu wako hadhiri na mbegu hii wanayoiacha imee?

Hatari hizi zote hawa watu wanagoma kuzipokea kwa sababu ya chuki zao tu.Lakini wakati utafika na kila kitu kitakuwa wazi.
 
Umekuwa kimya maana tukiuliza maswali unajibu kwa picha.
Mtoa mada ukienda kinyume nae Hana majibu.
Ila stori kama hizi ndo ulikuwa unazihitaj.Enjoy now

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
Day ...
Najitahidi kujibu kila swali na picha naweka kukazia maelezo.

Kwani picha inasema maneno 1000.
Wasomaji wengi nimewavutia kwa ajili ya hii Maktaba yangu ya picha .

Waingereza wana msemo, "Seeing is believing."
Kuona ndiyo kuamini.
 
Dah huyu mzee mwanzoni nilimchukulia Kama mtu mwenye elimu kubwa ya historia ya nchi lkn nadhani nilikosea. Ni mtu mwenye maarifa mengi ya UDINI Kila anachokiandika ni kulialia tu mwingine ni FaizaFoxy Hawa watu mh Kama ni dini Basi wameipokea vibaya. Bahati nzuri watanzania waislamu kwa wasio waislamu, wakristo kwa wasio wakristo hawana muda na UDINI lkn wako busy na DINI zao
Yamekuingia. Ukweli siku zote huwa mchungu.

Dini yake, wewe inakuhusu nini hata uumie?
 
Sis tunaijuwa, Nyerere/TANU ilileta uhuru. Abdul Sykes hakuwa Mtanganyika bali mtu wa Afrika Kusini. Hili wewe hutuambii. Kama ulikuwa hujui pata hiii ilmu toka kwangu. Picha hazielezi lolote zaidi na unavyozitafsiri. Piacha siyo prpoof kuwa hao walileta uhuru. Kama walikuwa serious kwa nini wakamwachia Nyerere. Kumbuka kudai uhuru ni siasa na siasa ni ushindani. Nyere alishindani nao aklawatolea mbali. Alikuwa na uwezo unaotakiwa na ndiyo maana ndiye alieonekana anafaa. Abdul Sykes aache kupigania uhuru wa kwao South Africa aje kupigania wa TZ. Kwanza wakoloni wangemtolea uvivu na ndiyo kwanza miaka ya kupata uhuru ingesogea mbele.
Ni kenge mwenye roho ya kibaguzi kama wewe unaumia mpaka leo unapoona ni wahindi na waarabu ndio wenye hela nchi hii, lakini hujui pia ndio wapo waliomchangia huyo Nyerere katika pilika zake za kudai uhuru.
Zee zima mvi mpaka utopoloni, lakini bado akili ya kibaguzi kuona hata wale waliojitolea kudai uhuru hawastahili kuwa watanzania kwa kuwa wana asili ya afrika kusini...Kenge wewe endelea kula kipensheni chako za CCM ambacho hata hakitoshelezi kwenda choo kila siku....
 
Yani rais akishakuwa muislam hizi mada za kijingajinga huwa zinakuwa nyingi sana. Akili mnaweka wapi? embu kafanye kazi acha kulalama vitu vya kusadikika. Umaskini na ujinga wako unao mwenyewe na uwezo wa kuutoa ni wewe mwenyewe na sio dini wala imani yako. Over.


Ukishasikiliza mazungumzo ya Mwalimu Nyerere katika hiyo video hapo juu sasa soma Hotuba yake aliyotoa Bungeni tarehe 10 Desemba, wakati Tanganyika inakua jamuhuri mwaka wa 1962.

Hotuba ya Nyerere ilijikita kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo.

Kwa nini ilikuwa lazima Mwalimu awataje Waislam katika hotuba ile?

Sababu ni jinsi Waislam walivyokuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukoloni na namna walivyounda TANU wakamchagua kama kiongozi na kuumuunga mkono toka siku alipochukua uongozi wa TAA katika uchaguzi wa tarehe 17 April, 1953 Ukumbi wa Arnautoglo alipogombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes aliyekuwa Act. President na Secretary wa TAA.

Kwa bahati mbaya sana hii ni historia ambayo ilifunikwa na hakuna yeyote aliyekuwa anaijua hadi nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kuchapwa mwaka wa 1998.

Mwalimu anasema katika hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika:

''Hakuna njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika; hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na Wachagga na Wanyakyusa.''

Hii ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema ya kupigania haki na usawa kwa raia wote wa Tanganyika.

Kauli hii ilikuwa ya kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua zifaazo kurekebisha hali hiyo.

Tarehe 5 Novemba, 1985 wakati Mwalimu anastaafu urais, Mwalimu aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam.

Hotuba hii ilijaa simanzi, Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo.

Katika hotuba hii Nyerere kwa mar ya kwanza hadharani alimtaja Abdul Sykes.

Mwalimu alimtaja na mdogo wake Abdul, Abbas Sykes na Dossa Aziz.

Wazee hawa aliokuwa anawahutubia wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru.

Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru.

Nyerere alisema neno zito sana kuwa upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake:

''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo.

Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho.

Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo.

Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''

Swali linalokuja hapa ni kuwa ikiwa Mwalimu alisharekebisha upogo huu baina ya Waislam na Wakristo haya malalamiko ya leo kutoka kwa Waislam kuwa wanabaguliwa tunauelezaje?

Waislam hawasemi kweli?

Mgawano wa madaraka ndani ya serikali ya Tanzania baina ya Waislam na Wakristo ni 20:80.

Tumefikaje katika hali hii?

Ni muhimu sana mtu anapotaka kujadili tatizo hili la udini muhimu akaangalia historia hii kwanza kama nilivyoieleza hapo juu kwa kusikiliza mazungumza ya Mwalimu kuhusu udini na kusoma Hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika mwaka wa 1962.

Tatizo hili la udini nimelijadili kwa kirefu sana katika kitabu cha Abdul Sykes.

Tatizo hili si tatizo la kupuuzwa na wala si la leo.

Tatizo hili lilianza mwaka wa 1958 na likasababisha ugomvi mkubwa baina ya Sheikh Suleiman Takadir na Julius Nyerere na Sheikh Suleiman Takadir akafukuzwa TANU.

View attachment 2096477
View attachment 2096478
 
Pale tunapoacha vigezo vya msingi katika utendaji na kukimbilia dini tunaenda kuua taifa. Nchi yetu haina dini, bali watu wake. Imani, kwa maana yoyote ile, isiwe kigezo cha utumishi kwenye taifa. Kwa muktadha huu, tusiache kujadili ndugu zetu wa-hindu, hawa tumewabagua zaidi. Mwisho, mzee wangu imani ya dini ni chombo cha kumsaidia binadamu ili amfikie Mungu wake, sasa wewe unataka kutumia imani kustahilisha mambo ya kidunia. Embu, tafakari malengo mahususi ya imani yako alafu utathmini fikra zako katika hicho unachodhani ni elimu unayoitoa.
 
Pale tunapoacha vigezo vya msingi katika utendaji na kukimbilia dini tunaenda kuua taifa. Nchi yetu haina dini, bali watu wake. Imani, kwa maana yoyote ile, isiwe kigezo cha utumishi kwenye taifa. Kwa muktadha huu, tusiache kujadili ndugu zetu wa-hindu, hawa tumewabagua zaidi. Mwisho, mzee wangu imani ya dini ni chombo cha kumsaidia binadamu ili amfikie Mungu wake, sasa wewe unataka kutumia imani kustahilisha mambo ya kidunia. Embu, tafakari malengo mahususi ya imani yako alafu utathmini fikra zako katika hicho unachodhani ni elimu unayoitoa.
Mixo...
Hii ni makala yangu ya tatu.
Naamini umezisoma mbili zilizotangulia.

Haya mambo yanetokea miaka 9 iliyopita:

MADINA YAKATAZWA KUWA SEHEMU YA MAKAZI KWA AMRI YA MKUU WA MKOA TANGA CHIKU GALAWA a

Nyaraka zimefika Dar es Salaam zinazoonyesha kuwa wakazi wa Madina kijiji kilichovamiwa kwa kisingizio kuwa kilikuwa na uhusiano na Al Shabab wamelazimishwa kuweka sahihi makubaliano kati yao na uongozi wa kata ya Negero kuhama eneo hilo kwa kuwa haparuhusiwi kuishi watu.

Kutokana na nyaraka hizo amri hiyo imetoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa.

Nyaraka inaonyesha kuwa waliotilishwa sahihi amri hiyo ya kuondoshwa Madina ni Muhamadi Mwandalo na Salimu Mwalimu na viongozi waliotia sahihi kwa niaba ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Negero ni Paul A. Mnyeke na Ramadhani A. Mwamilinga.

Nyaraka ina muhuri wa Afisa Mtendaji Kata Negero.

Makubaliano hayo yanasema wanakijiji hao wamepewa siku 10 kuishi Madina kuanzia tarehe 19 hadi 24 Desemba 2013 wawe wameshaondoka Madina na wamevunja nyumba zao na kuondoa vifaa vyao.

Makubaliano hayo yanataka nyumba ziwe zimevunjwa ingawa nyumba zilishavunjwa siku nyingi na vifaa vya wanakijiji hao kupotea katika uvamizi ule.

Makubaliano hayo nyaraka inaonesha yalifanywa tarehe 17 Desemba 2013.
Manazi wa Kijerumani waliwafanyia dhulma mfano wa hii Wayahudi wakati wa Vita Kuu Vya Dunia.

Wanasheria wanaweza kusaidia katika dhulma hii.
Kuna wanavijiji waliondoka Madina zamani kwa sababu mbalimbali.

Kijiji kiliposhambuliwa na kesi kufunguliwa dhidi ya Waislam Mahakama ya Handeni wakazi hawa waliohama walikuwa kimya na walipozungumza walitoa picha iliyokuwa wakati mwingine inamtisha msikilizaji.

Taratibu baada ya kusikia kuwa nyumba zimevunjwa na kuchoma moto na ardhi zao sasa wananyang'anywa wameanza kuhaha kutaka kujua kulikoni.

Wanazungumza kuhusu mali zao na mashamba yao na viwanja vyao na ardhi zao.

Kubwa sana na hili wengi hawakuwa wanalijua wanazungumza kuhusu machimbo ya dhahabu huko Madina...waliyokuwa wakimiliki kihalali na nyaraza za umiliki wanazo...

Halikadhalika tumepokea hapa ujumbe mkali kuwa hawa Waislam wa Madina hawastahili kuhurumiwa na kutetewa...

Jibu limekuwa wanastahili kuhurumiwa na kutetewa kwani hata kama tujaaliwe walikuwa katika makosa hapakuwa na sababu ya kuuliwa na nyumba na misikiti yao kuchomwa moto.

Ilikuwa hawa ''wakosaji'' wakamatwe wapelekwe mahakamani.

Anaetaka kujua zaidi kuhusu hili na atembelee Ubao.

Ukurasa huu uko wazi kusikiliza yanayoanza kujitokeza kutoka Madina.
 
Historia ya nchi hii inatakiwa itazamwe upya kwa nia ya kuondoa upotoshaji mwingi uliyopo ambao umepelekea watu wengi waliopigania uhuru wa Tanganyika kutokujulikana.
 
Historia ya nchi hii inatakiwa itazamwe upya kwa nia ya kuondoa upotoshaji mwingi uliyopo ambao umepelekea watu wengi waliopigania uhuru wa Tanganyika kutokujulikana.
Imeloa,
Kilipotoka kitabu cha Abdul Sykes mwaka wa 1998 kila aliyekisoma alishangazwa na aliyoyakuta ndani.

Kitabu kimependwa sana kwani watu walikuwa wanaisoma upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
 
Imeloa,
Kilipotoka kitabu cha Abdul Sykes mwaka wa 1998 kila aliyekisoma alishangazwa na aliyoyakuta ndani.

Kitabu kimependwa sana kwani watu walikuwa wanaisoma upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
Hii tabia ya kupotosha mambo muhimu ya nchi inafanywa na Ccm kwa lengo la kuwapa sifa za uongo viongozi wao wa juu hasa yule anayeshika mamlaka ya urais.

Tulipoanza shule mwanzoni kabisa ya miaka ya sabini tulikaririshwa mashuleni kwamba Nyerere ndiye aliyeleta uhuru na watu walifanywa wamwabudu kabisa kama vile asingekuwepo Tanganyika isingepata huo uhuru.

Kumbe swala la uhuru ni mkakati ulioanzishwa wakati huyo Nyerere akiwa bado mtoto mdogo kabisa na yeye alikuja tu kudandia train ya uhuru baadaye sana jambo ambalo limefanywa siri na watawala.

Historia ya Tanganyika na baadaye Tanzania inatakiwa iandikwe upya kwa kuzingatia ukweli na kuachana na propaganda na porojo zisizo na maana zinazolenga kuwapa watu wengine sifa wasiostahili.
 
Mount...
Umeanza kuandika na "Wewe..." dalili ya ghadhabu.
Naam umri wangu wote nimetafiti historia ya Waislam wa Tanganyika

Sababu ni kuwa hapakuwa na msomi aliyetaka kuandika historia yao.

Kimambo na Temu (1969) wameandika historia ya uhuru Waislam ambao ndiyo walikuwa mstari wa mbele hawamo.

Leo mimi nimeandika upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Huijui historia ya Misri.
Zungumza unachokijua.

Nchi zenye Waislam wengi hakuna wapagani.
Jifunze utafahamu.

Soma "In Search of Identity," tawasifu ya Anwar Sadat utajua nani wanaongoza serikali ya Misri.

Soma "The Road to Ramadan," cha Mohamed Heykal utaijua Misri na walioko madarakani.

Dini ni muhimu kupita kiasi katika kutawala nchi yenye dini kubwa mbili.
Ukiachia serikali itawaliwe na watu wa imani moja utasababisha farka na fitna katika jamii.

Hutoweza kujenga umoja na amani ya kweli nchini.

View attachment 2097635
Niko Alexandria, Egypt 1988.
hii hapa kitaalam inaitwa akili kubwa kuijibu akil ndogo. Mzee yan nakuelewa sana yan huo mwaka upo Egypt weng wapo mikoan kwao mwenye gar ni mkuu wa mkoa na waarabu na wahind wachache enz za Bedford
asome vitab hivyo ataelewa???
mzee wangu anaenda gulf Oman mwaka 1990 karibu kata nzima ilijua na barua tu sim ghali enzi hizo.
nikirithi magazet ya sani, vitabu vya Joram Kiango Msako wa Jambazi
Star wars, The ThirdReich,James HadleyChase,
Ustadh una nondo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mount...
Umeanza kuandika na "Wewe..." dalili ya ghadhabu.
Naam umri wangu wote nimetafiti historia ya Waislam wa Tanganyika

Sababu ni kuwa hapakuwa na msomi aliyetaka kuandika historia yao.

Kimambo na Temu (1969) wameandika historia ya uhuru Waislam ambao ndiyo walikuwa mstari wa mbele hawamo.

Leo mimi nimeandika upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Huijui historia ya Misri.
Zungumza unachokijua.

Nchi zenye Waislam wengi hakuna wapagani.
Jifunze utafahamu.

Soma "In Search of Identity," tawasifu ya Anwar Sadat utajua nani wanaongoza serikali ya Misri.

Soma "The Road to Ramadan," cha Mohamed Heykal utaijua Misri na walioko madarakani.

Dini ni muhimu kupita kiasi katika kutawala nchi yenye dini kubwa mbili.
Ukiachia serikali itawaliwe na watu wa imani moja utasababisha farka na fitna katika jamii.

Hutoweza kujenga umoja na amani ya kweli nchini.

View attachment 2097635
Niko Alexandria, Egypt 1988.
Mkuu una uwezo mkubwa ktk kujenga hoja,hapo nakupa saluti kuubwa.Ushauri wangu jikite kwenye weledi achana na mambo ya kuangalia ktk mitizamo ya kidini.Unakoelekea sasa utaanza kuhoji hata timu ya taifa ina waislam wangapi badala ya kuangalia uwezo,maadili,maarifa...Kama ulivyonishauri niachane na mambo ya Misri basi hebu nawe jiulize ni wakristo wangapi waliopo serikalini kwenye teuzi SMZ?Kwani uliambiwa teuzi zinafanyika ktk misingi ya uwiano kidini?Mbona hujawai kuhoji kwanini waislam wana vyuo na shule chache?
 
Mzee wangu naomba kujua tu kwamba ikiwa kutakuwa na balance baina ya idadi ya waislamu na wakristo katika wizara fulani hilo jambo lina faida gani kwa waislamu ?

Mfano waziri wa mambo ya ndani kwa sasa ni muislamu,je waislamu wamefaidika vipi na huyu mtu kuwa waziri ?
Hata mi nashangaa sana, siyo lazima nduguzanguni waislamu muajiliwe serikalini, ,kazi zipo nyingi sana, kilimo, ujenzi majumba, barabara,
Hata mpira kucheza nayo kazi nduguzanguni
 
Asante ningependa sana kupata majibu ya hoja zangu kwa sababu sijauliza ili nisifiwe bali nimeuliza ili nijibiwe

Nina imani nitajifunza tu kwenye majawabu yako mzee wangu
Political marginalization means that some groups of people are not able to PARTICIPATE democratically in the DECISIONS MAKING PROCESS
 
Mkuu una uwezo mkubwa ktk kujenga hoja,hapo nakupa saluti kuubwa.Ushauri wangu jikite kwenye weledi achana na mambo ya kuangalia ktk mitizamo ya kidini.Unakoelekea sasa utaanza kuhoji hata timu ya taifa ina waislam wangapi badala ya kuangalia uwezo,maadili,maarifa...Kama ulivyonishauri niachane na mambo ya Misri basi hebu nawe jiulize ni wakristo wangapi waliopo serikalini kwenye teuzi SMZ?Kwani uliambiwa teuzi zinafanyika ktk misingi ya uwiano kidini?Mbona hujawai kuhoji kwanini waislam wana vyuo na shule chache?

KUKATOKEA MALALAMIKO KUWA ZOEZI HILO LINA SURA YA UBAGUZI NA WAATHIRIKA NI WAISLAM

Nayakumbuka mambo matatu kama mifano mnasaba wa uzi huu:

1. Bodi Taifa ya Parole hapa nchini iliteuliwa na Frederick Tluway Sumaye aliyekua Waziri Mkuu wakati wa Urais wa Marehemu Benjamin Mkapa.

Sumaye aliteuwa wajumbe wote wa bodi wa imani moja bika kuwepo Muislam hata mmoja.

Miongoni mwao walikuwepo padri mmoja na mchungaji mmoja.

Alipoulizwa kwa nini kafanya hivyo akajibu kwa ukali sana kwamba watu waache kupanda mbegu za udini maana hatukukelewa hivyo na Mwalimu Nyerere.

Uteuzi uliofanyika ulizingatia ''merits,'' za walioteuliwa.

Siku chache baadae Marehemu Mzee Mkapa akatengua uteuzi wa bodi nzima na akaagiza iundwe upya kwa kuzingatia uwiano wa kijamii kama maeneo wanapotoka wajumbe na pia uwiano wa imani za watu kwa maana ya dini.

2. Professor mmoja wa UDOM aliyekua VC alipata malalamiko kuhusu baadhi ya watu kutotendewa haki kwenye ''admission.''

Wakati huo TCU ilikua haijaundwa.

Alipoamua kuitisha ''applications'' zote akakutana na maajabu. Kuna zaidi ya ''applicants'' 350 walikua wameachwa huku wakiwa wame ''qualify'' huku kukiwa na idadi ya kutosha kabisa wakiwa wamepata ''admission'' wengine wakiwa ''below cut-off point'' ya chuo.

Kwa “sudfa” au ''coincidence'' wote waliokua wameachwa kwa dhulma walikua na majina ya Kiislamu na wote walioku ''admitted'' walikua na majina ya Kikristo.

VC akatoa ''order'' mchakato urudiwe tena japo jambo hilo lilikua ''down played.''

3. Miaka ya karibuni kulikua na zoezi la kuwaondoa waalimu wa masomo ya arts sekondari waajiriwa wa serikali kuwarudisha shule za msingi. Zoezi husika halikuwahusu waalimu wa masomo ya sayansi na hesabu

Nilikua mkoa fulani kipindi zoezi hili linaendelea.

Kukatokea malalamiko kua zoezi hilo lina sura ya ubaguzi na waathirika ni Waislamu.

Ofisa mmoja Muislamu katika idara ya elimu ambaye hapo awali alikua amejaribu kuomba uhamisho kwenda mkoa mwingine kwa zaidi ya miaka miwili bila mafanikio alipokea malalamiko hayo na baada ya kujiridhisha ni ''genuine'' akayapeleka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri.

Kikaitwa kikao kati ya Mkurugenzi, Afisa Elimu, Afisa Elimu Taaluma, Ofisa Utumishi na yule ofisa aliyeipeleka ''issue'' kwa Mkurugenzi.

Wahusika wote kasoro yule aliyepeleka malalamiko walikua Wakristo na ilivyoonekana baada ya kikao kuanza ni kutaka kum ''pin'' huyo ofisa kwa nini analeta udini kwenye utendaji wa kazi za Halmashauri na hususan hilo zoezi la kitaifa.

Walianza kumpa maneno makali kabda hata hawajamuuliza kuhusu ushahidi.
Walipomuuliza atoe ushahidi wa madai yake akaoonyesha majina wa wahusika waliohamishwa.

Shule ina waalimu 68 kati yao Waislamu 18.
Waalimu wanaotakiwa kupelekwa primary schools ni 21.

Basi wakaondolewa wale wote 18 wenye majina ya Kiislamu na hao wengine 3 wasiokua Waislamu.

Kikao bado kikasema huo sio ushahidi maana Mkuu wa Kituo (Headmaster) ana ''discretion'' ya kuchagua mradi anafata ''secular'' iliyotolewa na Wizara (TAMISEMI).

Ndipo akaangusha bomu la''Atomic'' ambalo alikua hajawaambia ''before. Kwamba katika wale waalimu Waislamu 18 watatu ni wa Mathematics na sita ni wa masomo mengine ya sayansi na akawaonyesha.

Kikao hakikuendelea.

Mkurugenzi akamwambia Afisa Elimu akarekebishe hilo tatizo.

Wiki hiyo hiyo yule Afisa akapata barua ya uhamisho aliouomba kwa miaka miwili bila mafanikio.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom