Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,769
- 10,650
Taarifa zilizothibitishwa ni kwamba kiongozi huyo wa Simba FC Aveva anashikiliwa polisi urafiki kwa tuhuma za rushwa. Anashikiliwa na TAKUKURU tangu juzi kwa tuhuma za rushwa. Hakuna ufafanuzi zaidi uliotolewa baada ya polisi na TAKUKURU kugoma kufafanua zaidi kwa sababu uchunguzi bado unaendelea.
Chanzo: Efm radio
==================
UPDATES:
Taarifa zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii zinadai kwamba, Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva anashilikiwa na Jeshi la polisi kwenye kituo cha Urafiki.
Aveva anashikiliwa na Polisi kwa bibali cha Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa TAKUKURU lakini bado haijafahamika moja kwa moja anakabiliwa na tuhuma gani.
Kamanda wa Mkoa wa kipolisi Kinondoni, ACP Chistopher Fuime amethibitisha kumshikilia rais wa klabu ya Simba na alipoulizwa ni tuhuma gani zinazomkabili kiongozi huyo wa juu kabisa wa wekundu wa Msimbazi alisema ni vizuri swali hilo wakiulizwa TAKUKURU.
“Kama unaweza labda ungewauliza watu wa TAKUKURU wanaweza wakajua ni lini uchunguzi wao utakamilika ni lini watampeleka mahakamani. Sisi tunamshikilia kwasababu TAKUKURU hawana mahabusu binafsi, vinginevyo wangekuwanae kule na wangejibu maswali yote ambayo wananchi wanataka kujua,” amesema Foibe kamanda wa Mkoa wa kipolisi Kinondoni wakati anahojiwa na kituo kimoja cha radio cha jijini Dar es Salaam.
“Tunamshikilia, yupo kwenye mikono salama. Sisi tunaendelea na uchunguzi wetu, sheria inaturuhusu kufanya uchunguzi tunaruhusiwa kukamata, kupekuwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu,” amesema Musa Milaba afisa habari wa TAKUKURU.
Chanzo: Shaffih Dauda
===============
UPDATES;
Asubuhi ya August 4 2016 taarifa zilianza kusambaa katika mitandao ya kijamii kuhusiana na Rais wa Simba Evans Aveva kutiwa mikononi mwa Polisi kutokana na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kuagizwa
kukamatwa kwa kiongozi huyo.
Millardayo.com ilifuatilia kwa kina kuhusiana na taarifa hizo na kufanikiwa kumpata kaimu afisa msemaji wa TAKUKURU Tunu Mleli na kuweka wazi kuwa kilichomfanya Rais wa Simba kukamatwa ni tuhuma za uchepushwaji wa pesa za usajili za mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo Emmanuel Anord Okwi kwenda Etoile du Sahel ya Tunisia.
“Ni kweli Aveva amekamatwa na polisi baada ya TAKUKURU kuagiza hivyo kutokana na tuhuma za rushwa zinazomkabili, tuhuma zinazomkabili ni uchepushwaji wa fedha kutoka account ya Simba kwenda katika account yake na baadae kuanza kufanyiwa mgawanyo katika account nyingine, ni fedha za usajili wa Okwi kutoka Etoile du Sahel”
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Emmanuel Okwi aliuzwa na Simba mwaka 2013 na kujiunga na klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia kwa ada ya uhamisho wa zaidi ya Tsh milioni 450, malipo yalicheleweshwa kulipwa hadi FIFA walipoingilia kati na mwaka huu malipo ndipo yalikamilika.
Chanzo: Efm radio
==================
UPDATES:
Taarifa zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii zinadai kwamba, Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva anashilikiwa na Jeshi la polisi kwenye kituo cha Urafiki.
Aveva anashikiliwa na Polisi kwa bibali cha Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa TAKUKURU lakini bado haijafahamika moja kwa moja anakabiliwa na tuhuma gani.
Kamanda wa Mkoa wa kipolisi Kinondoni, ACP Chistopher Fuime amethibitisha kumshikilia rais wa klabu ya Simba na alipoulizwa ni tuhuma gani zinazomkabili kiongozi huyo wa juu kabisa wa wekundu wa Msimbazi alisema ni vizuri swali hilo wakiulizwa TAKUKURU.
“Kama unaweza labda ungewauliza watu wa TAKUKURU wanaweza wakajua ni lini uchunguzi wao utakamilika ni lini watampeleka mahakamani. Sisi tunamshikilia kwasababu TAKUKURU hawana mahabusu binafsi, vinginevyo wangekuwanae kule na wangejibu maswali yote ambayo wananchi wanataka kujua,” amesema Foibe kamanda wa Mkoa wa kipolisi Kinondoni wakati anahojiwa na kituo kimoja cha radio cha jijini Dar es Salaam.
“Tunamshikilia, yupo kwenye mikono salama. Sisi tunaendelea na uchunguzi wetu, sheria inaturuhusu kufanya uchunguzi tunaruhusiwa kukamata, kupekuwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu,” amesema Musa Milaba afisa habari wa TAKUKURU.
Chanzo: Shaffih Dauda
===============
UPDATES;
Asubuhi ya August 4 2016 taarifa zilianza kusambaa katika mitandao ya kijamii kuhusiana na Rais wa Simba Evans Aveva kutiwa mikononi mwa Polisi kutokana na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kuagizwa
kukamatwa kwa kiongozi huyo.
Millardayo.com ilifuatilia kwa kina kuhusiana na taarifa hizo na kufanikiwa kumpata kaimu afisa msemaji wa TAKUKURU Tunu Mleli na kuweka wazi kuwa kilichomfanya Rais wa Simba kukamatwa ni tuhuma za uchepushwaji wa pesa za usajili za mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo Emmanuel Anord Okwi kwenda Etoile du Sahel ya Tunisia.
“Ni kweli Aveva amekamatwa na polisi baada ya TAKUKURU kuagiza hivyo kutokana na tuhuma za rushwa zinazomkabili, tuhuma zinazomkabili ni uchepushwaji wa fedha kutoka account ya Simba kwenda katika account yake na baadae kuanza kufanyiwa mgawanyo katika account nyingine, ni fedha za usajili wa Okwi kutoka Etoile du Sahel”
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Emmanuel Okwi aliuzwa na Simba mwaka 2013 na kujiunga na klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia kwa ada ya uhamisho wa zaidi ya Tsh milioni 450, malipo yalicheleweshwa kulipwa hadi FIFA walipoingilia kati na mwaka huu malipo ndipo yalikamilika.