Baada ya Kurudishwa Kutoka Marekani.

Nilipoajiriwa,bosi wangu anamiliki biashara yenye mtaji wa zaidi ya dola Milioni sita au saba hv,ni mtanzania na ana miaka 33,
ana vitega uchumi vingi na vya kutosha,elimu yake ni darasa la saba na si zaidi.........

huyu jamaa amesafiri nchi mbalimbali kibiashara,anaongea kiingereza cha kawaida,ni msomaji mzuri wa jamiiforum ingawa hajajiunga lakini pia anajuai vitu vingi sana vya sasa hv na anaishi kisasa kama vijana wa kisasa.

Nilichojifunza kwa bosi wangu huyu ni kwamba,elimu ni muhimu sana katika maisha,lakini si lazima uwe na elimu kubwa ndo ufanikiwe,mafanikio ni mchanganyiko wa vitu vingi sana,kama kufanya kazi kwa bidii,kusali sana,kuwa na ujasiri wa maamuzi,elimu ya wastani,uelewa wa mambo mengi angalau kidogokidogo,nia ya kufanikiwa na mengine mengi.

sasa mm nasema hv,hao jamaa zako inawabidi wabadilishe mitazamo yao kuhusu maisha huku nyumbani,pia wajifunze wako katika kipindi gani cha kiuchumi na kibiashara,lazima waangalie kuna fursa gani waweze kuzichangamkia,wakichagua kazi wamekwisha...watazeekea nyumbani na mwishowe watakua very frustrated,na hapo kuna hatari ya kuanza kutumia vitu vya ajabu ajabu...wafahamu pia wazazi wao wanaumia sana wakiwaona jinsi walivyo,kusomesha mtu au kumpeleka marekani mtoto si kitu ambacho wazazi wengi wanakimudu ni ghali...tena sana

waambie pia maisha yamebadilika sana siku hz,kuishi au kufanya kazi marekani sio ishu tena,ni kawaida tu,cha muhimu ni noti,noti noti......nasisitiza wasipobadilisha mitizamo yao wataishia pabaya sana huwezi kusema hawawezi kupata kazi wakati kazi zipo zimejaa tele....wawe wabunifu....si lazima aanze na kazi ya kulipwa million mbili....inabidi waanzie chini
maana system imeshawatupa...

Nashukuru sana kwa ushauri mzuri mkuu. Ntafikisha ujumbe!
 
nawasihi sana wale waliopata fursa kuzitumia kwa maana na umakini na malengo yaletayo manufaa kwa sasa na badae. hao jamaa hatuwezi kuwasemea sana kwa sababu hawapo hapa tukasikia nini wao wangesema. kama walifikiri hawatarudi home kabisa au walikuwa na sababu gani za kukutwa na yote haya.
ila mliopo huko sasa elimu ni muhimu, kuweka akiba ni muhimu sana. wajipange wasijekutwa na mambo kama haya.
japo kufanikiwa katika maisha si kuwa na elimu tu, kunahusisha na mambo mengi.

Nakubaliana na wewe. Tukipata nafasi tuzitumie vizuri na kuinvest kwenye vitu vinavyo appreciate in value over time.
 
Marekani na kwingine watu wanaenda na kazi zipo!! Kuna makundi ya watu tena ada wanatumiwa lakini hawakusoma na wametesa wazazi wao sana!! Matokeo yao wameishia kubeba maboksi tu na shule hakuna na wakipata hela ni partying tu. Kuna wengine wanaenda wanasoma na maboksi wanabeba ili kujiongezea kipata na maisha yao ni mazuri tena sana!! Kuna wengine wanatafuta njia ya kufika marekani hasa kwa kutumia shule fake, wakifika kule wanabeba boksi na wakipata hela wanasoma!! Bravo!! Wengine wanaenda pale wanaishia kubeba boksi na wakipata hela wanatanua tu hakuna savings, no investments at home!! Yaani nothing!! Sasa wale ambao wanaenda nje hasa marekani ambako opportunity za kazi za vibarua vipo na wanatanua na siku ya siku wanapigwa PI sasa unataka tuwaonee huruma!!! Katika maisha kila mtu atavuna alichopanda!!! No sympathy!!!!!!

Umenena Ukweli Mkuu Asante!
 
Hivi 'elimu' ni nini? Inapatikana wapi? Uzoefu unaweza 'unaelimisha'?
Swali zuri, naomba nikupe maoni yangu
Kufanikiwa maishani unatakiwa uwe na akili. Wengi wenye akili nyingi wana elimu ya juu, ingawa siyo wote.
Mleta mada, nadhani alikuwa hajui tofauti ya kuwa na akili na kuwa na elimu ... nawajua wasomi wengi bongo ambao wanatia huruma na wasio wasomi hapa US ambao wanapeta.
Ukiamua kuparty bila kuinvest, hata kama una elimu gani, hiyo si akili nzuri. Ukiamua kuinvest na kufanya kazi kwa bidii, hata ukiwa fundi seremala, au fundi matope bongo utafanikiwa kama una akili.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Yooote tuandike hapa....Lakini cha msingi hawa jamaa wanahitaji msaada. Umeshapanga namna ya kuwasaidia hawa rafiki zako. Tuache blah blah wakati watu wana shida.
utamsaidia mtubmwenye umri wa 45? Unajua midlife crisis wewe? Acha kabisa aisee.
 
Mwanangu Money Stunna acha visingizio. Kwani unadhani ni wewe pekee uliyeishi Marekani? Mbona tupo wengi na tumesoma na kusomesha? Tafuta sababu nyingine. Kama umejipanga vizuri ni rahisi kusoma Marekani kuliko Bongo. Hivyo mwanangu jiangalie upya ubadili mikakati utasoma tu kama una nia ya kufanya hivyo hasa ukizingatia umuhimu wa kufanya hivyo.Nadhani hii itakusaidia kubadilisha perception yako juu ya hili.
 
Mwanangu Money Stunna acha visingizio. Kwani unadhani ni wewe pekee uliyeishi Marekani? Mbona tupo wengi na tumesoma na kusomesha? Tafuta sababu nyingine. Kama umejipanga vizuri ni rahisi kusoma Marekani kuliko Bongo. Hivyo mwanangu jiangalie upya ubadili mikakati utasoma tu kama una nia ya kufanya hivyo hasa ukizingatia umuhimu wa kufanya hivyo.Nadhani hii itakusaidia kubadilisha perception yako juu ya hili.

ndio unaweza kujisomesha sijakataa,lakin kwa vijana wengi inakuwa ngumu,mtu anasoma mwaka wa kwanza harafu anabez kwenye kazi anaacha,matumiz yanakuwa makubwa sana,asa kama hauna ndugu wa kukusapoti,bill zinakuwa nyingi,unaona ufanye full time job,vijana wengi inawashinda mkuu,mim nasemea kitu ninachoona si kuambiwa
 
Mwanangu Money Stunna umesema vyema. Hapa tatizo si Marekani bali mipango ya mtu. Nami naongea kitu ambacho nimefanya na si kusikia wala kusimuliwa. Hivyo mwanangu kazi kwako si kulaumu. Piga moyo konde ubadilike utabadili maisha yako.
 
It depends wamerudishwa Vipi .kama walikuwa hawana Ada ya shule? USA is the land of opportunity street smart is the way to go.ukitaka kitu chochote hapa unapata hakuna madeal.its about your choices
Natalia tushike mkono nasi tuje, unanihamasisha, na kweli USA nawapenda sana kwenye biashara hamna longolongo kama East, wanakupa mzigo kwanza unauza unawapa chao siku zinaenda sio hao wa East pesa kwanza ndo wakupe biashara
 
ndio unaweza kujisomesha sijakataa,lakin kwa vijana wengi inakuwa ngumu,mtu anasoma mwaka wa kwanza harafu anabez kwenye kazi anaacha,matumiz yanakuwa makubwa sana,asa kama hauna ndugu wa kukusapoti,bill zinakuwa nyingi,unaona ufanye full time job,vijana wengi inawashinda mkuu,mim nasemea kitu ninachoona si kuambiwa

That is true.
Hii kujisomesha ni rahisi mno kuitamka na ni ngumu kui practice. Wee umeishi marekani unafahamu hili. Chukulia mtu ameingia marekani leo kutoka bongo na hana ada ya shule na ana mpango wa kubeba box ili aingie shule, pay check yake ya week ni dola ngapi na ada ni kiasi gani, na atafanya kazi kwa muda gani bila kutumia cent tano hadi ada itimie. Na unajua huku pia kuna bills za kulipa, na kama alikuja bila hela ujue mara nyingi ametoka kwenye familia ambayo haina pesa za kutosha na ujue huko bongo watu wanamtegemea pia.
Mtu kama huyu mpaka aje ku-settle inachukua muda mrefu, na katika huo muda anaweza akapata bahati mbaya na akarudishwa nyumbani akiwa hana kitu. Utamlaumu kivipi huyo mtu?
Halafu kibaya zaidi walewale uliokuwa unawatumia hela ndio wanakuwa wa kwanza kusema jamaa karudi bila kitu, wanasahau pengine wao pia walikuwa wana ku-set back.
 
Ni ujinga na upumbafu kuona utakaa marekani na kufanikiwa....wakome kuwa na mawazo ya kibaharia kama mtu flani hivi humu jf iliyekaa marekani miaka lukuki mwisho wa siku anakuja tz kutaka kuwa mjumbe wa nec....

mkuu umeua mno,!jamaa ni tikiti maji haswaaaa!
 
That is true.
Hii kujisomesha ni rahisi mno kuitamka na ni ngumu kui practice. Wee umeishi marekani unafahamu hili. Chukulia mtu ameingia marekani leo kutoka bongo na hana ada ya shule na ana mpango wa kubeba box ili aingie shule, pay check yake ya week ni dola ngapi na ada ni kiasi gani, na atafanya kazi kwa muda gani bila kutumia cent tano hadi ada itimie. Na unajua huku pia kuna bills za kulipa, na kama alikuja bila hela ujue mara nyingi ametoka kwenye familia ambayo haina pesa za kutosha na ujue huko bongo watu wanamtegemea pia.
Mtu kama huyu mpaka aje ku-settle inachukua muda mrefu, na katika huo muda anaweza akapata bahati mbaya na akarudishwa nyumbani akiwa hana kitu. Utamlaumu kivipi huyo mtu?
Halafu kibaya zaidi walewale uliokuwa unawatumia hela ndio wanakuwa wa kwanza kusema jamaa karudi bila kitu, wanasahau pengine wao pia walikuwa wana ku-set back.

Assessment yako ni nzuri na inaukweli kidogo
 
Usimbeze nadhani anatoa ushauri kuhusu umuhiu wa kusoma. Vijana shikeni elimu. Anachosema mtoa mada ni sahihi kabisa. Angalia jjirani zako wenye maisha mazuri angalau kidogo ni wale waliosoma. Elimu ni ufunguo wa maisha.
Wewe ni mtu wa ajabu sana. Kama wewe ulitaka kurudi nyumbani ni wewe. Wao pengine walitaka kubaki na kujiendeleza. Hatuwezi wote tukawa sawa. Kusoma na kumaliza, kupata kazi sio wote wameweza jwenda kwenye hio series.
Wapo waliosoma US hawapati kazi huko na sio chaguo lao kurudi nyumbani.
Narudia tena, kama wewe umejinyookea mshukuru Mungu wako. Na sio kuwabeza na kuwadharau wenzako.
Hujui nini Mungu amewaandikia, soon or later watafanikiwa na watakuacha wewe hapo unajifanya ndo umeshapatia maisha.
Maisha ni pata potea ndugu. Chunga mdomo wako.
 
Bongo tambalale bana maadamu akili mukichwa,nashukuru uamuzi wangu nilioufanya wa kurudi bongo fasta baada ya kuona mambo si mambo huko majuu,maisha yamekuwa mazuri zaidi bongo kuliko huko nilikokuwa na nimewaacha jamaa wako hoi kimaisha na hawataki kurudi bongo,utafikiri wana kesi za mauaji,kila kukichwa ni kuombana vijisenti
 
Back
Top Bottom