Napata hisia kuwa historia ya Azam inaweza kuishia kuwa tofauti na historia za Lipuli,Tukuyu Star,Mseto,Pamba,Mwadui,Reli,Balimi,Kariakoo Lindi,CDA,Mji mpwapwa,Nyota Korogwe na timu nyingine zilizowahi kutikisa anga ya mpira Tanzania. Kwa nini nasema hivyo? Jibu ni rahisi INFRASTRUCTURE ( miundo mbinu). Tofauti na vilabu vyote nilivyovitaja Azam wamewekeza kwenye miundo mbinu. Kumbuka wamiliki wa Bakhresa group they are shrewd business people,hawafanyi mambo ya kubahatisha na hawana historia ya kuchezea hela. They know what they are doing,usije shangaa siku moja wakauza mchezaji kwa dola milioni moja. Na kusema kweli this is the new African trend anatokea tajiri,anamiliki timu,anawekeza,timu inawika Africa na anaanza kuvuna hela.....mifano hai ni Libolo ya Angola na Tp Mazembe ya DRC. Enzi za community based teams kushamiri zinaanza kupotea,hata Kenya AFC Leopards wameunda study group ya kuangalia uwezekano wa kuuza hisa za club. Stay tuned mtaniambia.
Bravo Azam,kazeni buti,your future is bright.