Baada ya miaka miwili simpendi tena

Baada ya miaka miwili simpendi tena

nimechafukwa

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2013
Posts
290
Reaction score
237
Nina mwanamke nimedumu naye miaka miwili lakini tatizo ni kwamba simpendi tena, kwakweli binti anatabia nzuri mkarimu na anajua kujishusha. Mimi mwenywe sijawahi kicheat lakini nimekuja kujigundua vitu navyopenda kwa mwanamke ni mwanamke mwenye miguu mizuri(ya bia) mahips na makalio.

Vitu hivyo mimi nikiviona basi nakua hoi, tatizo niliye naye hana hizo sifa za kunisisimua naogopa kumwacha sababu hajanikosea na wala sitarajii aje kunikosea mbeleni, she is loyal tatizo kwa sasa tu ndo hilo hanivutii. Je nifanyeje?
mjomba kuniuliza kwanini nilimtongoza na hana vigezo vyangu ilitokea tu bahati mbaya.

Je kuna mtu alishapitia hii hali?
 
nimechafukwa

Na ukimuacha utajutia Ataondoka na madudu yako.


swissme
 
Last edited by a moderator:
Kuna baadhi ya mambo huwa tunafanya ila majuto huja baadae tu japo hutokea mara baada ya kuona haja zako hazipo kwake ila baadae inakua kama laana kwa sababu analia umempotezea muda wake umemuumiza kile kilio hua sio kizur jamani unaeza jikuta unadate na wanawake kibao ila kama yy huwez mpata tena. everything happens for a reason, ipo namna si bure wewe
 
kuna baadhi ya mambo huwa tunafanya ila majuto huja baadae tu japo hutokea mara baada ya kuona haja zako hazipo kwake ila baadae inakua kama laana kwa sababu analia umempotezea muda wake umemuumiza kile kilio hua sio kizur jamani unaeza jikuta unadate na wanawake kibao ila kama yy huwez mpata tena. everything happens for a reason, ipo namna si bure wewe

hicho ndo kitu kinaniumiza kichwa sasa.....lakini bado mm kijana na sijaoa. kwann nioe nisiyempenda?..ntakua nacheat tu na Co vzuri
 
hicho ndo kitu kinaniumiza kichwa sasa.....lakini bado mm kijana na sijaoa. kwann nioe nisiyempenda?..ntakua nacheat tu na Co vzuri

Basi mwisho wa siku ni wewe ndo unaechagua maamuzi ya mwisho nakusahur fanya vile moyo wako unakoelekea
 
Mkataa pema pabaya panamuita. Ni vzr ukachukua uamuzi wa kumwambia ukweli na mkaachana kwa salama kwani siku zote kibaya cha jitembeza kizuri cha jiuza. Kwa sifa ulizompa hakika hatakosa wa kumfariji.
 
Nishawahi waza kidogo mawazo kama juu ya mchumba wangu..
Ni tamaa ya ngono tu ambayo ilinifanya niwaze ujinga huo...Usijaribu kumwacha huyo mwanamke kwa sifa ulizotaja.Hao unaowataja kua ni wazuri wametunzwa na kufikia hali hiyo.Usimwache utaja jilaumu.Usiwaze ngono Thamin upendo wake wa dhati.ACHA TAMAA!!
 
If you want out then just be done with it. Tell her outright (ON second thoughts don't- Ucmuumize msichana wa watu). Just find a favorable moment and reason to leave her. She will get a good man who will be seven times better

BUT.
While you will surely (Yani hata ukitoka tu hapo nje) get a girl with proper (in your perspective) legs configuration, there is going to come a time when you realize she was the only one who you could've been better off with (EVER!).
When this time comes, just be a man and take responsibility for your decisions? Usije tujazia seva hapa ukituomba tuumize vichwa tupate namna ya kukurudisha kwa "The Love of Your Life". Ni hayo tu!
 
Kuna baadhi ya mambo huwa tunafanya ila majuto huja baadae tu japo hutokea mara baada ya kuona haja zako hazipo kwake ila baadae inakua kama laana kwa sababu analia umempotezea muda wake umemuumiza kile kilio hua sio kizur jamani unaeza jikuta unadate na wanawake kibao ila kama yy huwez mpata tena. everything happens for a reason, ipo namna si bure wewe

Maelezo yako yanajitosheleza kwa washenzi wote wanaoacha wake zao kizembe zembe.
 
Jifunze tu kuvipenda alivyonavyo huna jinsi ingekuwa hajakuvutia mara ya kwanza usingemtongoza au sijui mlikutanishwa au ulimpatia wapu,mpende tu. Utakuja kupenda ambapo patakutia sononi tu
 
Akiongeza makalio na miguu ya kichina itakuwaje ?
 
Ni wazi kuwa hujui unachopenda kwenye mahusiano ya mapenzi. Kaa chini ujitafakari ili ufanye maamuzi sahihi usije ukapatwa na mengi huko mbeleni. Kupenda ni suala zito lakini cha ajabu wengi tunapenda kulichukulia kirahisirahisi. Usiji-commit kwa mtu kwa nia ya mapenzi wakati unamuhitaji kimwili au kuondoa upweke.
 
Mmmh unataka mke wa kuishi naye ndani au we kuuza naye sura? Ila Ni vizuri pia Kuwa na Mtu anayekuvutia, usije ukaishia Kuwa na michepuko kwa excuse ya kutafuta Miguu ya bia na ,
makalio. Muache tu binti wa watu, atampata atakayempenda na vimiguu vyake n flat screen. Coz nachoona Ni Kuwa upo naye kwa sababu tu unamuonea huruma kumuacha. Hakunaga mapenzi ya huruma,
 
Mkataa pema pabaya panamuita. Ni vzr ukachukua uamuzi wa kumwambia ukweli na mkaachana kwa salama kwani siku zote kibaya cha jitembeza kizuri cha jiuza. Kwa sifa ulizompa hakika hatakosa wa kumfariji.
Tena akae akilijua hilo na alizingatie SN.... Kwa NN wanaume wengine hamujitambui? Hv kugeuza mwanamke kama tishu mnaon vyema eee!!
 
Back
Top Bottom