OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 419
- 670
Kuna malipo ambayo sio kodi, matharani ni tozo, ushuru au ada na hakuna huduma ambayo mtu anaipata kutokana na malipo hayo zaidi ni kumuongezea mwananchi mzigo kwa kumuongezea gharama za maisha. Angalia mfano ufuatao
Katika stendi za mabasi, mathalani Stendi ya Magufuli, unatakiwa kulipa Tsh. 300 na hakuna huduma unaipata kujustfy malipo hayo, mtu mwenye tiketi anapita bila kulipa. Inawezekana unaenda ndani kukata tiketi, na unalazimika kulipa fedha hiyo ambayo imeshakuwa mazoea kwenye stendi nyingi nchini
NI hela ndogo, lakini kuna watu hata nauli wanasaidiwa ili kuweza kusafiri, ni vyema ofisi za mabasi ziwe nje, ili mtu akate tiketi aingie bure ili kupata huduma kama ni ya usafiri au nyinginezo
Gharama nyngine kwenye Stendi
Mbali na kulipa Tsh. 300 kwenye stendi bado mtu huyu atalipa Tsh. 300 kwenda haja. Je Tsh. 300 ya mwanzo ililipwa kwa ajili ya nini, kama ni malipo ya huduma za ndani kwa nini mtu asilipe Tsh. 300 ambayo itamuhakikishi kupata huduma zote za ndani ya stendi ikiwemo kwenda haja?
Fikiria hili!
Mama mwenye mtaji wa Tsh. 30,000 anauza matunda ndani ya stendi ambapo anakaa kuanzia saa 11 asubuhi hadi saa mbili usiku, anaweza kwenda haja mara ngapi, anapata faida gani kwenye biashara ndogo kama hii.
Masikini analia zaidi
Signed OEDIPUS
Katika stendi za mabasi, mathalani Stendi ya Magufuli, unatakiwa kulipa Tsh. 300 na hakuna huduma unaipata kujustfy malipo hayo, mtu mwenye tiketi anapita bila kulipa. Inawezekana unaenda ndani kukata tiketi, na unalazimika kulipa fedha hiyo ambayo imeshakuwa mazoea kwenye stendi nyingi nchini
NI hela ndogo, lakini kuna watu hata nauli wanasaidiwa ili kuweza kusafiri, ni vyema ofisi za mabasi ziwe nje, ili mtu akate tiketi aingie bure ili kupata huduma kama ni ya usafiri au nyinginezo
Gharama nyngine kwenye Stendi
Mbali na kulipa Tsh. 300 kwenye stendi bado mtu huyu atalipa Tsh. 300 kwenda haja. Je Tsh. 300 ya mwanzo ililipwa kwa ajili ya nini, kama ni malipo ya huduma za ndani kwa nini mtu asilipe Tsh. 300 ambayo itamuhakikishi kupata huduma zote za ndani ya stendi ikiwemo kwenda haja?
Fikiria hili!
Mama mwenye mtaji wa Tsh. 30,000 anauza matunda ndani ya stendi ambapo anakaa kuanzia saa 11 asubuhi hadi saa mbili usiku, anaweza kwenda haja mara ngapi, anapata faida gani kwenye biashara ndogo kama hii.
Masikini analia zaidi
Signed OEDIPUS