Baba wa Taifa na tatizo la Udini

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,887
30,233


Ukishasikiliza mazungumzo ya Mwalimu Nyerere katika hiyo video hapo juu sasa soma Hotuba yake aliyotoa Bungeni tarehe 10 Desemba, wakati Tanganyika inakua jamuhuri mwaka wa 1962.

Hotuba ya Nyerere ilijikita kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo.

Kwa nini ilikuwa lazima Mwalimu awataje Waislam katika hotuba ile?

Sababu ni jinsi Waislam walivyokuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukoloni na namna walivyounda TANU wakamchagua kama kiongozi na kuumuunga mkono toka siku alipochukua uongozi wa TAA katika uchaguzi wa tarehe 17 April, 1953 Ukumbi wa Arnautoglo alipogombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes aliyekuwa Act. President na Secretary wa TAA.

Kwa bahati mbaya sana hii ni historia ambayo ilifunikwa na hakuna yeyote aliyekuwa anaijua hadi nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kuchapwa mwaka wa 1998.

Mwalimu anasema katika hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika:

''Hakuna njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika; hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na Wachagga na Wanyakyusa.''

Hii ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema ya kupigania haki na usawa kwa raia wote wa Tanganyika.

Kauli hii ilikuwa ya kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua zifaazo kurekebisha hali hiyo.

Tarehe 5 Novemba, 1985 wakati Mwalimu anastaafu urais, Mwalimu aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam.

Hotuba hii ilijaa simanzi, Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo.

Katika hotuba hii Nyerere kwa mar ya kwanza hadharani alimtaja Abdul Sykes.

Mwalimu alimtaja na mdogo wake Abdul, Abbas Sykes na Dossa Aziz.

Wazee hawa aliokuwa anawahutubia wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru.

Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru.

Nyerere alisema neno zito sana kuwa upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake:

''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo.

Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho.

Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo.

Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''

Swali linalokuja hapa ni kuwa ikiwa Mwalimu alisharekebisha upogo huu baina ya Waislam na Wakristo haya malalamiko ya leo kutoka kwa Waislam kuwa wanabaguliwa tunauelezaje?

Waislam hawasemi kweli?

Mgawano wa madaraka ndani ya serikali ya Tanzania baina ya Waislam na Wakristo ni 20:80.

Tumefikaje katika hali hii?

Ni muhimu sana mtu anapotaka kujadili tatizo hili la udini muhimu akaangalia historia hii kwanza kama nilivyoieleza hapo juu kwa kusikiliza mazungumza ya Mwalimu kuhusu udini na kusoma Hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika mwaka wa 1962.

Tatizo hili la udini nimelijadili kwa kirefu sana katika kitabu cha Abdul Sykes.

Tatizo hili si tatizo la kupuuzwa na wala si la leo.

Tatizo hili lilianza mwaka wa 1958 na likasababisha ugomvi mkubwa baina ya Sheikh Suleiman Takadir na Julius Nyerere na Sheikh Suleiman Takadir akafukuzwa TANU.

1643208364377.png

1643208426446.png
 
Mwalimu anaweza akawa aliwahi kuwa na madhaifu kadhaa kama mwanadamu yeyote, lakini.....the man was genius.

It is mindblowing how he could make all those strong points spontaneously and without having a desa to peruse.

Aendelee kupumzika kwa amani.

Tunamshkuru kwa misingi mizuri aliyoiweka katika taifa,

Japo tumeona ubaguzi mkubwa sana recently, especially katika vyama vya siasa.
 
Pep,
Mwalimu angeacha misingi mizuri leo tusingejikuta kwanza tunaandika upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Pili tusingekuwa na mjadala huu uliotukutanisha hapa.
Mzee wangu, Mo

Naishi Tanzania sasa kwa zaidi ya miaka 30.

Katika kipindi hiki nimekua, nimesoma, nimetafuta kazi na nimefanya kazi na WATANZANIA.

Katika watanzania hawa, walikuwepo makabila tofauti na ya kwangu, dini tofauti na yangu.

Mpaka sasa hivi naandika, sijawahi kubaguliwa ama kumbagua mtu kwa dini yake.

Sijawahi kubaguliwa, wala mimi sijawahi kumbagua mtu kwa kabila lake.

Ni tofauti sana na hapo Kenya tu kwa mfano ambapo watu wanabaguliwa kwa makabila hadi leo.

Au ni tofauti sana na pale Nigeria (moja kati ya taifa elite kabisa Africa) ambapo wakristo na waislam wanabaguana kila leo.

Wanachomeana makanisa na misikiti.

Kwa hili, Baba wa taifa Mwl J.K Nyerere abarikiwe sana.

Mungu aendelee kumpa pumziko la milele.

He was one in a million
 
Mzee wangu, Mo

Naishi Tanzania sasa kwa zaidi ya miaka 30.

Katika kipindi hiki nimekua, nimesoma, nimetafuta kazi na nimefanya kazi na WATANZANIA.

Katika watanzania hawa, walikuwepo makabila tofauti na ya kwangu, dini tofauti na yangu.

Mpaka sasa hivi naandika, sijawahi kubaguliwa ama kumbagua mtu kwa dini yake.

Sijawahi kubaguliwa, wala mimi sijawahi kumbagua mtu kwa kabila lake.

Ni tofauti sana na hapo Kenya tu kwa mfano ambapo watu wanabaguliwa kwa makabila hadi leo.

Au ni tofauti sana na pale Nigeria (moja kati ya taifa elite kabisa Africa) ambapo wakristo na waislam wanabaguana kila leo.

Wanachomeana makanisa na misikiti.

Kwa hili, Baba wa taifa Mwl J.K Nyerere abarikiwe sana.

Mungu aendelee kumpa pumziko la milele.

He was one in a million
Pep,
Unayosema huenda ni kweli kabisa kuwa hujabaguliwa na wewe hujabagua mtu.

Muulize Mmarekani Mweupe kama yeye keshabaguliwa atakwambia bado sijabaguliwa na pengine atakuambia yeye hajabagua mtu.

Sasa nakuuliza je wewe uko katika kundi la wanaobaguliwa na hukubaguliwa?
Mbona unakwenda mbali sana Nigeria kutafuta mifano ya ubaguzi?

Vipi hali ya hapa ulikoishi kwa miaka 30?
Hali ikoje?

Nakusihi kwa ajili ya heshima yake tumwache Mwalimu tusimwingize katika huu mjadala wa mimi na wewe.

Huenda ikawa wewe hujui uhusiano wa wazee wangu na Mwalimu na historia yao wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wazee wangu ndiyo waliompokea Mwalimu Dar es Salaam 1952 na kuunda TANU 1954 kutoka African Association waliyoasisi 1929.

Historia hii nimeaindika, iko na inasomwa.

Naijua historia ya Mwalimu vizuri sana kiasi mimi ni mmoja wa watu waliohojiwa wakati inaandikwa historia ya Julius Nyerere na jopo la waandishi wa historia hii waliisifia Maktaba yangu kuwa moja ya maktaba kubwa tatu zilizo na taarifa za Mwalimu; maktaba ya Salim Ahmed Salim, Brigadier General Hashim Mbita na ya Mohamed Said.
1643221663793.png



1643214732565.png

Kulia ni Prof. Issa Shivji, Prof. Said Yahya Othman na Dr.
Ng'waza Kamata walipokuja kunihoji kuhusu Mwalimu.
 
Pep,
Unayosema huenda ni kweli kabisa kuwa hujabaguliwa na wewe hujabagua mtu.

Muulize Mmarekani Mweupe kama yeye keshabaguliwa atakwambia bado sijabaguliwa na pengine atakuambia yeye hajabagua mtu.

Sasa nakuuliza je wewe uko katika kundi la wanaobaguliwa na hukubaguliwa?
Mbona unakwenda mbali sana Nigeria kutafuta mifano ya ubaguzi?

Vipi hali ya hapa ulikoishi kwa miaka 30?
Hali ikoje?

Nakusihi kwa ajili ya heshima yake tumwache Mwalimu tusimwingize katika huu mjadala wa mimi na wewe.

Huenda ikawa wewe hujui uhusiano wa wazee wangu na Mwalimu na historia yao wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wazee wangu ndiyo waliompokea Mwalimu Dar es Salaam 1952 na kuunda TANU 1954 kutoka African Association waliyoasisi 1929.

Historia hii nimeaindika, iko na inasomwa.

Naijua historia ya Mwalimu vizuri sana kiasi mimi ni moja wa watu waliohojiwa wakati inaandikwa historia ya Julius Nyerere na jopo la waandishi wa historia hii waliisifia Maktaba yangu kuwa moja ya maktaba kubwa tatu zilizo na taarifa za Mwalimu; maktaba ya Salim Ahmed Salim, Brigadier General Hashim Mbita na ya Mohamed Said.

View attachment 2096546
Kulia ni Prof. Issa Shivji, Prof. Said Yahya Othman na Dr.
Ng'waza Kamata walipokuja kunihoji kuhusu Mwalimu.
Okay mzee, Mohamed

Nadhani tuyaache kama ulivyoshauri.

Kama nilivyosema awali, inawezekana hayati alikua na mapungufu mengi tu (kama sisi wote)

Lakini hata kama ni kwa uchache.....alituunganisha sana.

Inawezekana hapa kwetu upo ubaguzi, sikupingi....ila nimetolea mfano Nigeria ambap kule ubaguzi ni wazi wazi.

Kila mtu anaona, na anajua namna wale jamaa wanapeana joto ya jiwe
 
Ishu ya sheikh takadir na mwl. Nyerere marehemu sheikh ilunga aliizungumzia vizuri kabisa.
Makaveli...
Kisa chote kipo katika kitabu cha Abdul Sykes.
Watu wengi niliowaendea kuhusu historia ya Sheikh Suleiman Takadir waliogopa kunieleza.

Mtu aliyekubali kunipa historia ya Sheikh Takadir ni Mzee Haydar Mwinyimvua aliyekuwa rafiki yake kipenzi.

1643215140491.png

Kaburi la Sheikh Haydar Mwinyimvua
1643215070782.png

Sheikh Haydar Mwinyimvua Khatibu
 
Wakristu wao wanapambania haki ya Kabila, matambiko, Uchief, utemi wenzao Waislamu wanapigania Uislamu.
Mmeshapoteza hii game, soon or later mtajua, kwa maana hata wealth hamna pia, wealthy people Tanzania mnawajua !
 
Okay mzee, Mohamed

Nadhani tuyaache kama ulivyoshauri.

Kama nilivyosema awali, inawezekana hayati alikua na mapungufu mengi tu (kama sisi wote)

Lakini hata kama ni kwa uchache.....alituunganisha sana.

Inawezekana hapa kwetu upo ubaguzi, sikupingi....ila nimetolea mfano Nigeria ambap kule ubaguzi ni wazi wazi.

Kila mtu anaona, na anajua namna wale jamaa wanapeana joto ya jiwe
Pep,
Usikae mbali na mimi.
Nina mengi sana katika historia ya Waislam wa Tanganyika.

Nimekuwa nikitafiti na kuandika toka niko kijana mdogo sana labda wa 20s.
 
Pep,
Usikae mbali na mimi.
Nina mengi sana katika historia ya Waislam wa Tanganyika.

Nimekuwa nikitafiti na kuandika toka niko kijana mdogo sana labda wa 20s.
Ahsante mzee wangu.

Nimeketi kitako
 
Wakristu wao wanapambania haki ya Kabila, matambiko, Uchief, utemi wenzao Waislamu wanapigania Uislamu.
Mmeshapoteza hii game, soon or later mtajua.
Kijakazi,
Waislam hatuna ujinga huo wa kupambania dini yetu katika jumuiya hii ya watu wa dini tofauti.

Laiti wazee wetu wangefuata njia hiyo Mwalimu asingekuwa kiongozi wa nchi hii.

Tunachokipigani ni haki na usawa.
Angalia picha hii na hawa ni akina mama mwaka wa 1955:







1643215555773.png
 
Ahsante mzee wangu.

Nimeketi kitako
Pep,
Nakuhakikishia hutajuta.

Niulize swali lolote kuhusu harakati za uhuru kuanzia 1929 wazee wangu walipounda African Association hadi uhuru 1961 na changamoto zlizotokea kupelekea wazee wangu wote kufutwa katika historia hii.
 
Makaveli...
Kisa chote kipo katika kitabu cha Abdul Sykes.
Watu wengi niliowaendea kuhusu historia ya Sheikh Suleiman Takadir waliogopa kunieleza.

Mtu aliyekubali kunipa historia ya Sheikh Takadir ni Mzee Haydar Mwinyimvua aliyekuwa rafiki yake kipenzi.

View attachment 2096558
Kaburi la Sheikh Haydar Mwinyimvua
View attachment 2096557
Sheikh Haydar Mwinyimvua Khatibu
Nahitaji hiki kitabu mzee wangu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom