Baba Mkwe ananidai Mahari

Baba Mkwe ananidai Mahari

Lech Poznan

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2025
Posts
450
Reaction score
585
Hapa nilipo nimechanganyikiwa kabisa, Baba mkwe wangu ananidai Mahari Nimalizie Nusu iliyobakia shilingi Milioni moja na Mimi kwasasa Mambo Magumu na tulikubaliana Mwezi huu wa kumi na mbili sasa Mambo yangu bado siyo Mazuri na uwezo wa kumpa hiyo Milioni hakuna ila nina Nusu yake, Shida ni jinsi ya kumpigia simu na kumueleza inaonekana yeye anahitaji Milioni

Kwasasa anampigia simu mwanae na kumuulizia na Mke wangu kila siku ananiuliza umempigia simu Baba yani mpaka wakati mwingine nakua na hasira, Najiuliza Je, nimpigie simu nimwambie kiasi nilichonacho na Je, akigoma kuchukua nitafanyeje?

Naombeni Ushauri wenu maana wakati mwingi nakua na mawazo.
 
R.I.P in advance.
Kama umeanza kuchanganyikiwa kitanzi kinakuja
Kitanzi kinakuja kivipi?
Achana nao,mkuu uwe una hudhuria vikao

Wenzio huwa hatumalizii mahari,wanakula nusu inawatosha

Kwanza umewasaidia sana kumsitiri mtoto wao
Kwahiyo una nishauri nisimtafute ?
Huyu Mke wangu ananisumbua kweli mpaka kuna muda nataka kumfokea ila nauchuna na anataka nilipe mahari yote.
 
Kitanzi kinakuja kivipi?
Kwahiyo una nishauri nisimtafute ?
Huyu Mke wangu ananisumbua kweli mpaka kuna muda nataka kumfokea ila nauchuna na anataka nilipe mahari yote.
Mke mwambie huna

Baba mkwe mkaushie,akikupigia mwambie hujaipata bado

Kila siku hayo ndo yawe majibu yako,mwsho wa siku watatulia kimya daima milele
 
Ninaamini wakati wa utoaji mahari sehemu ya kwanza ulikuwa na wazazi upande wako na mshenga. Kwa sasa pia inatakiwa isitoe kama zawadi kwa baba mkwe. Ita mmoja wa wazazi na mshenga wakampelekee mzee hiyo nusu ukiahidi kumalizia kiasi kilochobaki wakati mwingine. Hakuna dhambu kuwa muwazi kile ulicho nacho kwa sasa.
Hapa nilipo nime changanyikiwa kabisa, Baba mkwe wangu ananidai Mahari Nimalizie Nusu iliyobakia shilingi Milioni moja na Mimi kwasasa Mambo Magunu na tulikubaliana Mwezi huu wa kumi na mbili sasa Mambo yangu bado siyo Mazuri na uwezo wa kumpa hiyo Milioni hakuna ila nina Nusu yake, Shida ni jinsi ya kumpigia simu na kumueleza inaonekana yeye anahitaji Milioni

Kwasasa anampigia simu mwanae na kumuulizia na Mke wangu kila siku ananiuliza umempigia simu Baba yani mpaka wakati mwingine nakua na hasira, Najiuliza Je, nimpigie simu nimwambie kiasi nilichonacho na Je, akigoma kuchukua nitafanyeje?

Naombeni Ushauri wenu maana wakati mwingi nakua na mawazo.
 
Hapa nilipo nime changanyikiwa kabisa, Baba mkwe wangu ananidai Mahari Nimalizie Nusu iliyobakia shilingi Milioni moja na Mimi kwasasa Mambo Magunu na tulikubaliana Mwezi huu wa kumi na mbili sasa Mambo yangu bado siyo Mazuri na uwezo wa kumpa hiyo Milioni hakuna ila nina Nusu yake, Shida ni jinsi ya kumpigia simu na kumueleza inaonekana yeye anahitaji Milioni

Kwasasa anampigia simu mwanae na kumuulizia na Mke wangu kila siku ananiuliza umempigia simu Baba yani mpaka wakati mwingine nakua na hasira, Najiuliza Je, nimpigie simu nimwambie kiasi nilichonacho na Je, akigoma kuchukua nitafanyeje?

Naombeni Ushauri wenu maana wakati mwingi nakua na mawazo.
Kwani ukigoma kumpa atafanyaje?

Atakuja kumchukua binti(probably no).

Sana sana ataongea ongea huko pembeni kwisha.

Yaani hata hiyo laki 5 usimpe, wewe mwenyewe unasema hela changamoto halafu utoe 500k kumpa mwanaume mwenzio
 
Back
Top Bottom