kisugujira
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 774
- 200
WanaJF,
Ni nani anayebisha kuwa serikali ya awamu ya nne tayari imeishavunja rekodi na kujiwekea historia itakayodumu karne na karne kwa kuleta madiliko makubwa katika maisha ya kila siku ya mtanzania? Sasa hivi kuna tabaka kubwa kati ya waliyonacho na wasiyo nacho ukilinganisha na awamu zilizopita!
Waliyonacho wanatibiwa ughaibuni na wasiyo nacho wanatibiwa katika zahanati au hospitali chache zilizojengwa hapa nchini ambazo zimekithiri rushwa na wakati mwingine kukosa kabisa dawa zinazohitajika! Awamu hii ya nne itakumbukwa kwa kuijali elimu inayotolewa kwa watoto wa wakulima na wafanyakazi masikini ambao hawana uwezo wa kuwasomesha watoto wao katika shule za walionacho ambazo ada yake ni gharama sana!
Awamu hii ya nne itakumbukwa daima kwa kulipandisha hadhi daraja 0 kuwa daraja la 5 katika matokeo ya kidato cha nne hapa nchini!
Je wewe unafikiri ni vitu gani vingine vitakavyoifanya awamu hii ya nne ikumbukwe daima?
Ni nani anayebisha kuwa serikali ya awamu ya nne tayari imeishavunja rekodi na kujiwekea historia itakayodumu karne na karne kwa kuleta madiliko makubwa katika maisha ya kila siku ya mtanzania? Sasa hivi kuna tabaka kubwa kati ya waliyonacho na wasiyo nacho ukilinganisha na awamu zilizopita!
Waliyonacho wanatibiwa ughaibuni na wasiyo nacho wanatibiwa katika zahanati au hospitali chache zilizojengwa hapa nchini ambazo zimekithiri rushwa na wakati mwingine kukosa kabisa dawa zinazohitajika! Awamu hii ya nne itakumbukwa kwa kuijali elimu inayotolewa kwa watoto wa wakulima na wafanyakazi masikini ambao hawana uwezo wa kuwasomesha watoto wao katika shule za walionacho ambazo ada yake ni gharama sana!
Awamu hii ya nne itakumbukwa daima kwa kulipandisha hadhi daraja 0 kuwa daraja la 5 katika matokeo ya kidato cha nne hapa nchini!
Je wewe unafikiri ni vitu gani vingine vitakavyoifanya awamu hii ya nne ikumbukwe daima?