Baa na vilabu kufungwa saa tatu usiku; tuko serious?

Baa na vilabu kufungwa saa tatu usiku; tuko serious?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,643
Reaction score
164,790
Kupitia TBC1, nikiwa katika ofisa moja muda huu, nimeona habari kuwa vilabu na baa sasa kufungwa saa tatu usiku.


Swali ni je, kufungwa saa tatu usiku kutasaidia?

Tuko serious kweli?
 
Kupitia TBC1, nikiwa katika ofisa moja muda huu,nimeona habari kuwa vilabu na baa sasa kufungwa saa tatu usiku.

Je,kufungwa saa tatu usiku kutasaidia?

Tuko serious kweli?
Wacha tuendelee kujivutavuta, ila nasema itafika hatua baa, shughuli za ibada mikusanyiko misibani nk vitafungwa!sifurahii ila ni hatua za lazima. Dunia inaposisitiza lockdown lengo iondokane na gonjwa ili kwa pamoja, na wasi wasi tutaongoza kwa kuadhirika kwa Africa mzima na kupelekea kutengwa sijui hali itakuwaje, na lazima awepo wa kulaumiwa!
 
Hakikisha before saa tatu vyombo vimekolea kisawa sawa, wakifunga you have got nothing to loose. Mwendo wa kutembeza mbili mbili ama ndoo kabisa umewadia,
“Ila ninawasiwasi kuna kale kamtindo ka kujifungia kwenye mapub na sauti ya muziki kushushwa chini katashamiri haswa haswa”
 
Maajabu hayatuishi kabisa mwenyewe nimeshangaa tena kuna alietangaza kuanzia jumatatu hivyo hii week end nzima kuanzia jana watu waendelee kama kawaida hivyo maambukizi yataanza kuzuiwa jumatatu? Unatuumiza kuna tatizo gani kwa hawa viongozi wetu wanapotoa haya matamko? Tusidanganyane mikusanyiko ya bar hatuwezi ku maintain hiyo social distance hivyo hivyo kwa kwenye nyumba za ibada na masokoni pia
 
Jinsi janga la CORONA lilivyoshughulikiwa na serikali ya Tanzania imeonyesha wazi kipi hasa ni kipaumbele cha serikali hii. Ni dhahiri Wananchi si miongoni mwa vipaumbele hivyo. Ni kweli kuwa total lockdown haina uhalisia na maisha ya mtanzania lakini Bar zina athari gani endapo zitafungwa kabisa kwa kipindi hiki. Anaehitaji kunywa anunue akanywe kwake. Hii haitamuathiri mmiliki wa bar kumuondoshea kipato chake wala kumhini mnywaji asiyeweza kukaa bila pombe.
 
Kupitia TBC1, nikiwa katika ofisa moja muda huu,nimeona habari kuwa vilabu na baa sasa kufungwa saa tatu usiku.

Swali ni je,kufungwa saa tatu usiku kutasaidia?

Tuko serious kweli?
nikiwa katika ofisi moja 🤣

ina maana mkuu ungekuwa nyumbani hii habari ingekupita 🤣
 
Kupitia TBC1, nikiwa katika ofisa moja muda huu,nimeona habari kuwa vilabu na baa sasa kufungwa saa tatu usiku.

Swali ni je,kufungwa saa tatu usiku kutasaidia?

Tuko serious kweli?
Ndio Viongozi wetu vijana ambao Kuna jamaa alifungua uzi kuwasifia,,Iyo habari nlimsikia Jana mhe. Albert akisema kuwa baa zote zifungwe saa tatu usiku kwa kuwa kuanzia saa tatu usiku wanywa pombe wanakuwa wamelewa na kuanza kushikana🤣🤣🤣 Duh nkasema yani RC anajenga hoja Kama hii si Bora tu angekaa kimya.
Siyo lazima wote waongee wengine wafunge tu midomo yao Mana kila wakiongea 🙈🙈🙈
 
Serikali inachofanya ni Ku punguza maambukizi kwa inavyoona inafaa jukumu lililobaki ni lako mtanzania mwenzangu kujilinda wewe na familia yako kwa njia utakazoona zinafaa usiende kanisani kama unaona itakusaidia usiende bar kama utaona inakusaidia usalama unaanzia kwako mwenye
 
Kupitia TBC1, nikiwa katika ofisa moja muda huu,nimeona habari kuwa vilabu na baa sasa kufungwa saa tatu usiku.

Swali ni je,kufungwa saa tatu usiku kutasaidia?

Tuko serious kweli?
Hizo baa zinafunguliwa saa kumi alasiri na hata hivyo hazina watu wengi kama kwenye migahawa na hoteli, siku hizo baa kuuza kreti kumi ni ishu sana kreti nne, kumbuka ukizifunga baa utavifunga viwanda vinavyotengeneza bia, soda na pombe nyingine na wanaohudumia watapoteza ajira. Muhimu serikali ifunge masoko ili wafanyabiashara wake watawanyike kwa kuuza mitaani kwenye magenge madogomadogo.
 
Tatizo tunataka kodi,kwahio tukifunga pesa za miradi yetu je?
 
Hatutaki kuiga hata yale mazuri ya nchi nyinhine, leo UG wagonjwa 57,sisi zaidi, ila eti tukifanya kama UG au KNY, tutakua tumeiga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wenye baa wajiandae kwa hasara tu mana hata wakiacha kaunta wazi watu wanunue wakanywee home hawatanunua coz baa bia na vinywaji vingine bei huwa juu tofauti na kwa Mangi hapo baa zikifungwa kina Mangi fulu shangwe pamoja na liqour store

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom