Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Hatuna budi kumshukuru Aliye Juu kwa uumbaji wake wa kushangaza ambao majira haya ya kiangazi yanaufunua kwa namna ya ajabu na ya kutisha. Tumshukuru kwa kutupa macho ya kuweza kushuhudia uumbaji huo na mioyo ya kufurahia kazi yake isiyo na mfano. Hivyo popote pale ulipo tumia sala au dua hii kumshukuru Mungu.
"Ee Mola uliye mwingi wa fadhili na rehema
Mkuu usiye na mfano wala usiye na mshirika
Unayetoa yale yote yaliyo mema
Na kuwajaza watu wako baraka
Ninakushukuru kwa uumbaji wako
Kwa viumbe viendavyo kwa maringo na mapozi
Viumbe ambavyo pasipo hivyo ulimwengu huu hakika ungekuwa sana na Jehanum!
Tunashukuru kwani katika uumbaji wako
Tunaona ukuu wa upendo wako kwetu.
Tunaomba uwabariki viumbe vyako hawa
Si kwa baraka zile za Kichina
Bali kwa baraka za Kijamaika na Brazili!
Na zile za kwetu za Kimakonde!
Na utuwezeshe sisi tunaofurahia uumbaji huo
Kuzidi kukaa macho bila kupepesa
Ili tusipitwe na lolote na tukalikosa!
Na tunawaonea huruma wale wanaoishi kwenye nchi ambazo uumbaji wako
Si rahisi kuonekana namna hiyo!
Ila tunaomba sana tena chonde chonde.. hata tukiingia majaribuni usitutoe mapema
Ila kwahakika usituache tuzame huko na kujisahau
Ila kama ulivyomfanyia Yona/Yunus yule nabii nasi hatimaye uturudishe kwenye nchi kavu!"
Na watu wote wasema AMEN, aMINA, AMEEN!
"Ee Mola uliye mwingi wa fadhili na rehema
Mkuu usiye na mfano wala usiye na mshirika
Unayetoa yale yote yaliyo mema
Na kuwajaza watu wako baraka
Ninakushukuru kwa uumbaji wako
Kwa viumbe viendavyo kwa maringo na mapozi
Viumbe ambavyo pasipo hivyo ulimwengu huu hakika ungekuwa sana na Jehanum!
Tunashukuru kwani katika uumbaji wako
Tunaona ukuu wa upendo wako kwetu.
Tunaomba uwabariki viumbe vyako hawa
Si kwa baraka zile za Kichina
Bali kwa baraka za Kijamaika na Brazili!
Na zile za kwetu za Kimakonde!
Na utuwezeshe sisi tunaofurahia uumbaji huo
Kuzidi kukaa macho bila kupepesa
Ili tusipitwe na lolote na tukalikosa!
Na tunawaonea huruma wale wanaoishi kwenye nchi ambazo uumbaji wako
Si rahisi kuonekana namna hiyo!
Ila tunaomba sana tena chonde chonde.. hata tukiingia majaribuni usitutoe mapema
Ila kwahakika usituache tuzame huko na kujisahau
Ila kama ulivyomfanyia Yona/Yunus yule nabii nasi hatimaye uturudishe kwenye nchi kavu!"
Na watu wote wasema AMEN, aMINA, AMEEN!