Azam TV news: Dira ya dunia BBC wakae sawa

Azam TV news: Dira ya dunia BBC wakae sawa

GHOST RYDER

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
1,025
Reaction score
475
Hakika Mabadiliko yaliyoandikwa na Gazeti la Mwananchi leo yanadhihirishwa na Ukweli juu ya Habari ambayo nimeishuhudia katika dakika 33 zilizopita sasa kwa habari yao ya Saa zima.

Nimependezwa na Muundo wa Habari na mpangilio wa Habari zao; siataki kuzungumzia weledi wa wasomaji wa leo Bw. Charles Hilal na Bi. Ivona Kamuntu kwa maana ujuzi wao si wa kutilia shaka.

Wameweka interviews break jambo ambalo ni nadra sana katika habari za vituo vingine lakini pia zinaletaa maana ya bridging kwenye habari na kucomplement main story.

Wamaeongeza habari za kusomwa moja kwa moja na msomaji Studio na sio zile za Ripota na mkeka wake mwanzo hadi mwisho wa Habari.

Yanahitajika marekebisho madogo sana kama kujali muda wa kuanza maana leo mmeanza mmechelewa kiasi dakika 4 hivi; inawezekana ni sababu ya mabadiliko ila ni vema kuheshimu muda sana.

Kimsingi ni hatua njema sana kwa ubunifu huu na walau Tanzania tutashuhudia habari ya kwetu wenyewe ambayo itakidhi kiu ya watazamaji wenu.

Licha ya kuwa DTH si vibaya mkafikiria namna bora za kujitangaza na masoko zaidi ili watanzania wengi wanufaike na huduma zenu.

ADIOS
 
Wasipojiunga na ving'amuzi vingine kama continental au startimes, coverage yao itakuwa kwa population ndogo sana. Lazima wawe na angalau FTA mbili za habari na kuzi integrate na visimbuzi viwili-vitatu...!
 
Hizi stori nitaendelea kuzisikia na kuzisomaga tu
Maana nishanunua ving'amuzi viwili toka kujiunga na digital continental na star times
Na sina mpango wa kufuja tena pesa yangu kwa maving'amuzi
 
Hakika Mabadiliko yaliyoandikwa na Gazeti la Mwananchi leo yanadhihirishwa na Ukweli juu ya Habari ambayo nimeishuhudia katika dakika 50 zilizopita sasa kwa habari yao ya Saa zima.

Nimependezwa na Muundo wa Habari na mpangilio wa Habari zao; siataki kuzungumzia weledi wa wasomaji wa leo Bw. Charles Hilal na Bi. Ivona Kamuntu kwa maana ujuzi wao si wa kutilia shaka.

Wameweka interviews break jambo ambalo ni nadra sana katika habari za vituo vingine lakini pia zinaletaa maana ya bridging kwenye habari na kucomplement main story.

Wamaeongeza habari za kusomwa moja kwa moja na msomaji Studio na sio zile za Ripota na mkeka wake mwanzo hadi mwisho wa Habari.

Yanahitajika marekebisho madogo sana kama kujali muda wa kuanza maana leo mmeanza mmechelewa kiasi dakika 4 hivi; inawezekana ni sababu ya mabadiliko ila ni vema kuheshimu muda sana.

Kimsingi ni hatua njema sana kwa ubunifu huu na walau Tanzania tutashuhudia habari ya kwetu wenyewe ambayo itakidhi kiu ya watazamaji wenu.

Licha ya kuwa DTH si vibaya mkafikiria namna bora za kujitangaza na masoko zaidi ili watanzania wengi wanufaike na huduma zenu.

Ila wasipojiunga na ving'amuzi vingine kama continental au startimes, coverage yao itakuwa kwa population ndogo sana. Lazima wawe na angalau FTA mbili za habari na kuzi integrate na visimbuzi viwili-vitatu...!!
 
Hatuna muda nao maana hatuwezi kukusanya mavingamuzi meeengi ndani ya nyumba,, kama wanataka wapate watazamaji wengi wajiunge pia na vingamuzi vingine kama wanavyofanya wengine, otherwise nitaendelea na nilicho nacho tu,, labda wavigawe bure...
 
Haya maving'amuzi sasa yamekua mengi mara zuku,ting,continental,azam.....hivi haiwezekani kukawa na king'amuzi kimoja wote wakajisunda humohumo? Mtu unawezaje kuwa na king'amuzi zaidi ya kimoja kwa style hii....
 
Hizi stori nitaendelea kuzisikia na kuzisomaga tu
Maana nishanunua ving'amuzi viwili toka kujiunga na digital continental na star times
Na sina mpango wa kufuja tena pesa yangu kwa maving'amuzi
kwakweli hata mimi huu ubepari wa kila TV station kuwa na king'amuzi chake siutaki, ninacho kimoja tu habari nyingine nasikiliza kwenye radio na kusoma magazeti na mitandao.
 
Kuna kipindi ITV hawakukubali kujiunga na king'amuzi chao watu wakasema mbovu sana eti mzee Mengi mbinafsi na kashfa kibao kumbe walikuwa kwenye makubaliano na sasa ITV inapatikana Azam, ila azam kwa nini hajiungi na visimbuzi vya wenzake au naye ni mbinafsi?

Ingekuwaje azam abaki na kisimbuzi chake aoneshe habari yake, ITV wabaki na kisimbuzi chao cha digitek waoneshe habari zao, star tv wakabaki na continental yao wafanye mambo yao na ting pia. Azam angepata watazamaji wa kutosha kweli? Ajiunge na wenzake aache mbwewe huu si unga wa ngano bana.
 
Haita ka iwezekane. BBC wana mareporter kila pande ya dunia sasa wewe unazungunzia tv ambayo hata hapa bongo tuu kuna baadhi ya maeneo hawana ma reporter?
 
Yaani maana yake unasema azam wakae sawa na BBC world service you can't be seriously.
 
Wakalele kule...tutaendele kuwasikia kwenye ma-uzi tu......wajiongezi
 
Mleta mada naona unaleta utani, kituo ambacho hakina ma-reporter countrywide ukilinganishe na kituo chenye ma-reporter worldwide? Ubora wa Tv station siyo tu majengo, samani, vyombo vya matangazo pekee, kuna mambo mengi yanajumuishwa.
 
Back
Top Bottom