GE2025 Baada ya Lissu kutoletwa Mahakamani kwa sababu za kiusalama; Kesi yapangwa November 12, 2025 , Jamhuri waagizwa kuleta mashahidi

GE2025 Baada ya Lissu kutoletwa Mahakamani kwa sababu za kiusalama; Kesi yapangwa November 12, 2025 , Jamhuri waagizwa kuleta mashahidi

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
427
Reaction score
666
Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wakili Tundu Lissu, ambayo ilipangwa kuendelea kusikilizwa tarehe 3 Novemba 2025, haikuweza kuendelea kama ilivyopangwa. Kesi hiyo iliahirishwa hadi 10
Novemba 2025, lakini hata tarehe hii ya leo Lissu hajafikishwa mahakamani.

Wakili wa Serikali, Thawabu Issa, ameieleza Mahakama kuwa wamewasiliana na Mkuu
wa Gereza la Ukonga na amewaambia kuwa Tundu Lissu hakufikishwa mahakamani kutokana na hali ya kiusalama. Aidha, Wakili wa Serikali ameeleza pia kuwa mashahidi waliopaswa kutoa ushahidi walikuwa wanatokea Ruvuma na Mbeya, lakini kutokana na hali ya usalama kutokuwa ya kuridhisha jijini Dar es Salaam, hawakuweza kusafiri kufika mahakamani.

Kutokana na hilo, upande wa Jamhuri uliomba ahirisho la siku 14 kwa mujibu wa kifungu
cha 302 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, ukieleza kuwa kushindwa kwa
mashahidi kufika kulitokana na sababu za kiusalama.

Baada ya kusikiliza maombi hayo, Mahakama imekubali ombi la upande wa mashtaka
lakini imeahirisha kesi hadi tarehe 12 Novemba 2025 na sio siku 14 walizoomba kwa ajili ya kuendelea na usikilizwaji. Mahakama imeagiza upande wa Jamhuri kuhakikisha mashahidi wanakuwepo siku hiyo na Tundu Lissu afikishwe mahakamani.
 
serikali yenye kila nyenzo inashindwa kuleta mtuhumiwa mahakamani kwa sababu za kiusalama? Come on aya mambo ndo yanachochea chuki kwa watu Upumbavu unafanyika kama huu maanza kutafuta mchawi kesi ya Lissu ifike mwisho kama mnamfunga mfungeni kama mnawamchia mwachieni kwa tulioshudia kwenye uchaguzi nani anaweza kuamini mahakama ziko uhuru ni muhimili unaojitegemea? hizi taasisi zimewekwa kwa maana nzuri sema viongozi wanazitumia vibaya ni mda zipewe power
 
Tukisema Serikali ya CCM imechoka tunamaanisha. Ikiwa wameshindwa kumlinda mtu mmoja watawezaje kutulinda Watz wanaozidi milioni sitini na tatu??

Upande wa Jamhuri wana beti, tar 11/11 kuna mchongo fulani utakaotoka. Sasa wanasikilizia upepo utabumaje. Kisha tar 12/11 watakuwa wameelewa nn cha kufanya.
 
Ukiona hivo ujue Lissu kagoma kushirikiana na wauaji.
 
Back
Top Bottom