Hapo unaposema suala la Machinga eti alishauriwa vibaya nadhani haupo sawa. Alichofanya Mama ni jambo la kupongezwa na yeyote mwenye akili. Nchi haiwezi kuwa na watu wanaotaka kufanya biashara za nyanya na dagaa kwenye barabara au popote tu ilimradi mtu kajisikia , ni vurugu hakuna utaratibu , miji inaonekana michafu.TISS.
Mama anatakiwa afanyekazi na anaowaamini kwani Sukumagang walikuwa kotekote so wakishaondoka hao basi kwani watakuwa chini ya uangalizi.
Hata Sirro kupewa Ubalozi ni sehemu ya uangalizi.
Mwendazake alisisi chama ndani ya chama kwani lazima waondolewe ili kumfanya Kiongozi Mku awe huru ktk utendaji wake.
Mama anafanyia Kazi ktk mazingira magumu hata machinga kuondolewa alishauriwa vibaya ili aendelee kuchukiwa kwani chuki kwake ni kubwa.
Na tukumbuke mama ameridhi madeni makubwa ambayo anayoyalipa ndo maana mambo mengine hayaendi lakini wengine wanaojua hili hawaliongelei
Ukienda kwa wenzetu unakuta miji misafi sana hakuna nyanya barabarani wala vibandabanda visivyoeleweka, kama unataka huduma nenda sehemu husuka sokoni hata kama ni mbali. Mbona majumbani mwenu hamuweki jiko la mkaa Sebuleni mkapika Kande.
Mama amefanya vema sana suala la Machinga, pia Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam ameonyesha uthubutu kuliheshimisha jiji ikiwa ni pamoja na Mbezi yetu.
HAKIKISHENI MACHINGA HAWARUDI KUHARIBU MAADHARI YA JIJI LETU