Baadhi ya Wakuu wa Taasisi kugoma kuhamia makao makuu ya nchi Dodoma si uhaini? Jeuri hii wanaitoa wapi?

The Sunk Cost Fallacy 2

JF-Expert Member
Nov 8, 2022
7,382
8,437
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge na Uratibu amesema Kuna Taasisi za umma Kwa makusudi zinagoma kuhamia Makao Makuu ya Nchi Dodoma..

Suala kama Kuna wakuu wa Taasisi wanagomea uamzi wa Nchi je huu sio uhaini? Nani anawapa hiyo jeuri? Wanagoma kama kina nani?👇



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu George Simbachawene ameziagiza taasisi 42 za serikali kuhamia Dodoma mwaka wa fedha 2022/2023 huku taasisi 36 zikielekezwa kufanya hivyo mwaka wa fedha 2023/2024 bila kuwa na kisingizio chochote

Ametoa maagizo hayo Jijini Dodoma kwenye zoezi la utoaji vibali vya Ujenzi wa Ofisi za taasisi mbalimbali ambapo amesema kuwa taasisi 19 zitahamia Dodoma mwaka wa fedha 2024/2025 huku Taasisi 27 zikielekezwa kuzingatia aina ya majukumu zilizonazo na kuendelea kutekeleza majukumu yake mkoani Dar es Salaam kwani mpaka sasa tayari taasisi 65 zimeshahamia Makao makuu ya nchi.

Katika hatua nyingine Waziri Simbachawene amesema jumla ya taasisi 189 zilikua zinatekeleza majukumu yake Jijini Dar Es Salaam ambapo taasisi 55 zimetekeleza maelekezo hayo kwa kujenga ofisi zake Dodoma na hadi sasa taasisi 20 zimekamilisha ujenzi na 16 zinaendelea na hatua mbalimbali huku 19 zikiendelea na maandalizi ya ujenzi baada kupewa vibali.👇

 
Kivipi ulikuwa wa kipuuzi na kisiasa?
Kwa sababu hakukuwa na sababu ya msingi ya kiuchumi, na zaidi, zoezi hilo ni zoezi lenye gharama sana, hususan kwa nchi yenye uchumi mdogo kama wetu.

Jenerali Ulimwengu anasema mji mkuu wa Tanzania ni barabara inayounganisha Dar na Dodoma, kwa sababu kila siku imejaa safari za wakubwa wa chama na serikali wakisafiri kati ya Dar na Dodoma.

Dar ilikuwa na vitu vyote vya kuwa mji mkuu, hakukuwa na sababu ya msingi ya kuichumi, na hata kisiasa hakukuwa na sababu nzuri.

Hizo habari za kusema mji mkuu uwe kati uwe karibu na watu wote ni ujinga tu, kwa sababu ugatuzi wa madaraka ungefanyika na polepole teknolojia kutamalaki, serikali ingewafuata watu angalau mpaka wilayani kila wilaya.

Tumeamua kuhamisha mji mkuu kwa pupa, gharama zake tunaziona mpaka leo watu hawataki kuhamia huko.

Wa Nigeria wenzetu walitaka kuhamisha mji mkuu, wakaja kwetu kujifunza, wakaenda CDA pale. Wakachukua mipango yetu, wakaenda kwao, wakahamisha mji mkuu kutoka Lagos kwenda Abuja na kumaliza zoezi kabla yetu. Lakini wenzetu walikuwa na hela za mafuta, ambazo sisi hatuna.

The whole exercise was very unnecessary and extravagant, ni vile tu tumezoea kuishi kwa mbiu ya "zidumu fikra za Mwenyekiti, zidumuuu".

Dar es salaam grew up organically to be the natural capital, you can't fight nature like that.

Yani hapa ni sawa na tuna uamuzi tukae chini kutoka mlimani halafu maji ya mto yatiririke tuyachote kiurahisi, au tukae juu mlimani tuyapandishe maji kwa water pump bila sababu.

Sisi tumeamua kuyapandisha maji juu, bila sababu.

Tunaingia gharama kununua pump, kujenga miundombinu ya kupandisha maji, kulazimisha watu waende juu tunakotaka kukaa.

Lakini watu si wajinga, wanaona kukaa juu hakuna tija, tena **** matatizo mengi, ndiyo maana wanakaa chini wapate maji kiurahisi, wanaenda juu wakiitwa kuhesabiwa tu.
 
Uamuzi wa kuhamisha mji mkuu kwenda Dodoma ulikuwa wa kipuuzi na kisiasa zaidi.

Haya ndiyo matokeo yake.
Yaani waziri pia Mbunge badala ya kutetea Hela zinazopotea Kwa kulazimisha watu kuzichezea kisa waonekane wapo Dodoma zitumike hata kukwamua umaskini katika Jimbo lake yeye anang'ang'ania watu watumbue Hela ili waonekane wapo Dodoma!! Muheshimiwa Simbachaweni watu wako ni Maskini sana Jimboni!! Kuhamia Dodoma wakati Kuna Serekali mtandao hakuna Tija!! Kwa vile ni Mgogo unaona kuhamia Dodoma ni Tija!?
 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge na Uratibu amesema Kuna Taasisi za umma Kwa makusudi zinagoma kuhamia Makao Makuu ya Nchi Dodoma..

Swala kama Kuna wakuu wa Taasisi wanagomea uamzi wa Nchi je huu sio uhaini? Nani anawapa hiyo jeuri? Wanagoma kama kina nani?👇




Na yeye pamoja na boss wake wanawaogopa hao watu, kwanini akimbilie kwenye media badala mamlaka ya uteuzi?
 
Yaani waziri pia Mbunge badala ya kutetea Hela zinazopotea Kwa kulazimisha watu kuzichezea kisa waonekane wapo Dodoma zitumike hata kukwamua umaskini katika Jimbo lake yeye anang'ang'ania watu watumbue Hela ili waonekane wapo Dodoma!! Muheshimiwa Simbachaweni watu wako ni Maskini sana Jimboni!! Kuhamia Dodoma wakati Kuna Serekali mtandao hakuna Tija!! Kwa vile ni Mgogo unaona kuhamia Dodoma ni Tija!?
Mkuu hao mawaziri wa sasa kuwalaumu kwenye hili ni sawa na kumlaumu mtoto ambaye baba yake ni kichaa na kashafanya madudu kibao huko nyuma.

Ukishaingia kwenye hii serikali tu, umekubali ujinga. Labda uwalaumu kwa kukubali kuingia kwenye hii serikali.

Yani mtu ukishaingia tu unakutana na uamuzi kama wa kuhamia Dodoma ulishafanywa zamani sana na kupitishwa, na serikali ishafundishw na Mchongameno isirudi nyuma isije kugeuka jiwe la chumvi, sasa utaupingaje uamuzi kama huo?

Na naturally watu hawakubaliani nao, so unapewa kazi ya kufanya mvua inyeshe kutoka chini kwenda juu.

Ndiyo maana watu wanaona wakipata nafasi ya kupiga wanapiga tu, serikali yenyewe imejaa maamuzi ya kijinga ya muda mrefu sana tu.
 
Mkuu hao mawaziri wa sasa kuwalaumu kwenye hili ni sawa na kumlaumu mtoto ambaye baba yake ni kichaa na kashafanya madudu kibao huko nyuma.

Ukishaingia kwenye hii serikali tu, umekubali ujinga. Labda uwalaumu kwa kukubali kuingia kwenye hii serikali.

Yani mtu ukishaingia tu unakutana na uamuzi kama wa kuhamia Dodoma ulishafanywa zamani sana na kupitishwa, sasa utaupingaje uamuzi kama huo?

Na naturally watu hawakubaliani nao, so unapewa kazi ya kufanya mvua inyeshe kutoka chini kwenda juu.
Bora wapite kimya bila kihamasisha, ujinga Mkubwa ni pamoja na kuhamisha bandari kwenda Dodoma
 
Yaani waziri pia Mbunge badala ya kutetea Hela zinazopotea Kwa kulazimisha watu kuzichezea kisa waonekane wapo Dodoma zitumike hata kukwamua umaskini katika Jimbo lake yeye anang'ang'ania watu watumbue Hela ili waonekane wapo Dodoma!! Muheshimiwa Simbachaweni watu wako ni Maskini sana Jimboni!! Kuhamia Dodoma wakati Kuna Serekali mtandao hakuna Tija!! Kwa vile ni Mgogo unaona kuhamia Dodoma ni Tija!?
Na hili ndo linamsukuma... Maslahi binafsi
 
Zamani huko walikuwa wananadi sababu 2 kubwa:
1. Serikali kuwa karibu na watu wengi
2. Usalama dhidi ya maadui kutoka nje wanaoweza kushambulia mji mkuu Dar kutoka baharini..

Sababu zote hizi zimeshapitwa na wakati kutokana na maendeleo ya teknolojia
 
Back
Top Bottom