Awareness: Uwapo safarini usikubali kula chakula cha kupewa na msafiri mwenzako

Mwanzo Shiza

Member
May 21, 2018
79
36
Siku za hivi karibuni ndugu yetu Dadi Mohamedi (49) na Omary Burian(27) wamekutwa na mkasa wa kuibiwa wakiwa wanasafiri kutoka Dar Mtwara na basi la Zungu. Imeelezwa kuwa waliibiwa vitu vyaombalimbali baada ya kula biscuti zinazoaminika kuchanganywa na madawa ya kulevya. Vijana watatu wanaodaiwa kuhusika na tukio hilo wamekamatwa na jeshi la polisi mkoa wa Lindi. wanaendelea na mahojiano. Na ndugu zetu waloibiwa wanaendelea na matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Lindi (Sokoine). Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali hiyo ameeleza kuwa afya zao zinaendelea vizuri. KWA TUKIO HILI TUJIFUNZE KUTOPOKEA NA KULA CHAKULA CHA KUPEWA NA WASAFIRI WEZETU.
 
NI KWELI MKUU MTU UNAPOKEAJE CHAKULA TOKA KWA MTU MLIOKUTANA TU NDANI YA MUDA MFUPI? TUJARIBU KUPUNGUZA TAMAA
 
Acha tuendelee kupokea tu watanzania watu safi sisi, tunapendana sanaa.
 
Bahat mbaya tu,
Me huwa nakula sana ila tu isiwe mayai ya kuchemsha na mahindi ya kuchemsha hayo ndio situmii
 
Kama mfukoni sina kitu, kwenye buti sina mzigo, nipo mimi tu na kiTecno naachaje kula rosti kuku ambayo nimekaribishwa,
 
Umakin unahitajika hapa, tusiamini watu kirahs jus because umekutana nae kwa safari na story zimematch. Huwez jua mtu ana lengo gan
 
Back
Top Bottom