Baadhi ya watu wa JF na tabia zao

Tariq f

JF-Expert Member
Dec 11, 2021
233
345
JamiiForums ni jukwaa nililotokea kulipenda sana toka nijiunge nayo mnamo mwaka jana. Jukwaa hili nimetokea kuwa na uraibu nalo kabisa, kiasi kwamba haiwezi kupita siku bila kutupia jicho.

Tokea nijiunge kwenye hili jukwaa nimekuwa nikijifunza kutoka kwenu viongozi, nikiburudika na pia nikijengeka katika nyanja tofauti tofauti.
Vile watu wakigombana na kupatana huwa nafurahi sana, pia nafurahishwa na baadhi ya wanachama wa humu na tabia zao.

Baadhi ya wakali hao ni kama wafuatao;

Smart911 hajawahi mtukana mtu wala kumdhihaki mtu na mara zote anatakia watu mema, majibu yake hayazidi mistari miwili.

Bujibuji Simba Nyamaume mkongwe wa JamiiForums, mara zote huwa anatupa darasa vijana na kuhamasisha watu kwenye mambo mbalimbali.

Mshana Jr huyu jamaa ana ushawishi mkubwa JF, kiasi kwamba akitoa uzi lazima nikaucheki, na si kwangu tu bali kwa maelfu ya wana JF.

mpwayungu village huyu jamaa anaongoza kwa maadui JF, yaani mwamba angekuwa mubashara nahisi angedundwa hata ngumi, ila jamaa hajali ana kusongakusonga mbele.

GENTAMYCINE aka popoma, jamaa anapenda sana sifa, kila kukicha anatengeneza ID mpya, halafu anaanzisha hoja huku anajibu mwenyewe.

martial jb huyu jamaa huwaga namfuatilia sana, kwanza huwa anakuwa na hoja zenye nguvu na pia hachagui jukwaa, popote utamkuta yaani kiraka.

DeepPond huyu jamaa ni msimulia hadithi, anajua kweli kupangilia matukio ya simulizi kwa kifupi hamchoshi msikilizaji.

Tate Mkuu yaani yeye hata kama ukiiongelea Yanga kwa kheri yeye lazima atakubadilikia tu, akili yake imejaa unjano na utopolo.

Lizzy humwambii kitu kuhusu jukwaa la vyakula na JF Snaps.

HS CODE huyu jamaa utamkuta jukwaa la ajira tu, sijui hajaajiriwa? Anapenda uzi wa utumishi kuchelewa kuitwa kwenye saili.

NtYga huyu mwamba utamkuta uzi wa Manchester United tu! Tena maoni ni ya Kingereza.

National Anthem huyu mwamba huwa hatengenezi uzi, ila huwa anatoa maoni tu, kwenye ujinga anatoa maoni ya ujinga kwenye umakini anakuwa makini.

Erythrocyte huyu jamaa humwambii kitu kuhusu CHADEMA, nahisi ni Lissu huyu, anatoa maoni kwenye jukwaa la siasa tu.

CONTROLA mwamba yupo makini sana.

Extrovert mwamba yupo mnyenyekevu sana na anaonekana ni mpambanaji.

Kalpana mwanamama wa Simba, yaani ukiona Simba imeongelewa ujue lazima atie mguu.


Naomba wengine muendelee kuwaorodhesha na tabia zao, maana orodha si ya kitoto.
 
Jamii forums ni platform niliyotokea kuipenda sana toka nijiunge nayo mnamo mwaka jana,
Platform hii nimetokea kuwa addicted nayo kabisa kiasi kwamba haiwezi kupita siku bila kutupia jicho
Tokea nijiunge kwenye hii platform nimekuwa nikijifunza kutoka kwenu viongozi, nikiburudika na pia nikijengeka katika nyanja tofauti tofauti
Vile watu wakigombana na kupatana huwa nafurahi sana,
Pia nafurahishwa na baadhi ya members wa humu na tabia zao; baadhi ya wakali hao ni kama wafuatao

Smart911 hajawahi mtukana mtu wala kumdhihaki mtu na always anatakia watu mema, reply zake hazizid mistari miwili

Bujibuji Simba Nyamaume mkongwe wa jamii forums, always huwa anatupa darasa vijana na kuhamasisha watu kwenye mambo mbalimbali

Mshana Jr huyu jamaa ana influence kubwa jf, kiasi kwamba akitoa uzi lazima nikaucheki na si kwangu tu bali kwa maelfu ya wana jf

mpwayungu village huyu jamaa anaongoza kwa maadui jf, yaani mwamba angekuwa live nahisi angedundwa hata ngumi, ila jamaa hajali ana keep moving

GENTAMYCINE aka popoma, jamaa anapenda sana sifa, kila kukicha anatengeneza ID mpya, halafu anaanzisha hoja huku anajibu mwenyewe

martial jb huyu jamaa huwaga namfuatilia sana, kwanza anakuwaga na hoja strong na pia hachagui jukwaa popote utamkuta yaani kiraka

DeepPond huyu jamaa ni story teller, anajua kweli kupangilia matukio ya simulizi in short hamchoshi msikilizaji

Tate Mkuu yaani yeye hata kama ukiiongelea yanga kwa kheri yeye lazima atakubadilikia tu, akili yake imejaa unjano na utopolo

Lizzy humwambii kitu kuhusu jukwaa la vyakula na jf snaps

HS CODE huyu jamaa utamkuta jukwaa la ajira tu, sijui hajaajiriwa!? anapenda uzi wa utumishi kuchelewa kuitwa kwenye saili

NtYga huyu mwamba utamkuta uzi wa Manchester United tu! Tena comments ni za kiingereza

National Anthem huyu mwamba huwa hatengenezi uzi, ila huwa ana comment tu, kwenye ujinga ana comment ujinga kwenye usiriaz anakuwa siriaz

Erythrocyte huyu jamaa humwambii kitu kuhusu chadema, nahisi ni lissu huyu ana comment kwenye jukwaa la siasa tu

CONTROLA mwamba yupo makini sana

Extrovert mwamba yupo humble sana na anaonekana ni fighter..

Kalpana mwanamama wa simba, yaani ukiona simba imeongelewa ujue lazima atie mguu..



Naomba wengine muendelee kuwaorodhesha na tabia zao, maana orodha ni si ya kitoto...
mwaJ, Sky Eclat, Evelyn Salt , Zion Daughter, mwa Jay, sweetlady, suzy, Pearl, cacico nimewamiss sana mjue
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom