Baada ya kuwajibishwa, dk. Nchimbi na Kagasheki kurudi tena barazani!!

Mada imeletwa for opinion polls! Ili watu fulani wasafishwe na kuhalalishwa!!

Ama kweli 'Nji' hii inaendeshwa ki-zuzu sana!!!

PP
 
Iakuwa vichekesho, hii itakuwa test nzuri sana kwa Bunge letu kama kweli lina meno!
 
RAIS Jakaya Kikwete anatarajia kuipanga upya safu ya Baraza lake la Mawaziri wakati wowote, huku baadhi ya wabunge na mawaziri wakitakiwa kusitisha mapumziko yao ya mwisho wa mwaka na kurejea jijini Dar es Salaam haraka.

Miongoni mwa wabunge waliositisha mapumziko yao na kurejea nchini ni aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi, aliyekuwa nchini Afrika Kusini na aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, aliyekuwa Uswisi.
Wabunge hao walipoteza nafasi zao za uwaziri baada ya ripoti ya Kamati ndogo ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, kuwagusa mawaziri hao kwamba walishindwa kuwajibika katika utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Ujangili.

Dk. Nchimbi anapewa nafasi ya kurejea kwenye Baraza la Mawaziri kutokana na kushiriki kwake kuipinga operesheni hiyo, ambayo kwa kiwango kikubwa ilikuwa chini ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, na kwamba alishawahi kumuandikia barua Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akiipinga.

Kwa upande wake Kagasheki, anatajwa kurudi kwenye Baraza la Mawaziri
kutokana na kubainika kwamba hakuwa na kosa na kwamba operesheni hiyo ilitekelezwa zaidi kijeshi na haikuwa chini ya wizara yake moja kwa moja.

Aidha Kagasheki anatajwa kuwa mmoja wa waliokuwa mawaziri hodari kutokana na uwezo wake wa kufuatilia mambo, ambapo akiwa ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii, alianza harakati za kukomesha biashara haramu ya pembe za ndovu.

SOURCE:mtandao-net.blogspot.com
UNAIONAJE HIYO?

To be honest, Balozi alikuwa mchapakaz, na ukifuatilia sakata lenyewe unakuta yeye kama yeye uhusika wake ni kama 0.1% tu. Ila kwa collective responsibility, alivyofanya kustep aside ni sahihi. Hivyo akiteuliwa tena kwenye baraza la Mawaziri siyo mbaya, kwa mtazamo wangu.
 
Huyo mzee Kagashjeki haa mimi naomba sana tafadali naomba Mungu arudi. Kwanza pia kaonyesha nidhamu ya hli a juu hata baada ya tukio

Ukimtazama tu unajua ni mtu muadilifu, aliyejaa ueledi. Mapungufu mengine ni ya kibinadam.
 
nchimbi?? aliandika barua kwa waziri mkuu kuipinga hiyo hoja,alipewa jibu gani?? iwapo yeye ataonekana safi kwa njia hiyo basi yule aliyepewa barua anamakosa(waziri mkuu).pinda alichukua maamuzi gani baada yakupokea barua yq nchimbi? kama hakuifanyia kazi huo ni uzembe..acheni kuwasafisha kirahisi hivi
 
Kama Nchimbi anarudi ina maana Pinda anapigwa chini. Kumrudisha Nchimbi ni kukubali kuwa kweli alimwandikia barua PM lakini PM akasema wapigwe tu tumechoka na hili ni kosa kubwa ambalo katika nchi zinazojua wajibu wa viongozi anatakiwa kufikishwa mahakamani na hivyo hafai kuwa Waziri Mkuu

PM hawezi kupigwa chini; hakuna kikao cha karibuni cha Bunge kuidhinisha PM mwingine; Rais angekuwa serious, kikao kile kilichomalizika kingemwidhinsja PM mwingine
 
nchimbi?? aliandika barua kwa waziri mkuu kuipinga hiyo hoja,alipewa jibu gani?? iwapo yeye ataonekana safi kwa njia hiyo basi yule aliyepewa barua anamakosa(waziri mkuu).pinda alichukua maamuzi gani baada yakupokea barua yq nchimbi? kama hakuifanyia kazi huo ni uzembe..acheni kuwasafisha kirahisi hivi

Kwenye hotuba ya Raisi ameweka wazi kuwa yeye ndiye aliyeagiza majeshi ya ulinzi na usalama kushiriki kwenye hiyo "campaign". Hakukuwa na uwezekano wa waziri mmoja kubatilisha maamuzi ya baraza la mawaziri lililoongozwa na Mh Raisi "collective responsibilities".
 
Kwa hili mimi nikiongea zaidi ntaambulia ban! Walifikiaje maamuzi ya kuwaachisha haraka kama hawakuangalia vigezo vyote hivyo wanavyoviona sasa hivi kwamba vinawapa sababu ya hao mawaziri kusimamishwa?
 
nchimbi?? aliandika barua kwa waziri mkuu kuipinga hiyo hoja,alipewa jibu gani?? iwapo yeye ataonekana safi kwa njia hiyo basi yule aliyepewa barua anamakosa(waziri mkuu).pinda alichukua maamuzi gani baada yakupokea barua yq nchimbi? kama hakuifanyia kazi huo ni uzembe..acheni kuwasafisha kirahisi hivi

Hivi mimi nikisema kuwa rais ndiyo alipaswa kujiwajibisha au kuwajibishwa je,nitakuwa na kosa? Embu chukulia naye pinda alimpelekea kikwete,na kikwete alipuuza unadhani si yeye ndiye tatizo? Pia kama yeye ndiye alibariki hiyo operesheni c ni kosa la pili hilo la kumfanya aachie kitengo? Wabunge wetu huko DDM they are nonsense,wanamuogopa kikwete badala yake wana waya waya tu.
 
==> Najaribu kumpigia cm JK...nimuombe Rais wangu.....WARUDISHE HAWA WAWILI.....Wizara zile zile....kwanza ni wachapa kazi....wazalendo....na wanajali maslahi ya taifa......NCHIMBI hakuona haya wala kuzubaa pale polisi walio enda kinyume na taratibu au kukutwa na rushwa ALIWAFUKUZA MARA MOJA.....

....KAGASHEKI is a super minister....ni mtiifu...mpiga kazi....hupigania taifa lake kila siku....na kawabana majangili kisawasawa....
...NAJUA JK...ni msikivu...mwelewa....anaongozwa na busara.....ATAWARUDISHA HAWA. Wawili....
 
Tatizo la nadharia hii ni kuwa kufanya hivyo ni kugombanisha (au kuchonganisha) mihimili miwili ya dola. Sidhani Kama wako tayari kwa hili.
 
Hivi hii nchi tukoje jamani!!! Tuna watu mil 46 hao wote waachie wengine jamani
 
Hivi mimi nikisema kuwa rais ndiyo alipaswa kujiwajibisha au kuwajibishwa je,nitakuwa na kosa? Embu chukulia naye pinda alimpelekea kikwete,na kikwete alipuuza unadhani si yeye ndiye tatizo? Pia kama yeye ndiye alibariki hiyo operesheni c ni kosa la pili hilo la kumfanya aachie kitengo? Wabunge wetu huko DDM they are nonsense,wanamuogopa kikwete badala yake wana waya waya tu.

mi nafikiri juu ya nani atamfunga paka kengele...hiyo 20% ya wabunge wasiokuwa na imani na jk itapatikana? watu wenyewe watakuwa chini ya jaji mkuu kama mwenyekiti,ikiwa jaji huyuhuyo kawekwa na jk.njia ndefu hiyo kaka makorongo mengi sana
 
Hapa kuna mawili, yawezekana mheshimiwa ana watu wachache sana wakuchagua kama mawaziri au anao wengi ila hajui kuchagua......sasa sitaki kuamini kama mheshimiwa hajui kuchagua...nionavyo mimi avunje record kwa kuvunja tena baraza la mawaziri lakini hivi sasa atuwekee hata kama ni sura ngeni au zilizozoeleka lakini awe mkali kwa hii miaka miwili iliyosalia aongoze mawaziri kufanya vitu ambavyo wananchi wanataka ni si ambavyo chama au vyama vinataka bila kujali itikadi....binafsi ningependa kuona nafasi za uwaziri zinakuwa za kiutendaji....watu watume CV zao zifanyiwe screening na vetting ikiwezekana kama hakuna board ambayo ni adilifu hapa Tanzania tuombe hata unbiased International consultants watusaidie halafu waziri aajiriwe kwa mkataba na apewe targets zake kama ni maliasili unapatiwa targets ambazo ni realistic kabisa ukishindwa kuzifikia basi mkataba wako na serikali unakuwa umeishia hapo kama ni waziri wa fedha na uchumi unapewa support yote na kwakutumia ujuzi wako basi ulisaidie taifa katika ku manage inflation na kuzuia anguko la shillingi yetu na vitu kama hivyo kwakuwa vinawezekana kabisa.....sijapata muda wa kusoma rasimu ya katiba hadi mwisho lakini kama katiba itakuwa na muelekeo wa hivyo nadhani tutapata mawaziri wawajibikaji sana....
 
Back
Top Bottom