Baada ya Serikali kusema ipo tayari kulipia matibabu ya Lissu; Peter Msigwa, Godbless Lema na Mbowe wakosoa kauli hiyo

Wa Tz nani katuloga kama serekari imekubali kusaidia matibabu Ls litakuwa jambo jema tulipokee tunachohitaji sisi ni kuona Ls analejea katika hari yake na si vinginevyo tusitengeneze kauli zitakazo wafanya serekari kughaili jambo hili kwa kauli zetu

Nadhani dada @Faizafox kachoka fanya masahihisho. Binafsi nikiona mtu kaandika sentensi sehemu ya kuweka L anaweka R ama hajui kuwa Nomino huanza na herufi kubwa huwa nakumbuka umuhimu wa ELIMU, ELIMU, ELIMU.
 
Katika suala hili la Lissu...wapi familia yake? Yaani mama, baba mdogo au mkubwa, shangazi na mama wadogo? Wakina Lema ndo wamegeuka baba wadogo zake na wasemaji wa familia.

Ni vema familia ya Lissu ikamuondoa Lissu katika minyororo ya wanasiasa hadi hapo atakapopona. Awepo msemaji wa familia juu ya mwenendo wa afya ya mpendwa wao na wasiwaachie hawa mashakubimbi ndio wakawa wasemaji....ugonjwa wa Lissu umegeuka kuwa ngazi ya kujipatia umaarufu.
Hauwezi ukawa na uchungu kumzidi mkewe. Yupo na anaona kinacho endelea. Hao ndugu wengine ukiwaona utawafahamu?

Chadema ni zaidi ya ndugu zake mbona wengine waliishia tu kwenda general Dodoma baada ya hapo wakapotea....... Hao wanao jisafisha saivi mbona mwanzo walipewa nafasi wakajitoa....Msilete malumbano yasiyo na tija....muacheni mana hata hizi kelele hazisaidii.
 
Yule katibu mkuu aliyetumwa akatibiwe India, ebu mnikumbushe vizuri,, aaargghhh. Hivi leo tarehe ngapi waungwana, kumbe sijaenda job. Alllaaah
 

Taarifa ya Ummy Mwalimu ya kuitaka Famili ya Lissu kuandika barua kama wanaitaji matibabu ya Lissu. na kwamba Serikali ipo tayari kujibu Lissu sehemu popote Duniani. Kwanza aache Uongo na upotoshaji, Serikali haipo tayari, ndo maana Spika kwa kinywa chake alikataa kwamba wao hawapo tayari kumtibu Lissu katika Hospital ya naiorbi. Vilevile sio utaratibu pale Mbunge anapokuwa mgonjwa kwamba Familia ndo iandike barua. Katibu wa Bunge na Spika ndo wanapaswa.

Leo siku ya 14 Spika wa bunge wala katibu wa bunge hawajawahi kutembelea Familia wala kumtembelea Mgonjwa Hospitalini.

Spika aliugua sana hivi karibuni, Wakina Mwakyembe Mwandosya, na wengine wengi wa CCM, je Utaratibu ulikuwa wa kuandika barua? Leo siku ya 14 Serikali haijatoa chochote.

Ummy, Mwamie aliyekutuma kwamba tutamlinda kwa sala zetu, hatujashindwa kama Wanachama, Hatujashindwa kama Watanzania kuchanga Shilingi moja moja kumtibia Lissu. Sala inasaidia Uponyaji, lakini wanaofanya sala manwakamata.

Kumbuka Familia ya Lissu ni Watanzania wote wanaopenda Utawala wa sheria na Kidemokrasia. Famililia ya Lissu ni Watanzaina wote wanaoguswa na Mbunge kupigwa Risasi hadharani na bunge lisichukue hatua sitahiki. Hatujashindwa kumlipia matibabu, Tutachanga Shilingi MOja moja tutauza hata mali zetu ili Lissu asikose matibabu.

Nikwambie Ummy mwambie aliyekutuma na wewe usikubali kutumwa vitu kama hivi, unafahamu nini kinaendelea. Ndo sababu Serikali yenyewe pamoja na viongozi wa Bunge wamekosa usajili wa kuja kumsalimia Mbunge ambaye yupo taabani sababu wanajua jambo hili limetendwa na nani.

Vinginevyo Bunge lingekuwa la kwanza kumlilia Lissu sababu Lissu ni Familia ya Bunge na baadala yake leo ni siku ya 14 Spika wala Naibu Spika aliyekuja Hospitali. Hata Ulipoombwa Muongozo wa kuteua wabunge bungeni waje kumtembelea Lissu, naibu Spika alisema walioko huko Nairobi wanatosha.

Mbunge wa CCM aliyekuja kumjulia hali Lissu ni Lazaro Nyalandu, hakuna Mbunge wala kiongozi wa Serikali wala Wa CCM aliyekuja kumtembelea Lissu Hospitali.

Hivyo Mheshimiwa Ummy hizo ngonjera hazisaidii.

Serikali ilipotaka kwanza apitie.muhimbili ni familia iliyosema itakuwa comfortable ikimpeleka ndugu yao...! Kwa hiyo ni famiia yenyewe ndiyo inaweza kuamua kama ina hitaji msaada wa serikali au lah..
 
Ndugai na wengineo wanapoumwa huanzia muhimbili kisha kupatiwa rufaa.
Tundu lissu hakufuatishwa utaratibu hata moja, hivyo ni lazima yatoke maombi rasmi ili taratibu zivunjwe.
Lema, Msigwa acheni upotoshaji!
 
Back
Top Bottom