Siri ya sifuri
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 2,615
- 2,264
Wakuu, leo ningependa tujadili juu ya huyu mlezi asie na bahati mbele ya jamii. (mama wa kambo)imekua ni nadra sana kwa jamii ama mtu mmojammoja kuonesha heshima au kuwa na shukrani kwa huduma ya malezi inayotolewa na mama wa kambo. siku zote yeye amekua niwakukosolewa na kulaumiwa tu,
Hebu tuchukulie pale mama wa kambo anapokua karibu na mtoto huyu wa mumewe, watu tunaona anamnyanyasa na pale anapomuacha huru watu tunaona hamjali matokeo yake mlezi huyu anapoteza msimamo na kushindwa kumlea mtoto vizuri na matokeo yake mtoto anakosa malezi bora.
Yote hayo yanatokea si kwasababu hawana mapenzi ya kweli kwa watoto wa waume zao bali ni kwasababu ya kutaka kuiridhisha jamii inayowazunguka ambayo inawatu wenye mitazamo tofauti. hivi ni kwanini mama wa kambo hathaminiwi na hapewi heshima inayostahili?
Hebu tuchukulie pale mama wa kambo anapokua karibu na mtoto huyu wa mumewe, watu tunaona anamnyanyasa na pale anapomuacha huru watu tunaona hamjali matokeo yake mlezi huyu anapoteza msimamo na kushindwa kumlea mtoto vizuri na matokeo yake mtoto anakosa malezi bora.
Yote hayo yanatokea si kwasababu hawana mapenzi ya kweli kwa watoto wa waume zao bali ni kwasababu ya kutaka kuiridhisha jamii inayowazunguka ambayo inawatu wenye mitazamo tofauti. hivi ni kwanini mama wa kambo hathaminiwi na hapewi heshima inayostahili?